MADA: Fahamu zaidi kuhusu mbinu za kilimo cha tikitimaji, faida na changamoto zake

MADA: Fahamu zaidi kuhusu mbinu za kilimo cha tikitimaji, faida na changamoto zake

mie nayajua matikiti kindaki ndaki lakini usilogwe kuvuna msimu huu wa nov..maana embe na nanasi zinakuwa nyingi..mtikiti mkubwa dalali anakuambia ataununua kwa 1200/=...khaa!kwanza nikiandika usk sitalala...!
 
Chukua wastani wa walioajiriwa na wakulima ni wapi wenye nafuu kimaisha? Ukipata jibu rudi hapa utoe mrejesho.
Really? Wewe kuanzia upate akili hilo tumbo lako tu pekee limekugharimu shilling ngapi mpaka umri huo ulionao? Au unakula vyuma?

Hakuna biashara inayolipa duniani kama ya chakula na kilimo ndio chakula, huwezi kusema eti kilimo ni hasara kisa ulilima bila kutumia akili vizuri.
 
Really? Wewe kuanzia upate akili hilo tumbo lako tu pekee limekugharimu shilling ngapi mpaka umri huo ulionao? Au unakula vyuma?

Hakuna biashara inayolipa duniani kama ya chakula na kilimo ndio chakula, huwezi kusema eti kilimo ni hasara kisa ulilima bila kutumia akili vizuri.

Kama kilimo kinalipa hivyo nini kinawafanya wakulima wawe masikini wa kutupwa?
 
Bora uigawanye, nusu kilimo na usilime tikiti soko lake lnasuasua ,au la uchanganye ulime tikiti kidogo na mazao mengne...alafu nusu ya pesa bora ufungue duka la vitu vya kike uvifate south africa utatoboa sana
 
Habari yenu,
Nadhani hapa kuna wataalamu wa kilimo, nimepata sehem nataka nilime matikiti maji kwa kuangalia nimeona ndo biashara inayolipa haraka haraka,

Mtaji nilionao wa kuanzia ni 20,000,000 naomba ushauri wenu juu ya hatua za kufuata,
Wekeza katika kilimo cha miwa ya Sukari ekari 10 tu,hiyo pesa unarudisha ndani ya miez 13 tu.
 
Kama kilimo kinalipa hivyo nini kinawafanya wakulima wawe masikini wa kutupwa?
Wakulima wapi unawaongelea wewe? Au kwako tafsiri ya mkulima ni ipi?

Viwanda vya sukari Tanzania vinaendeshwa na wakulima

Viwanda vya beer Tanzania vinaendeshwa na wakulima

Viwanda vya juice hali kathalika
Viwanda vya ngano?

Wewe umeseti mawazo yako kwa mlalahoi anaebangaiza pale kijijini na jembe la mkono ndio umemchagua awe role model wako kwenye sector ya kilimo hivi hiyo ni akili?

Kama wewe wa ulimwengu wa kileo unaishi maisha ya mababu zako walioishi ilimwengu wa giza, mjinga kati yako na wao ni yupi? Walikosa fursa za kufanya kilimo cha kisasa kwa technology and strategy za kisasa sababu ya ufinyu wa resources na sababu zenye mantiki kabisa, vipi wewe unaishi kwenye ulimwengu wa simplicity namna hii?

Wachina wanataka mihogo na kuna watu wanapiga mamilioni wanakucheka unavyolalama mitandaoni kulaani kilimo
 
REDEEMER.,
Unaongea nadharia wakati mimi naongelea uhalisia. Nitajie jina la kijiji wanachotoka wazazi/babu zako nikaone haya mawazo yako. Vinginevyo ww ni muuza sura kama wauza sura wengine.
 
Unaongea nadharia wakati mimi naongelea uhalisia. Nitajie jina la kijiji wanachotoka wazazi/babu zako nikaone haya mawazo yako. Vinginevyo ww ni muuza sura kama wauza sura wengine.
Unachobisha ni kwamba hakuna mkulima aliefanikiwa Tanzania hata mmoja au ni mimi sikuelewi?

Tanzania kuna tractors ngapi zinauzwa kwa mwaka? Unajua bei ya tractor?

Babu yangu alikua na John Deer kama saba hivi, usiongelee hekari za mikahawa, you must be dumb
 
USIKURUPUKE,hakikisha unapata mtu ambaye keshawahi lima ndo awe taa yako,usiweke pesa yote shambani hasa na eka moja tu,hakikisha hilo shamba una uhakika nalo


sio kupata mtu alolima tu mkuu

mimi nilikua nageuka pande zote 4 nipo na wataalam toka sua..nikafel..! tikiti sokoni bei zake utaweza lia...
 
kilimo pasua kichwa ni kama betting unless ufanye greenhouse kwa zao lenye masoko tayari ..
 
Usthubutu kuingiza kiasi kikubwa cha pesa kwenye biashara ambayo hujaifahamu bado. Max ingiza m3. Ikirudi ndio uingize nyingi zaidi.
 
Habari yenu,
Nadhani hapa kuna wataalamu wa kilimo, nimepata sehem nataka nilime matikiti maji kwa kuangalia nimeona ndo biashara inayolipa haraka haraka,

Mtaji nilionao wa kuanzia ni 20,000,000 naomba ushauri wenu juu ya hatua za kufuata,
Tenga milioni 3 nikupatie heka 30 huku Lindi tulime korosho wote tuwe majirani mwa shamba langu
 
Au nenda zambia au Malawi kaanzishe duka la nguo au bar itakulipa kuliko kuiwekeza nchini hiyo hela
 
Back
Top Bottom