Mada maalum kwa wanandoa

Mada maalum kwa wanandoa

Watoto Wana umri gani?
Kuna mmoja wa kiume ana miaka miwili na miezi mitatu, wa kike ana miezi mitatu (huyu hakutaka nijihusishe kumpa jina kabisa jina katoa yeye na ndugu zake jina nililotoa mimi yeye halitaki anataka mtoto aitwe jina la Bibi yake mzaa mama wakati huyu mtoto wa kiume aliniambia nisitoe jina la babu yaani la Baba yangu ila yeye sasa kampa jina la mama yake)
 
Yani rafiki yake MTU wa form four, na mshonaji hapo nimepata kujua uelewa wa mkeo jinsi ulivo mdogo, mda wote alificha makucha baada ya ndoa kayatoa
Mwenyewe hapa mpaka sasa najiuliza, kaficha makucha miaka minne ya uchumba, kashindwa kuyaficha japo miaka miwili ya ndoa?!!!
 
Huyu mkeo ni mwanamke mpumbavu mno hasa number 4 ka kubuhu au ulioa mwanamke wauswahilini maana duh ana akili za kushikiwa huyo mambo ya ndoa na majirani wapi na wapi
Huyu kalelewa na shangazi yake, baada ya kumshirikisha Dada yangu ( baada ya kumpa taarifa ajenda ya kikao ) akaniambia huyo hata shangazi yake aliyemlea na kumsomesha alikua akigombana nae, nikamuuliza kwa nini hukuniambia mapema kabla sijaoa, ye akanijibu kuwa aliona katulia na alishampa kitchen party kama mke mtarajiwa wa kaka yake
 
Hapo kwenye akili za kushikiwa hapo upo sahihi
Maana yeye akiona fulani anamfanyia mme wake hivi na yeye atataka kufanya, pia Bongo movie zimemuharibu sana, hajui kama wenzake wanaigiza na nia yao ni kufundisha kwamba wanayoigiza yanatokea katika jamii na hayafai kumfanyia mwenzi wako, hili yeye halijui
 
Hahaaa
Mimi kabla ya kuoa nilikuwa mtu wa out sana, so mwenzangu hakuwa kivile sana kwenye ishu za out, nikaona huyu atanifaa mana atanidhibiti kama si kunipunguzia ishu za out, we balaa lake baada ya yeye kuchoma ndani, yani siyo udhibiti ule wa speed governor ni hakuna tena ishu za out (mwaka sasa labda nidanganye safari ya kikazi), eti anasema ukisikia hamu ya kwenda out ingia jf mana hiyo ndiyo imekuteka akili.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Heheee mngekubaliana kuneutralize muweke like 1 day per week, as outing tamu Sana beans na Ina imarisha mahusiano
 
Mmh Mama Terry umo humu? Ni yule tunayemjua ama?
Hahaa yule yule, leten matatizo yenu yote niwape uzoefu, ndoa tamu Sana Kama kweli mlipendana tangu day one, sio ulipenda pesa ukifika ndan unazizoea unaanza kutafuta mambo yako.
Afu mjifunze kuneutralize interest zenu kwa kujali furaha pande zote, ongeen pamoja kwa kila Jambo na kubwa zaidi mkiweza kujua maisha yenu Ni yenu tu hayamhusu yeyote nje itakua poa Sana.
Na ndoa zenye furaha zaidi Ni watu wanaojua kipato Cha mwenzie, ujue ukificha anakufikiria unapata nyingi kumbe huna hata kumi.
Mjifunze pia kuwa na budget like % Fulani ya maendeleo, nyingine ya kula Bata na nyingine kila mtu atume kwao na other personal needs.
 
1. Alikua anataka kunitawala yaani yeye awe juu mimi niwe chini yake, yaani mimi niwe kama mwanamke na yeye awe mwanaume

2. Tendo la ndoa mpaka atake yeye au ajisikie

3. Jeuri na kiburi vyote vyake ana majibu ya hovyo yaani anaweza kunijibu anavyotaka kama anamjibu mwanae

4. Alikua anatabia ya kunikorofisha makusudi nikichukia ananisema vibaya kwa majirani na ndugu zake mwisho mimi naonekana mbaya ( HII NDIYO SABABU KUU ILIYOPELEKEA NIMUACHE )
Yaani naweza kusema yeye alikua akifurahi kuniona mimi nikiwa matatizoni maana kama kuna mtu ananidai basi yeye atasimama kidete utadhani yeye ndo anayenidai

5. Mbishi...ukimwelekeza kitu kwa nia ya kumwelewesha ye hataki anajiona mjuaji kwa kila kitu

Yaani yeye akishasema kitu ndo kasema hivyo anachotaka ni utekelezaji tu(FINAL SAY )

6. Hataki kusemwa au kukosolewa pindi anapokosea ( kuna kipindi alikua akionea watoto wa dada yangu kumbe wale watoto mmoja ambaye ni mkubwa alikua akiwaambia wazazi wake Baba na Mama ila wao walikua hawamwambii kwa kuhofia ataonekana hapendwi ila siku mtoto akaja kushtaki kwangu nikamchana kwamba anachokifanya sio kitu kizuri....AKANUNA HUYOOO...akaona haitoshi akajitenga yeye na mtoto wetu wa kwanza akawa anamtenga asicheze na wenzie, kuona hivi nikamwita tena kisha nikamwambia tena mbele ya Dada, alichosema dada ni kwamba hizo taarifa ye aliambiwa muda tu ila alishindwa kuniambia mimi kwa kuhofia nitaona anamchukia wifi yake )

7. Mbinafsi...Changu chake....chake ni chake hata kama mimi ndo nilipambana au nilifanikisha mpaka akakipata ila ni mwiko kunishirikisha...( Kuna kipindi alikua akifanya biashara flani sijawahi kushirikishwa kuhusu mapato wala nini yaani akimaliza biashara hela inafichwa hukooo...ila mimi nikirudi kazini nikitoka tu akawa anasachi mifuko ya suruali zangu ajue kuna pesa kiasi gani akikuta pesa, kesho yake ataanza kuniambia anadaiwa nikimwambia sina hela atanijibu zipo kiasi fulani kwenye suruali yangu yaani hata kama tayari ipo kwenye bajeti ya kodi ya nyumba ye atataka itumike anavyotaka yeye mwisho wa siku naanza kuhangaika peke yangu ye ananiangalia tu )

8. Anaigiza....yaani yeye anaishi ili kuwafurahisha majirani au watu, yupo tayari kwenda kumsaidia kazi jirani huku zilizopo ndani hakuzimaliza kisha baadae anaanza kulalamika kuchoka nikimwambia ananijibu mimi MSHAMBA WA MAISHA

9. Ameharibiwa na vipindi vya kwenye runinga hasa hivi vya kina Mama Terry bila kusahau na Bongo Movie

10. Anapenda kujionyesha....yaani anataka kuonekana yeye yupo juu kwa lugha nyepesi hataki kuishi katika uhalisia anataka kuonekana anaishi maisha fulani hivi ya hadhi ya juu

N.B;

KIPINDI CHA UCHUMBA TABIA HIZI SIKUWAHI KUZIONA MAANA NILIANZA NAE MAHUSIANO 2014 HADI 2018 MWISHONI NDO TULIFUNGA NDOA
Duuh pole Sana, huyo sio mke Ni shidaa Kama uloandika Ni kweli
 
Y: Una malengo, ndoto, mipango, matamanio yako ambayo unatamani uyatimize katika uhai wako.
Tabia, makuzi na malezi tofauti.

X: Vilevile na huyu ana malengo, ndoto, mipango, matamanio yake ambayo anatamani ayatimize au ayafikie katika uhai wake.
Tabia, makuzi na malezi tofauti.

SASA MNAKUTANA UKUBWANI ILU MUWE KITU KIMOJA, HAPA NDIYO MTIHANI ULIPO.
 
Hayo yote ni ya kweli hakuna hata moja nililomsingizia, ukipitia na comment zangu zilizotangulia zipo tabia zake nyingine ambazo hapo sikuziandika

Wakati nipo kwenye harakati za maandalizi ya ndoa nilijiambia huyu mwanamke sitamuacha mpaka nijue anachepuka

Lakini baada ya kukutana na tabia hizo ikabidi ninyooshe mikono juu maana nimefikiria mengi sana na kugundua kwamba nisipomuacha mwisho wangu utakua mbaya

Duuh pole Sana, huyo sio mke Ni shidaa Kama uloandika Ni kweli
 
Huyu kalelewa na shangazi yake, baada ya kumshirikisha Dada yangu ( baada ya kumpa taarifa ajenda ya kikao ) akaniambia huyo hata shangazi yake aliyemlea na kumsomesha alikua akigombana nae, nikamuuliza kwa nini hukuniambia mapema kabla sijaoa, ye akanijibu kuwa aliona katulia na alishampa kitchen party kama mke mtarajiwa wa kaka yake
Huyo hajielewi aisee shida huwa mnavutiwa na uziri wa nje na kusahau uzuri wa roho, tabia na kujielewa
 
Mkeo aliishia lasaba nini au ni slay quern anaweza kulea watoto vzuri?
Hapo kwenye akili za kushikiwa hapo upo sahihi
Maana yeye akiona fulani anamfanyia mme wake hivi na yeye atataka kufanya, pia Bongo movie zimemuharibu sana, hajui kama wenzake wanaigiza na nia yao ni kufundisha kwamba wanayoigiza yanatokea katika jamii na hayafai kumfanyia mwenzi wako, hili yeye halijui
 
Mkeo aliishia lasaba nini au ni slay quern anaweza kulea watoto vzuri?
Kaishia kidato cha pili

Kulea anaweza ila sasa huyu nna wasi wasi kichwani hazimtoshi, huyu mtoto wa miezi mitatu kaanza kumnywesha uji akiwa na miezi miwili,
Nikamuuliza kwa nini, akanijibu maziwa ya kunyonya hashibi ndo maana anasumbua analia mara kwa mara ( mtoto ni kibonge )
Nikamwambia kwa nini hukuniambia nitenge bajeti ya maziwa? Jibu hana

Kubwa kuliko mtoto akawa anamsumbua kunywa uji akataka kumpiga kibao...mtoto wa miezi miwili apigwe kweli, siku hiyo nilimuangalia tu na angempiga ningemrukia kichwa hicho sijui ingekuaje
 
Kuna mmoja wa kiume ana miaka miwili na miezi mitatu, wa kike ana miezi mitatu (huyu hakutaka nijihusishe kumpa jina kabisa jina katoa yeye na ndugu zake jina nililotoa mimi yeye halitaki anataka mtoto aitwe jina la Bibi yake mzaa mama wakati huyu mtoto wa kiume aliniambia nisitoe jina la babu yaani la Baba yangu ila yeye sasa kampa jina la mama yake)
Duh [emoji26] watoto wadogo sana
 
Kaishia kidato cha pili

Kulea anaweza ila sasa huyu nna wasi wasi kichwani hazimtoshi, huyu mtoto wa miezi mitatu kaanza kumnywesha uji akiwa na miezi miwili,
Nikamuuliza kwa nini, akanijibu maziwa ya kunyonya hashibi ndo maana anasumbua analia mara kwa mara ( mtoto ni kibonge )
Nikamwambia kwa nini hukuniambia nitenge bajeti ya maziwa? Jibu hana

Kubwa kuliko mtoto akawa anamsumbua kunywa uji akataka kumpiga kibao...mtoto wa miezi miwili apigwe kweli, siku hiyo nilimuangalia tu na angempiga ningemrukia kichwa hicho sijui ingekuaje
Kwanini ulioa mtu aliyeishia form two maana uelewa wake mdogo au ndo ile dhana huwa mna assume humu Jf kuoa asiye na shule ila akutii sasa madhara yake ndo haya, hapo nakupa pole umejifunga kitanzi kitakachokutesa the rest of ur life, yani anampa mtoto uji hajafikisha six month's the big problem ninayo ioana hapo mumepishana uelewa na vipaumbele mmoja mtu mzima mwingine hafikirii mbele hapo assume siku haupo duniani watoto wataishije, mumepeleke elimu ya watu wazima bila hivo atakuua Kwa pressure ikiwezekana usizae karibuni tena
 
Hahaa yule yule, leten matatizo yenu yote niwape uzoefu, ndoa tamu Sana Kama kweli mlipendana tangu day one, sio ulipenda pesa ukifika ndan unazizoea unaanza kutafuta mambo yako.
Afu mjifunze kuneutralize interest zenu kwa kujali furaha pande zote, ongeen pamoja kwa kila Jambo na kubwa zaidi mkiweza kujua maisha yenu Ni yenu tu hayamhusu yeyote nje itakua poa Sana.
Na ndoa zenye furaha zaidi Ni watu wanaojua kipato Cha mwenzie, ujue ukificha anakufikiria unapata nyingi kumbe huna hata kumi.
Mjifunze pia kuwa na budget like % Fulani ya maendeleo, nyingine ya kula Bata na nyingine kila mtu atume kwao na other personal needs.
Mama Terry niruhusu niweka mada maalum kwa ajili yako ujibu maswali ya wengi... Am sure kuna wengi wangetaka kujua mengi kuhusiana nawe... Waiting useme SU...
 
Back
Top Bottom