Mada maalum kwa wanandoa

Mada maalum kwa wanandoa

Wakistaafu ndipo akili huwasogea maana wake nao huchukua usukani na watoto
Mliooa mnakwama wapi? maana kila baharia nayemkuta na mchepuko bar,nikimuuliza kwa nini anachepuka utasikia ooo!!! mke wangu mjamzito,ooo!!mke wangu amejifungua,ooo!! mara mke wangu yupo siku zake mwezini,ooo!! mara mke wangu ana kelele sana, nyumbani hapakaliki,utasikia mara ooo!! mke wangu ameenza kuzeeka ili siwezi kumwacha sababu nimetoka nae mbali, mabaharia mnafeli wapi????? mabaharia nini kinawashinda kwenye ndoa???
 
Ni siku nyingine tena imepita, tumerudi salama majumbani mwetu, kuungana tena na wapendwa wetu, familia na watoto pia... Baadhi yetu hatujarejea, tuko mishe na viti virefu... Baadhi tuna sababu za msingi na nyumbani wanafahamu na tumewapa taarifa, wanatusubiri watupokee kwa upendo, kwa furaha kwa bashasha kuu

Baadhi hali ni tofauti, hatungependa kuchelewa nyumbani.... Tungependa tuwahi, tuungane na familia, tuimalize jioni kwa furaha kuu kabla hatujaungana kwa dinner na maombi ya usiku.... Lakini hali ni tofauti tunapoteza muda nje saa zisogee ili tukifika tu ni chakula kuoga na kulala... Tunakimbia kero na malumbano yasiyoisha
Ndoa haina furaha.... Ndoa haina amani, majuto ni mengi mno moyoni.. Kila mmoja anajutia kivyake... Hakuna upendo tena... Hakuna kuaminiana tena... Ni mwendo wa kutuhumiana na kuviziana.... [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]baba ana chumba chake.. Mama naye ana chake... Ama la chumba ni kimoja lakini kila mmoja ana kitanda chake...
Hakuna upendo, hakuna sharing, hakuna majadiliano ya changamoto, ya maumivu ya kushinda na kushindwa, ya kutiana moyo na kufarijiana... Kila mtu kivyake... Kila mtu na lwake... [emoji144][emoji144][emoji144][emoji144][emoji24][emoji17][emoji17][emoji17]

Karibuni wanandoa wote.. Ni mada ya kupeana faraja na kushare maumivu... Itambueni nguvu ya kuongea... Kuongea hupunguza maumivu mengi... Kupitia mada hii utajiona hauko pekeyako na pengine utaona kuwa kumbe wewe una nafuu kubwa ukisikia ya mwenzako. Jisikie huru ufunguke....
Funguka kwenye ndoa yako iliyoumizwa na kujeruhiwa sana, iliyotiwa vidonda na makovu ya kila aina
Ya usaliti
Ya kuchapiwa
Ya kusingiziwa
Ya kunenewa mabaya
Ya kudharauliwa kutukanwa na kudhalilishwa
Funguka upate nafuu
Funguka upate faraja
Funguka upunguze sumu mwilini
Funguka upate kupona sasa....
Karibuni wanandoa wote

Jr[emoji769]
Mi sijui ni asili yangu!
Naamini katika mfumo dume tu.
Hawa watetezi wa haki sawa ningekuwa na uwezo sio wawe na ofisi tu, hata kuonekana Tanzania ni kosa lingekuwa kwao. Namshukuru Mungu wala sijivuni kwangu mi mfalme flani hivi. Kumpa mke wangu nafasi sijui taanzaje, au anune tu ndani bila sababu haaaaaa! Bahati nzuri hata ukweni wanakubali yule Bw. ni mtata.
Kosa kubwa kwa sasa ni hali inayoonyeshwa wakati wa uchumba(fake), wanandoa wakisha halalishwa ndipo tabia halisi hujiweka wazi kwa wote(wanawake hasa) Lakini pia kupenda kupita kiasi husabisha kutokuonyana wanandoa (mume wajibika)
Ni kosa matatizo yenu yavuke chumbani( wanawake hawana dogo yashafika kwao)
Ushauri tu makofi mara 1 kwa miezi 2 nayo ni dawa, ili mke ajue kujishusha ni lazima kwake.
 
kwa upande wangu naona ndoa ni uvumilivu, na kikweli ili muweze kudumu lazima mmoja ajishushe, ila mkiwa wote juu lazima hamta dumu na ndoa itashambaratika, kuna kipindi inatokea mnakuwa na migogoro, mnalala kitanda kimoja ila hata salamu akuna hichi nikipindi kibaya sana.
Na kipindi hicho ndicho kusalitiana huwa ni rahisi sana
 
Kwani wanaume huwa hawana walio wapenda lakini hawakuwaoa?
Yan hakuna sekta ngum km ndoa...!!sema reason kuu naamini ni uvumiliv kukosekana...ndoa n uvumiliv

Kingne mwanamke anaolewa na juma wakat moyoni kuna rama!!.....yan ingkuwa mtu uloanza nae ndo unaoana nae ndoa ingkuwa tam saana

Ila unaoana na mtu mwenye network kibao lazma ulie...!!ukizima umeme mwenzio anawasha jenereta
 
1. Alikua anataka kunitawala yaani yeye awe juu mimi niwe chini yake, yaani mimi niwe kama mwanamke na yeye awe mwanaume

2. Tendo la ndoa mpaka atake yeye au ajisikie

3. Jeuri na kiburi vyote vyake ana majibu ya hovyo yaani anaweza kunijibu anavyotaka kama anamjibu mwanae

4. Alikua anatabia ya kunikorofisha makusudi nikichukia ananisema vibaya kwa majirani na ndugu zake mwisho mimi naonekana mbaya ( HII NDIYO SABABU KUU ILIYOPELEKEA NIMUACHE )
Yaani naweza kusema yeye alikua akifurahi kuniona mimi nikiwa matatizoni maana kama kuna mtu ananidai basi yeye atasimama kidete utadhani yeye ndo anayenidai

5. Mbishi...ukimwelekeza kitu kwa nia ya kumwelewesha ye hataki anajiona mjuaji kwa kila kitu

Yaani yeye akishasema kitu ndo kasema hivyo anachotaka ni utekelezaji tu(FINAL SAY )

6. Hataki kusemwa au kukosolewa pindi anapokosea ( kuna kipindi alikua akionea watoto wa dada yangu kumbe wale watoto mmoja ambaye ni mkubwa alikua akiwaambia wazazi wake Baba na Mama ila wao walikua hawamwambii kwa kuhofia ataonekana hapendwi ila siku mtoto akaja kushtaki kwangu nikamchana kwamba anachokifanya sio kitu kizuri....AKANUNA HUYOOO...akaona haitoshi akajitenga yeye na mtoto wetu wa kwanza akawa anamtenga asicheze na wenzie, kuona hivi nikamwita tena kisha nikamwambia tena mbele ya Dada, alichosema dada ni kwamba hizo taarifa ye aliambiwa muda tu ila alishindwa kuniambia mimi kwa kuhofia nitaona anamchukia wifi yake )

7. Mbinafsi...Changu chake....chake ni chake hata kama mimi ndo nilipambana au nilifanikisha mpaka akakipata ila ni mwiko kunishirikisha...( Kuna kipindi alikua akifanya biashara flani sijawahi kushirikishwa kuhusu mapato wala nini yaani akimaliza biashara hela inafichwa hukooo...ila mimi nikirudi kazini nikitoka tu akawa anasachi mifuko ya suruali zangu ajue kuna pesa kiasi gani akikuta pesa, kesho yake ataanza kuniambia anadaiwa nikimwambia sina hela atanijibu zipo kiasi fulani kwenye suruali yangu yaani hata kama tayari ipo kwenye bajeti ya kodi ya nyumba ye atataka itumike anavyotaka yeye mwisho wa siku naanza kuhangaika peke yangu ye ananiangalia tu )

8. Anaigiza....yaani yeye anaishi ili kuwafurahisha majirani au watu, yupo tayari kwenda kumsaidia kazi jirani huku zilizopo ndani hakuzimaliza kisha baadae anaanza kulalamika kuchoka nikimwambia ananijibu mimi MSHAMBA WA MAISHA

9. Ameharibiwa na vipindi vya kwenye runinga hasa hivi vya kina Mama Terry bila kusahau na Bongo Movie

10. Anapenda kujionyesha....yaani anataka kuonekana yeye yupo juu kwa lugha nyepesi hataki kuishi katika uhalisia anataka kuonekana anaishi maisha fulani hivi ya hadhi ya juu

N.B;

KIPINDI CHA UCHUMBA TABIA HIZI SIKUWAHI KUZIONA MAANA NILIANZA NAE MAHUSIANO 2014 HADI 2018 MWISHONI NDO TULIFUNGA NDOA
Kwanza nikupe hongera na pongezi nyingi kwa uvumilivu muda wote huo!
Mi huwa ni mwepesi mno kuvua mkanda!
 
Na siku apate tatizo yeye halafu mke azembee kidogo utasikia limwanamke lina roho mbaya linataka nife wakati yeye hajawahi timiza wajibu wake, zamani walikuwa na mafundisho mazuri ya ndoa, siku hizi watu wanajifundishia kwenye laptops
 
.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3],watu na ndoa zao shida tu,mimi sidhani kama nitaoa
Upweke
IMG-20191115-WA0077.jpeg
 
Hapana mkuu,mwanamke akiwa sahihi kwako na akakupenda kweli hakika ukimuonyesha upendo ndo utafurahi zaidi maana atakuona kama nuhu kwake
Tatizo lipo hivi unaweza kuta mke hana shida yeyote ila sasa muoaji hasomeki mambo huanzia hapo, wanawake huvumilia madhira mengi kuliko wanaume
 
Back
Top Bottom