Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

mkuu unaposema mafuta Super unamaanisha nini? fafanua hapo
 
Hata mimi jamani siwapati,hayo mafuta super ni yapi hayo?
 
Oxygen inaweza kufanya gari ile mafuta mengi kuliko kawaida au hewa nyingi iingie au kidogo iingie kwenye combustion chamber na hivyo kufanya iwe na low performance, kazi ya oxygen sensor ni kupima kiwango cha oxygen ambacho kinatoka kwenye exhaust system ikipima hicho kiwango taarifa huwa zinaenda kwenye ECU (electronic control unit) ambapo ndipo ina tasfiri ifanye nini,kama oxygen ipo nyingi kwenye exhaust system ina maana combustion haipo vizuri kwa hiyo ECU inaongeza hiyo ratio ya air to fuel and vice versa...itafikia kipindi gari yako itakuwa inachoma mafuta mengi kuliko hewa na hapo utaiona inaanza kutoa moshi mweusi tii,badilisha hiyo sensor na kawaida sensor huwa zinabadilishwa kila baada ya 100,000 km
 
Wakuu heshima kwenu.
Nina gx 110 ya mwaka 2001. Ukiwa kwenye speed zaidi ya 100 km/hr alafu ukakanyaga brake uskani unatetemeka. Speed inapopungua mpaka 80 km/hr usukani unatulia. Tatizo linaweza kuwa ni nini wakuu?
 
Wakuu nina Hillux 1995, ya petroli 1998cc niliagiza japan ikiwa na km 150,000. Bado iko katika hali nzuri sana, ila fuel consumption ni km 7.5 kwenye lami high way km 60 hadi 80 kwa saa, sijawasha a/c. Nimenda Bosch wakashauri nibadilishe fuel filter, badoo. Nifanyaje?
 

Fuata ushauri wao wako vizuri wale na kwa asilimia kubwa hawababaishi
 
Fuata ushauri wao wako vizuri wale na kwa asilimia kubwa hawababaishi

hahahaha mkuu kumbe na wewe bado unasujudia majina???

kwani Bosch ni wakinani hasa??
haya kwa utaalam wako wamemwambia abadilishe petrol filter.kabadili lakini bado ???.

shikamooo diagnosis machiney zimeharibu mafundi wengi sana aisee.na mm ilibakia kidogo niangukie huko aisee.nikaamua kutoitegemea kabisaa.

sasa hivi mafundi mmekuwa wazembe na wavivu sana ukimpa FUNDI Gari kama haiwaki TAA ya check engine basi ujue imekula kwako lazima atoke kapa hapo
 

acha ubahiri mkuu na usiwe unapuuza mambo.kama upo dar nitafute mm nitakufanyia bei chee hiyo sensor 40000 nakukufungia kabisa
 

acha ubahiri mkuu na usiwe unapuuza mambo.kama upo dar nitafute mm nitakufanyia bei chee hiyo sensor 40000 nakukufungia kabisa.

hata kama huna Hera nitakukopesha ila mpaka nijilidhishe na ulipaji wako uwe si mtata
 

Hapana LEGE nimezungumzia in general sense kwakuwa nimekuwa kwenye hiyo field muda mrefu ndio maana nikatumia neno 'at least '
 
Last edited by a moderator:
Toyota Sienta, taa ya check engine imewaka takriban wiki tatu sasa, pia gari ukianza kuondoka inajivuta kama ina sense obstacle mbele, yaani ukikamyaga mafuta inasita kisha inafumguka hata ukiachia, fundi amecheck na kubaini fuel filter imeziba kwa uchafu. Inakuwaje wakati ameisafisha ikawa sawa kwa wiki moja tu tatizo limejirudia, au nimelenga asiye adui?
Naomba ushauri wataalam.
 

Kwanza fuel filter huwa ni ya kubadili na si ya kusafisha hilo ni kosa pia checki na fundi aangalie gearbox
 
Mshana jr naomba kama unauzoefu wa gearbox za CVT unisaidie kuhusu service yake,,,yahn natakiwa kubadili hydrolic bahada ya km ngapi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…