Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

ISUZU (SUV) zote ni brand ni za kijinga tu . Bora kununua SANLG (Bodaboda) kuliko hizo ISUZU
 
Nakushauri usubiri mwezi August, September na Oktoba 2015 uwakodishie chama chochote cha siasa wapate gari la kupigia kampeni. wanasiasa wakizidiwa mambo wanakuwaga vipofu wala hawatahisi hizo gharama. Fedha utakayopata nenda kanunue Feroza, Harrier, Rav 4, Klugger, Suzuki grand Vitara au Prado kwa raha zako!!!
Mama mdogo naomba picha ya feroza
 
Mama mdogo naomba picha ya feroza

Oopps, ni Verossa siyo Feroza!! Usikonde, tazama hii hapa chini:
Verossa.jpg
 
Wadau hivi karibuni nimenunua ISUZU BIG HORN SUV ya mwaka 1998 imetembea 280,000 kms daah sasa nimeanza kutembelea inakula mafuta kama JINI MAHABA ya 1 ltr = 3kms yaani pamoja na kufungua vioo na kuweka FREE mara kibao imekuwa hatari. Najutaa kununua huu mgari na hela ya mkopo jamaa wa NMB ndo wameanza kukata mwezi huu
.Usifanye kosa kama langu mdau

Kaikatie bima kubwa (comprehensive), kisha waone wazee wa kubamiza, kisha weka miguu juu, popcorn pembeni ukisubiri bima wakulipe!
 
Mi Isuzu bora kwangu ni tipper tu.........nitapiga shughuli..........na hizo km kabisa ukanunua..........?.........bora uwape kuku tu watagie mayai..........au fuata ushauri wa kubadili engine.........
 
Nenda microfinance/SACCOS yoyote uiweke kama Dhamana wape na kadi original, chukua mkopo wa maana halafu tokomea jumla ubadilishe na simu, wao ndo watalipiga mnada wapate hela yao. DEAL CLOSED.

Huu ushauri nimeupenda.........
 
Mkuu Nenda Toyota watafute wale mafundi wapo vizuri sana kwenye hizo Cruiser unaongea nao watakufanyia kwenye karakana zao,ukishindwa Nenda keko garage pia wanazielewa vizuri sana cruiser


Mkuu N'yadikwa Toyota bei zao si mchezo!!!!

Wale ni shidaaaa akaulize asikie cost zake.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu N'yadikwa Toyota bei zao si mchezo!!!!

Wale ni shidaaaa akaulize asikie cost zake.

Mkuu Lusungo tofauti na hawa Toyota je naweza Pata wapi at least fundi mzuri wa kunitengenezea hiyo gari, nilichomwelewa mkuu N'yadikwa ni kuwa gari haitengenezwi chini ya mwamvuri wa Toyota bali ninakubaliana na fundi wa Toyota then kazi hiyo inafanyika kwenye gereji/eneo nje ya Toyota lakini na wataalam hao hao wa Toyota ,
Asante wakuu
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Lusungo tofauti na hawa Toyota je naweza Pata wapi at least fundi mzuri wa kunitengenezea hiyo gari, nilichomwelewa mkuu N'yadikwa ni kuwa gari haitengenezwi chini ya mwamvuri wa Toyota bali ninakubaliana na fundi wa Toyota then kazi hiyo inafanyika kwenye gereji/eneo nje ya Toyota lakini na wataalam hao hao wa Toyota ,
Asante wakuu


Yeah kuna Fundi Wa Toyota nimeona kaweka contacts zake kwenye Uzi flan hivi labda ufanye hivyo....

Kuna GARI nilitaka tengenezea hapo nilikimbia nikaipeleka njombe kwa wamisionari ikatibiwa swaafi kwa bei nzuri Sana.
 
Habari wana Jf, naomba ushauri kwa watalaamu wa magari, nataka kununua Nissani X-tail, vipi kuhusu ubora wake na kwa matumizi ya TZ hasa kanda ya kati ambako barabra si nzuri sana.
 
Mkuu nunua tu haina tatizo lolote. Mi nanayo mwaka wa tano sasa
 
Spea zake zinapatikana kwa urahisi? Na bei ya spea ikoje?
 
lakini nasikia ukitaka kuiuza huwa hainunuliki kwa urahisi
 
Habari wana Jf, naomba ushauri kwa watalaamu wa magari, nataka kununua Nissani X-tail, vipi kuhusu ubora wake na kwa matumizi ya TZ hasa kanda ya kati ambako barabra si nzuri sana.

mi sikushauri ununue hyo maana bodi yake ni plastic kbisa ukimgusa mtu kidogo sana ni majanga mchina huyo ni heri nunua harrier iko vizur na haipishani bei sana na xtrail yani hii gar kwa kweli ni heri harrier ni nzur imetulia hata used inauzka.
 
Back
Top Bottom