Mada maalumu ya picha za watu maarufu waliowahi kuwepo na waliopo duniani

Mada maalumu ya picha za watu maarufu waliowahi kuwepo na waliopo duniani

images (20).jpeg
images (19).jpeg


Julius Caesar maarufu kama Kaisari alikuwa ni mtawala wa kisiasa na kijeshi enzi za Warumi.

Anakumbukwa hasa kwa mafanikio mbalimbali yanayoonekana kuathiri dunia hadi leo.

Baadhi ya mafanikio hayo ni:

1.Kama kiongozi wa kijeshi aliteka Gallia (Ufaransa) na kuifanya jimbo la Kiroma. Kutokana na hiyo lugha ya Kifaransa na lugha nyingi kama Kireno, Kihispanyola n.k (kwa ujumla wake huitwa Romace languages) ni lugha zenye ukaribu sana na Kilatini, lugha ya Roma ya Kale.

2.Waroma wa Kale walimheshimu kushinda viongozi wote waliomfuata au kutangulia akatangazwa kuwa mungu.

Jina lake lilipata kuwa neno kwa ajili ya cheo cha watawala wa Kiroma waliomfuata. Kutokana na badiliko hilo la jina "Caesar" kuwa cheo, lugha mbalimbali zilipokea cheo hicho kama vile Kijerumani ("Kaiser"), Kirusi ("Tsar") na Kiswahili ("Kaisari" - kutokana na neno la Kijerumani).

3. Aliunda kalenda ambayo imekuwa msingi wa kalenda ya kimataifa leo (Kalenda ya Juliasi). Kwa heshima yake, mwezi wa saba unaitwa Julai.

4.Katika historia ya Roma yee ndie aliepelekea kufa kwa Jamhuri ya Roma (Roman Republic) na kuzaliwa Dola la Roma (Roman Empire) aliloliwekea misingi na lililotawala sehemu kubwa ya bara la Ulaya na Asia kwa miongo mingi.

Moja ya misemo (quotes) maarufu ya Kaisari ni pamoja na "Veni, Vidi, Vici" kwa Kiingereza "I came, I saw, I concured" kiswahili "Nilikuja, Nikaona, Nikashinda" huu msemo aliutumia katika ripoti yake ya vita baada ya kushinda vita iliyomchukua muda mfupi dhidi ya Pharnaces II wa Pontus.
 
George Stinney 1929-1944 aliehukumiwa akiwa na miaka 14 tu kwa kosa la kuwauwa wasichana wa kizungu wawili Betty (11) na Mary Emma 7 huko South Carolina USA

Kesi ya kijana huyo mweusi iliamuliwa na kuhusishwa na mauwaji kwa dakika 10 tu na kuamua auwawe kwa kiti cha umeme
Ni kijana mdogo kuwahi kuhukumiwa kifo
Alilazimishwa kukubali kuwa kauwa wakati sio yeye muuwaji
View attachment 1798710
Na miaka ya hivi karibuni ilikuja kuonekana kuwa hakuwa na hatia
 
View attachment 1798723View attachment 1798724

Julius Caesar maarufu kama Kaisari alikuwa ni mtawala wa kisiasa na kijeshi enzi za Warumi.

Anakumbukwa hasa kwa mafanikio mbalimbali yanayoonekana kuathiri dunia hadi leo.

Baadhi ya mafanikio hayo ni:

1.Kama kiongozi wa kijeshi aliteka Gallia (Ufaransa) na kuifanya jimbo la Kiroma. Kutokana na hiyo lugha ya Kifaransa na lugha nyingi kama Kireno, Kihispanyola n.k (kwa ujumla wake huitwa Romace languages) ni lugha zenye ukaribu sana na Kilatini, lugha ya Roma ya Kale.

2.Waroma wa Kale walimheshimu kushinda viongozi wote waliomfuata au kutangulia akatangazwa kuwa mungu.

Jina lake lilipata kuwa neno kwa ajili ya cheo cha watawala wa Kiroma waliomfuata. Kutokana na badiliko hilo la jina "Caesar" kuwa cheo, lugha mbalimbali zilipokea cheo hicho kama vile Kijerumani ("Kaiser"), Kirusi ("Tsar") na Kiswahili ("Kaisari" - kutokana na neno la Kijerumani).

3. Aliunda kalenda ambayo imekuwa msingi wa kalenda ya kimataifa leo (Kalenda ya Juliasi). Kwa heshima yake, mwezi wa saba unaitwa Julai.

4.Katika historia ya Roma yee ndie aliepelekea kufa kwa Jamhuri ya Roma (Roman Republic) na kuzaliwa Dola la Roma (Roman Empire) aliloliwekea misingi na lililotawala sehemu kubwa ya bara la Ulaya na Asia kwa miongo mingi.

Moja ya misemo (quotes) maarufu ya Kaisari ni pamoja na "Veni, Vidi, Vici" kwa Kiingereza "I came, I saw, I concured" kiswahili "Nilikuja, Nikaona, Nikashinda" huu msemo aliutumia katika ripoti yake ya vita baada ya kushinda vita iliyomchukua muda mfupi dhidi ya Pharnaces II wa Pontus.
Sio ndo huyu aliuliwa au nimeshaanza kusahau Roman law
 
Rais wa awamu ya 5 aliongoza nchi kwa miaka 5 na miezi 5. Kuna nini nyuma ya namba 5 kwa huyu bwana!
 
Rais wa awamu ya 5 aliongoza nchi kwa miaka 5 na miezi 5. Kuna nini nyuma ya namba 5 kwa huyu bwana!
Aligombea ubunge mara 5
1). 1990 - hakufauru
2). 1995 alishinda
3). 2000 alishinda
4). 2005 alipita bila kupingwa
5). 2010 alipita bila kupingwa.

Baada ya 1995 kupata uzoefu wa uongozi wa kisiasa katika ngazi ya unaibi waziri wa ujenzi, liapishwa kuwa waziri mara 5 kama ifuatavyo
1) 2000 chini ya Mkapa -Waziri wa Ujenzi
2)2005 Chini ya Kikwete - Waziri Ardhi
3) 2006 Chini ya Kikwete Waziri wa Uvuvi na maendeleo ya mifugo
4). 2008 Chini ya Kikwete Waziri wa ujenzi
5). 2010 Chini ya Kikwete Waziri wa ujenzi.
2). 2005.

Ukichunguza sana huenda ana watoto 5, nyumba 5 n.k.
 
George Stinney 1929-1944 aliehukumiwa akiwa na miaka 14 tu kwa kosa la kuwauwa wasichana wa kizungu wawili Betty (11) na Mary Emma 7 huko South Carolina USA

Kesi ya kijana huyo mweusi iliamuliwa na kuhusishwa na mauwaji kwa dakika 10 tu na kuamua auwawe kwa kiti cha umeme
Ni kijana mdogo kuwahi kuhukumiwa kifo
Alilazimishwa kukubali kuwa kauwa wakati sio yeye muuwaji
View attachment 1798710
Ngozi nyeusi tumetoka mbali na bado tu safarini! 🤔
 
Alikua anajulikana kwa jina la captain Derrick mkandala lufufu.

Huyu ndugu alikua Ni mtu anaetafsiri filam kutoka katika lugha yoyote kuja lugha ya kiswahili, Ni miongoni mwa watu wa kwanza kufanya kazi hio hapa nchini.

Ingawa wakati huu wapo watu wengi wanaofanya kazi hio, pamoja na kufariki kwake bado watu wengi wanamchikulia mfano wa kuigwa.
PIX1.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
David Livingston mwingereza kutoka Scotland, alikua ni mmisionari wa kikisto wa dhehebu la Kibatist aliefanya shughuli zake Africa.

Huko aliweza kugundua mengi ambayo hayakuwa yamegundulika na wazungu bado.

Huko aligundua pia biashara mbaya ya utumwa ambayo ilisababisha kufa kwa watu wengi.

Alikuja na hoja ya kukomesha utumwa Africa, kwamba ili utumwa uweze kukoma ilihitajika Africa kuletwe Ukristo, Africa kuletwe biashara, Africa kuletwe maendeleo.

Pengine mawazo yake yale ndio yanaishi Africa kwa Sasa.

Alifariki katika ardhi ya Africa na moyo wake ulizikwa Africa, na mwili wake uliandaliwa hapa Tanzania kule bagamoyo kwa Safari ya maziko huko ulaya mwaka 1873.
View attachment 1800599
 
Unapozungumzia umoja wa Africa hawa wazee hawataachwa kutajika.

Wazo lilianza kwa rais wa gana kwame nkrumah la kuunganisha. Watu wote wenye asili ya Africa popote walipo, pan-africanism.

Wazo liliungwa mkono kwa kwa kiasi kikubwa na baadhi ya viongozi wa Africa wakati huo akiwemo julias kambarage nyerere.

Nyerere alikuja na wazo kwamba ili umoja wa waafrica wote uwezekane ilitakiwa kwanza ziundwe jumuiya za kikanda ili Kuwezekana tamaduni zizoeleke, lugha zizoeleke nk.

Umoja huo uliundwa nchini Ethiopia, hii Ni kwa sababu Ethiopia ndio nchi pekee Africa ilioweza kuushinda ukoloni.
1767843182.jpg
 
Back
Top Bottom