Madaktari na wataalamu wa chakula, kwanini haishauriwi kuongeza chumvi baada ya chakula kuiva?

Madaktari na wataalamu wa chakula, kwanini haishauriwi kuongeza chumvi baada ya chakula kuiva?

agudev

Member
Joined
Apr 5, 2016
Posts
80
Reaction score
128
Hili swali nimekuwa nikijiuliza bila kuelewa, nimekuwa nikisikia majibu kama chumvi mbichi na chumvi iliyoiva, sielewi ni namna gani chumvi inaitwa imeiva wakati yenyewe ni kemikali.

Tuchukulie mifano hii:
  1. Nimepika maharage kilo moja bila kutia chumvi halafu nikaja kuongeza vijiko vitatu vya chumvi baada ya maharage kuiva na kuiacha kwa muda ili chumvi iyeyuke na kuenea kwenye maharage
  2. Nimepika maharage kilo moja na kuongeza chumvi vijiko vitatu nikaacha viive kwa pamoja

Je, kuna tofauti gani kati ya mapishi haya mawili ikiwa kiasi sawa cha chumvi kimewekwa kote na kimesabaa kwa uwiano sawia?
 
Kuongeza chumvi baada ya chakula kuiva haishauriwi kwa sababu inaweza kuwa hatari kwa afya yako...

Kwa kawaida, chumvi ina kiwango kikubwa cha sodiamu ambayo huyeyushwa na kuunguzwa pale inapochemswa..

kuongeza baada ya hapo hupelelekea mwili kupokea kiwango kikubwa cha sodium ambayo hupelekea kuongeza shinikizo la damu, na hii inaweza kuongeza hatari ya magonjwa ya moyo na mishipa ya damu, na pia magonjwa mengine kama kisukari...
 
Kuongeza chumvi baada ya chakula kuiva haishauriwi kwa sababu inaweza kuwa hatari kwa afya yako...

Kwa kawaida, chumvi ina kiwango kikubwa cha sodiamu ambayo huyeyushwa na kuunguzwa pale inapochemswa..

kuongeza baada ya hapo hupelelekea mwili kupokea kiwango kikubwa cha sodium ambayo hupelekea kuongeza shinikizo la damu, na hii inaweza kuongeza hatari ya magonjwa ya moyo na mishipa ya damu, na pia magonjwa mengine kama kisukari...
Naomba kupishana na wewe hapa mkuu, kusema kwamba chumvi ina kiwango kikubwa cha Sodium ni sawa na kusema maji yana kiwango kikubwa cha Hydrogen, Ili chumvi iitwe chumvi ni lazima iwe na Sodium kwa sababu ni mojawapo ya kitu kinaichotengeneza.
Kwani kuna chumvi yenye Sodium kidogo na chumvi yenye Sodium nyingi?
 
Kuongeza chumvi baada ya chakula kuiva haishauriwi kwa sababu inaweza kuwa hatari kwa afya yako...

Kwa kawaida, chumvi ina kiwango kikubwa cha sodiamu ambayo huyeyushwa na kuunguzwa pale inapochemswa..

kuongeza baada ya hapo hupelelekea mwili kupokea kiwango kikubwa cha sodium ambayo hupelekea kuongeza shinikizo la damu, na hii inaweza kuongeza hatari ya magonjwa ya moyo na mishipa ya damu, na pia magonjwa mengine kama kisukari...
Mkuu umemaliza kila kitu,,,uzi ufungwe.
 
Sio kwamba hairuhusiwi, hapana! ila ni "Haishauriwi" kufanya hivyo kutokana na maelezo yafuatayo:

Ukiweka chumvi wakati wa kupika chakula utafanya chumvi ienee vizuri katika chakula chako, hivyo kiwango cha chumvi itakayotumika kitakua ni kile tu kinachotakiwa kunogesha chakula chako hivyo mwili wako utapata kiwango kidogo cha chumvi.

lakini ukitumia chumvi ya kuongeza kidogo kidogo mezani wakati wa kula, itakufanya utumie chumvi nyingi zaidi ya inavyotakiwa
(Assume ukiwa unakula nyama isiyowekwa chumvi kabla ya kupikwa, kila wakati utakua unachovya chumvi ili usikie ladha si ndio?)

Hali hii itasababisha mwili wako kuwa na chumvi nyingi hivyo kukusababishia Magonjwa kama shinikizo la damu (Blood pressure and hpertension) na mawe ya figo (kidney stone)
 
Chumvi ipikwe/isipikwe ni chumvi ileile.

Ila tu wezekano wa kutumia chumvi nyingi zaidi unaongezeka ukiongezea chumvi mezani.

Ni afadhali kama kuna hisia ya chumvi kutokutosha kwenye mboga zilizopikwa, mtu aongezee kwenye chungu/bakuli la jumla. Ile ya kila mmoja kujiongezea si rahisi kuthibiti uwingi wa chumvi inayoliwa.
 
Back
Top Bottom