MzalendoHalisi
JF-Expert Member
- Jun 24, 2007
- 4,679
- 1,612
HIVI WANAVYOSEMA MTU HUYU AMUKULA CHUMVI NYINGI KUWA AMEISHI MIAKA MINGI WANADANGANYA? KULA CHUMVI KIDOGO NI KUISHI MIAKA MICHACHE??
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
kuna sodium ambayo ipo compact yaan element mbili zimeungana lakini unapoyeyusha chumvi maanake unavunja vunja zile element kuwa atom ndogo ndogoNaomba kupishana na wewe hapa mkuu, kusema kwamba chumvi ina kiwango kikubwa cha Sodium ni sawa na kusema maji yana kiwango kikubwa cha Hydrogen, Ili chumvi iitwe chumvi ni lazima iwe na Sodium kwa sababu ni mojawapo ya kitu kinaichotengeneza.
Kwani kuna chumvi yenye Sodium kidogo na chumvi yenye Sodium nyingi?
Mkuu, Nikueleze kwa Lugha nyepesi ya form two.Hili swali nimekuwa nikijiuliza bila kuelewa, nimekuwa nikisikia majibu kama chumvi mbichi na chumvi iliyoiva, sielewi ni namna gani chumvi inaitwa imeiva wakati yenyewe ni kemikali.
Hii unayoita chumvi "iliyoiva" ni chumvi iliyoyeyuka kwenye maji, unaweza ukachukua chumvi ukaikoroga kwenye maji na ikayeyuka bila kuipika.Mkuu, Nikueleze kwa Lugha nyepesi ya form two.
Chumvi mbichi (NaCl), ni ile Ikiwa haijawekwa kwenye kimiminika chenye Joto. Yaani ile kavukavu ya kunyunyizia.
Chumvi iliyoiva: Ni ile ikisha pikwa kwenye Chakula, Chumvi huwa ina break bond in Sodium na Chloride. Molecules za maji huwa zinavunja bond ya ions baina ya Sodium na Chloride. hivyo zinatoa huo muunganiko wake na kila mineral inakuwa inajitegemea.
REASON:
Mwili unakuwa vizuri zaidi endapo ukipokea Chumvi ikiwa imesha break bond(CHUMVI ILIYOIVA). Therefore. Kila mineral itafanya kazi yake separate mwilini.
Swali lako ndio jibu tatizo kujifanya mjuaji wa kuhoji.Chumvi ikiyeyushwa kwa kuchemshwa na ikiyeyuka bila kuchemshwa, ina tofauti gani kikemikali?
Kuhoji sio ujuaji, watu wengi wanaamini kwamba kuna kitu kinaitwa chumvi mbichi na chumvi iliyoiva kitu ambacho sio kweli.Swali lako ndio jibu tatizo kujifanya mjuaji wa kuhoji.
Kama hakuna chumvi mbichi na iliyoiva basi tusaidie, utafiti wako wa kisayansi unasemaje, ili sisi tusiojua, tuamini kwamba waliosema inayopikwa na chakula ndio inayofaa kiafya ni waongo.Kuhoji sio ujuaji, watu wengi wanaamini kwamba kuna kitu kinaitwa chumvi mbichi na chumvi iliyoiva kitu ambacho sio kweli.
Sababu inayoleta mashiko kuhusu kuongeza chumvi mezani baada ya kupika ni ile ya mchangiaji Superfly aliyesema kwamba inakuwa rahisi kuzidisha chumvi ikiwa unakula halafu kila tonge unasindikizia na chumvi, hii nafikiri ndio sababu inayofanya utumiaji wa chumvi kutoshauriwa baada ya mapishi.
Kwanza tuwekane sawa mwenzetu tupe matumizi yako ya chumvi.Nahitaji sababu, ukisema tu "chumvi mbichi haishauriwi" ina maana gani? Halafu kwanza chumvi inakuwaje mbichi?
Kwamba Sodium ikiunguzwa inayeyuka na kutoka kama mvuke?Kwa kawaida, chumvi ina kiwango kikubwa cha sodiamu ambayo huyeyushwa na kuunguzwa pale inapochemswa..
Mkuu Ionic bond kati ya Potassium na Iodine haiwezi kuvunjika kwa joto la nyuzi joto 100 centigrade.Kuna Chumvi na kuna chumvi ya mezani,(table salt),chumvi ya mezani ipo moja tu ambayo ni Sodium Chloride,lakini chumvi zipo za aina nyingi sana kutokana na muunganiko wa aina za ions.
kawaida chumvi ya mezani imeundwa na 4o% Na na 60% Cl,na vitu vingine vinavyoitwa "Additives" kama vile potasium iodide,sodium iodide na sodium iodate,huwezi ukaichukua chumvi yeyote ile ambayo imeundwa na sodium chloride na ukaiita "CHUMVI YA MEZANI",ili chumvi iwe na sifa ya kuitwa ya mezani ni lazima iwe na sifa mbili,mosi iwe ni Sodium Chloride,pili iwe na Additives.
kinachofanya chumvi ya mezani iwe na madhara kwa kiasi kikubwa ni hizo additives ambazo zinatakiwa ions zake zitenganishwe kwa kichochezi joto nje ya mwili ili kurahisisha usharabu wake katika mwili,
Ikumbukwe kuwa ions zikiwa zimeungana na kutengenez kampaundi basi ilikuivunja kampaundi hiyo kunaahitajika joto flani ambalo linatosheleza kuitenganisha kampaundi hiyo na katika muda flani.
sambamba na hilo hizi additives lengo lake kubwa ni kusupply IODINE ambayo huwezi kuipata ikiwa peke yake lazima iwe katika kampaundi,sasa ikitokea ukala chumvi ya mezani mbichi maana yake additive kampaundi inaenda tumboni kama ilivyo na ikifika kule uwezo wake wa kusharabiwa unakuwamdogo,kitu kinachopeleke mtokeo mapya ya kikemikli kati ya kampaundi hiyo na na nyinginezo ambazo badhi ya matokeo yake ya mwisho yakuwa na athari katika mfumo wa chakula(Tumbo,utumbo mpana na mwembamba),mfumo wa mkojo(Figo),na mfumo wa usafirisha(Moyo) kitu kinachoweza kupelekeamtokeoya kansa katika mfumo wa chakula kama Colon carcinoma,Kidney problems kama kidney stones ,na matatizo ya moyo kama pressure.
Tafiti zinaonesha kwamba chumvi ya mezani ambayo kitaalamu inaitwa "Doubly fortified" yaani ina additives za ain mbili ikiwemo additive yenye madini chuma ndani yake kama "Ferrous Furmarate" hiyo ndio inaathari kubwa sana,lakini hii inapaswa kutumikakwa makundi malumu maana huwa inaleng a kukabilina na upungufu wa iodine na madini chuma kwa ajilli ya damu hasa kwa watoto.
Namna ambavyo athari zake hutokea ni elimu nyingine,kwa ufupi nawasilisha.
Watu wengi wanadhani kula chakula chenye chumvi ndogo inamaanisha tu kutoongeza chumvi kwenye chakula chao wakati wa kula. DHANA HII SI SAHIHI. Chumvi unayopikia chakula na chumvi unayoongeza wakati wa kula ni kitu kile kile. Wanaposhauri tusiongeze chumvi wakati wa kula, mantiki ni kwamba tayari una chumvi ya kutosha iliyomo ndani ya chakula kilichoandaliwa, hivyo usiongeze zaidi. Haina maana kwamba chumvi ikichemshwa au ikipikwa inakuwa salama, madhara yake ni yaleyale sawa na ile ambayo haijachemshwa au kupigwa.Hili swali nimekuwa nikijiuliza bila kuelewa, nimekuwa nikisikia majibu kama chumvi mbichi na chumvi iliyoiva, sielewi ni namna gani chumvi inaitwa imeiva wakati yenyewe ni kemikali.
Tuchukulie mifano hii:
- Nimepika maharage kilo moja bila kutia chumvi halafu nikaja kuongeza vijiko vitatu vya chumvi baada ya maharage kuiva na kuiacha kwa muda ili chumvi iyeyuke na kuenea kwenye maharage
- Nimepika maharage kilo moja na kuongeza chumvi vijiko vitatu nikaacha viive kwa pamoja
Je, kuna tofauti gani kati ya mapishi haya mawili ikiwa kiasi sawa cha chumvi kimewekwa kote na kimesabaa kwa uwiano sawia?
Umedanganyika muda mrefu. Hauko sahihi. Chumvi ni chumvi tu. Punguza matumizi ya jumla ya chumvi.Mkuu, Nikueleze kwa Lugha nyepesi ya form two.
Chumvi mbichi (NaCl), ni ile Ikiwa haijawekwa kwenye kimiminika chenye Joto. Yaani ile kavukavu ya kunyunyizia.
Chumvi iliyoiva: Ni ile ikisha pikwa kwenye Chakula, Chumvi huwa ina break bond in Sodium na Chloride. Molecules za maji huwa zinavunja bond ya ions baina ya Sodium na Chloride. hivyo zinatoa huo muunganiko wake na kila mineral inakuwa inajitegemea.
REASON:
Mwili unakuwa vizuri zaidi endapo ukipokea Chumvi ikiwa imesha break bond(CHUMVI ILIYOIVA). Therefore. Kila mineral itafanya kazi yake separate mwilini.
je vipi kuhusu nyama choma ambayo haiwekwi chumvi wakati inachomwa?Sio kwamba hairuhusiwi, hapana! ila ni "Haishauriwi" kufanya hivyo kutokana na maelezo yafuatayo:
Ukiweka chumvi wakati wa kupika chakula utafanya chumvi ienee vizuri katika chakula chako, hivyo kiwango cha chumvi itakayotumika kitakua ni kile tu kinachotakiwa kunogesha chakula chako hivyo mwili wako utapata kiwango kidogo cha chumvi.
lakini ukitumia chumvi ya kuongeza kidogo kidogo mezani wakati wa kula, itakufanya utumie chumvi nyingi zaidi ya inavyotakiwa
(Assume ukiwa unakula nyama isiyowekwa chumvi kabla ya kupikwa, kila wakati utakua unachovya chumvi ili usikie ladha si ndio?)
Hali hii itasababisha mwili wako kuwa na chumvi nyingi hivyo kukusababishia Magonjwa kama shinikizo la damu (Blood pressure and hpertension) na mawe ya figo (kidney stone)
Very reasonable!! Na nimekuelewa vizuri,Sio kwamba hairuhusiwi, hapana! ila ni "Haishauriwi" kufanya hivyo kutokana na maelezo yafuatayo:
Ukiweka chumvi wakati wa kupika chakula utafanya chumvi ienee vizuri katika chakula chako, hivyo kiwango cha chumvi itakayotumika kitakua ni kile tu kinachotakiwa kunogesha chakula chako hivyo mwili wako utapata kiwango kidogo cha chumvi.
lakini ukitumia chumvi ya kuongeza kidogo kidogo mezani wakati wa kula, itakufanya utumie chumvi nyingi zaidi ya inavyotakiwa
(Assume ukiwa unakula nyama isiyowekwa chumvi kabla ya kupikwa, kila wakati utakua unachovya chumvi ili usikie ladha si ndio?)
Hali hii itasababisha mwili wako kuwa na chumvi nyingi hivyo kukusababishia Magonjwa kama shinikizo la damu (Blood pressure and hpertension) na mawe ya figo (kidney stone)