Madaktari wengi ni misukule walio hai

BICHWA KOMWE -

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2022
Posts
6,373
Reaction score
16,073
Nimetumia neno msukule kwa makusudi maalumu. Msukule sio tusi ni nomino, ni jina la mtu aliyetekwa nyara kiroho na kupotezwa kimazingara.

Kwanini madaktari ni misukule? Nitafafanua kwa ufupi na kwa kiwango kinachoeleweka.

Madaktari wengi akili zao zimefungwa minyororo, hawana wazo huru, wala hawana ujuzi huru. Wamebeba furushi la elimu ya kukaririshwa na kumezeshwa kama makinda ya bundi-mwitu.

Nikizungumza daktari, kwa muktadha wa kitanganyika, namaanisha watu wote wanaojiita wataalamu wa sayansi ambao kimsingi wala sio wataalamu, wengi wao wana diploma za D mbili kisha wakaunga unga mpaka Kairuki University au Bugandooh kisha wakavaa makoti meupe wakaanza kujiita madaktari na wanasayansi.

Kiukweli wako mbali sana na sayansi. Hawaijui wala hawaielewi sayansi. Ukimuuliza daktari wa kitanganyika kwanini kansa haina dawa anakwambia kansa haina dawa kwa sababu mabeberu hawajaleta chanjo.

Mfumo mzima wa daktari wa kitanganyika umejengwa katika muhimili wa kukariri na kusubiri maagizo ya mabeberu.

Beberu likiamuru kwamba kansa haina dawa basi ujue daktari wa kitanganyika hapindui meza. Ni mwendo wa kansa haina dawa hadi pale beberu litakapoamua vinginevyo.

Huu ni msukule wa kitanganyika katika mavazi meupe. Akili imefungwa minyororo ya chuma.

Corona ilituaibisha. Wanasayansi wetu wa kitanganyika walijificha uvunguni wakisubiri kuokolewa na mabeberu. Alhamdulillah mabeberu wakatutupia magunia ya chanjo tuyafakamie tupendavyo.

MY TAKE: Madaktari wote wafutiwe leseni zao wakawe wachimbaji wa kawaida wa mitaro ya barabara.
 
๐—ฆ๐—ฎ๐˜€๐—ฎ ๐—ต๐˜‚๐—ผ๐—ป๐—ถ ๐—ธ๐—ฎ๐—บ๐—ฎ ๐˜„๐—ฎ๐—ธ๐—ถ๐—ณ๐˜‚๐˜๐—ถ๐˜„๐—ฎ ๐—น๐—ฒ๐˜€๐—ฒ๐—ป๐—ถ, ๐˜‚๐˜€๐—ฒ๐—บ๐—ถ ๐˜„๐—ฎ๐—ธ๐—ผ ๐˜„๐—ฎ ๐—ธ๐˜„๐—ฎ๐—บ๐—ฏ๐—ฎ ๐—ป๐—ถ ๐—บ๐—ถ๐˜€๐˜‚๐—ธ๐˜‚๐—น๐—ฒ ๐—ถ๐—น๐—ถ๐˜†๐—ผ ๐—ต๐—ฎ๐—ถ ๐—ป๐—ฑ๐—ผ ๐˜‚๐˜๐—ฎ๐—ธ๐˜‚๐˜„๐—ฎ ๐—ฎ๐—ฝ๐—ฝ๐—น๐—ถ๐—ฒ๐—ฑ ๐—ธ๐˜„๐—ฎ ๐˜„๐—ฎ๐—ป๐—ฎ๐—ป๐—ฐ๐—ต๐—ถ ๐˜„๐—ผ๐˜๐—ฒ ๐—ถ๐—ธ๐—ถ๐˜„๐—ฒ๐—บ๐—ผ ๐—ป๐—ฎ ๐˜„๐—ฒ๐˜„๐—ฒ.?????
 
Kivipi?
 
Kimsingi kama taifa bado tupo nyuma, na sio afya tu ni kila sekta.

Na usiwaseme waliopitia diploma, maana MD wengi wametokea advance, na hao ndio waliofaulu sana lakini bado tupo hapo kama taifa.
 
Inaonyesha una dharau sana na taaluma za watu
Lakini inaonyesha taaluma hio unayoizungumzia huijui na wala haikuhusu ndio maana unaropoka ropoka tu
Misukule hutengenezwa kwa mifumo ya mwanga au mchawi ambaye ndio huendesha taratibu zote

Na kama umeona madaktari ni misukule basi wametengenezwa na serikali
Mikakati ya serikali kuboresha mafunzo kwa watoa huduma za Afya Tanzania inaionaje?
Vifaa vyenye teknolojia ya hali ya juu katika kugundua magonjwa na matibabu vipo?

Usiongee upumbavu na kukashifu watoa afya wakati ndugu zako , wewe na familia yako mnawategemea hao hao ambao mnawaona misukule
 
Namuona yule prof mwenye gubu akisoma hapa.

๐Ÿคฃ
 
Madaktari wa kukaririshwa hawana ubunifu zaidi ya kutegemea ubunifu wa wengine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ