"Made in China 2025" Mpango wa China wa kujitegemea kiteknolojia wafikia asilimia 88

"Made in China 2025" Mpango wa China wa kujitegemea kiteknolojia wafikia asilimia 88

Nchi iache kuendekeza siasa . Uelekeo wa dunia ya sasa ni ulimwengu wa sayansi na teknolojia
Uko sahihi. Hili ndilo jambo ambalo China wanalipambania sana sci-tech

Mara nyingi Xi kwenye hotuba zake anataka sana modernization ndani ya China na cross cutting technology

Na ndio kipaumbele chake tangu awe raisi
 
Pamoja na jitihada kubwa za Serikali, kuna jambo moja linahitaji TAMKO nalo ni ukosefu wa waalimu wa Hesabu/Saiyansi kwa shule za msingi na Sekondari wakati hayo masomo ndio yanaibeba China

Mfano; Shule za msingi na Sekondari hakuna waalimu wa Hesabu
Pengine waalimu waliopo wenye sifa ya kufundisha somo la hesabu shule za Msingi ni 8% ya mahitaji wakati kwa Sekondari pengine ni 20% ya mahitaji; Hiyo inakupa picha halisi kuwa hatuwezi kufika popote.....
Cha kushangaza waalimu wa ARTS wanafika pengine 98% ya mahitaji
Hili halina haja ya utafiti kwa kuwa KILA MWAKA WANAFUNZI WA SHULE ZA SERIKALI ZA MSINGI HUPATA ALAMA SIFURI KATIKA SOMO LA HESABU Pengine kwa asilimia 80% kitu ambacho ni hatari sana kwa maendeleo ya Nchi. Pengine ndio sababu hata kodi hazilipiki kwa kuwa, watu hawajui hesabu!

Unaweza kuona pia, wagunduzi wa kwetu kila pahala wengi wao ni wale ambao hawajasoma vizuri pengine walifeli kwa kukosa msingi wa Hesabu/saiyansi huko mashuleni kwa kuwa, hakuna waalimu.

Mimi nafikiri tuanzie hapo; TAMKO LITOLEWE kuongeza waaalimu wa hesabu wafike angalau 70% ; kilichopo sasa hivi ni aibu; mwalimu aliyepata sifuri kwenye somo la hesabu anafundisha hesabu!!!...

Lakini pia, wezi wa mali za uma watambulike kama wezi na sio kuwapa majina mepesi mepesi kama, wabadhirifu nk nk na hivyo kupelekea kupewa adhabu nyepesi nyepesi....Wachina hawana mchezo na wezi wa mali za umma!!!
 
SHIDA YA TANZANIA UNAFIKI UMEWEKWA MBELE NA UWOGA ULIOJAZWA
China hawaogopani na wala hawana unafiki

Wiki iliyopita kuna wakurugenzi wawili wamehukumiwa adhabu ya kifo kwa sababu ya rushwa

HIi imesaidia sana kuwe na nidhamu kwenye pesa za serikali China

20240605_192629.jpg
 
Pamoja na jitihada kubwa za Serikali, kuna jambo moja linahitaji TAMKO nalo ni ukosefu wa waalimu wa Hesabu/Saiyansi kwa shule za msingi na Sekondari wakati hayo masomo ndio yanaibeba China
Ndio maana ukiangalia hata viongozi wengi kwenye serikali ya China, Chinese leaders have engineering background
 
Nimesoma hii thread yote bila kupepesa macho. Huku nikiendelea kuombea na kutumaini siku moja Tanzania itapata mtu mwenye uwezo mkubwa, mwenye maono yanayoendana na kasi ya dunia na uwezo wa kutengeneza njia bora zitakazotufikisha huko. Mtu mmoja tu.

Na nikisema mtu mmoja sio utani. Bali namaanisha kwa asilimia 100%. Wanasema asiyejua Historia ame-destined kupotea. Ukiangalia history utagundua mapinduzi na matokeo yote makubwa yalisababishwa na kufanywa na mtu mmoja au wachache kwa ujumla wao. Ukianza kwenye Technology, Science, Vita, Siasa, Dini, Sanaa, Tamaduni, Kiuchumi, Maadili... nk.

Thomas Edison ndio mtu aliyekuja na taa ya umeme, Albert Einstein amekuja na Theory of Relativity iliyotengeneza Nuclear Bomb. Hitler alishawishi Taifa zima kuua watu million 20+. Muhammad na Christ wanashawishi Mabillioni ya watu mpaka leo. Michael Jackson anatambulika na kila mtu duniani na alisikilizwa na dunia nzima siku za uhai wake. Ni pattern inayojirudia over and over again.

Siku huyo mtu akitokea hapa Tanzania ndio siku tutatoka kwenye hili tope lililotugandisha kwa miaka zaidi ya 60 bila kwenda popote Economically wala Technologically. Wakati nchi tulizopatanazo uhuru zikiwa mbali nasi kwa millions of miles kila sekta.

Hahaha, kila navyozidi kuandika naanza kujishtukia nimegeuka fanatic wa prophecies na Messiahs. Now naanza kuwaelewa waFreemen wenye itiikadi kali. Lisan AL Gaib.
 
Kwa sasa kiuhalisia njia pekee ya kukuza uchumi wa Taifa ni Technology. Taifa kama Taifa linahitaji kuadapt kasi ya ukuaji wa Technology duniani. Kuanzia kwenye Education, Transportation, Communication, Agriculture, Economics na Public Infrastructures in general.

Lakini utahitaji viable, straightforward executable plan itakayotufikisha huko.

Maana yake Serikali itatakiwa kuwekeza kwenye vijana wa sasa hivi wenye uchu na Technology na kuja na long term plan juu yao. (If mtu mwenye akili hiyo angekuwepo.)
Ningesema Serikali iwekeze vyuoni. Lakini sio kweli. Vyuoni kumejaa watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri wenye ndoto za kujikwamua kimaisha binafsi kwa kupata ajira TCRA ili apate kufaidi vizuri yeye na familia yake. To hell mwananchi wa chini.

Hivyo kuwekeza vyuoni ni idea ya kipuuzi ya kumwagia kuku mchele. Kila mtu atagombania ale kivyake. Pia utekelezajia wa hiyo plan utakuwa ni mgumu, sababu hautoweza kujua kina nani wana akili gani, mawazo gani na nia gani kitaifa. Ni mchanganyiko mkubwa wa watu wenye background tofauti na viwango tofauti vya fikra na utambuzi.
Na watu wanaotakiwa ni wachache sana.

Hivyo basi, solution ni kuja na sehemu maalumu zitakazo kutanisha aina ya watu wanaohitajika. Watu wenye akili zenye udadisi, fikra chanya na mawazo mapya ya kutatua changamoto za aina zote. Watu wenye curiosity watakao discuss, think na ku-tear apart problems, find their nature and solve them. Kutatua changamoto kuanzia kwenye Military, Weaponry, Medicine, Engineering, Energy, Economics, Agriculture, Public infrastructures, Robotics, Software, Hardware na mpaka changamoto za chini kabisa za mwananchi wa kawaida.

Technology Hubs au kiufupi TechHubs. Ni sehemu zitakazokutanisha watu wa aina hiyo. Unaweza sema ni equivalent na Silicon Valley ukienda Marekani. Watu wenye nia kweli na uchu wa udadisi, innovations na inventions watakutana hapo. Sababu hakutakuwa na malipo bali pure passion na hunger ya kuona Taifa lako na akili yako ikitumika ipasavyo na kukutana na watu mnaofanana mitazamo. That's where Technologically Advanced Countries Emerge.

Mataifa makubwa na yanayojitambua mambo haya huwa mandatory ili kutunishiana misuli nani ni mbabe, lakini hapa kwetu tufanye kwa nia ya kujikwamua wenyewe.

Nalipa kodi. Na ni haki yangu kushauri Taifa litumie vipi kodi yangu effectively for the betterment of the entire country and future generations.
Serikali itenge maeneo makubwa na kujenga majengo makubwa yatakayo kutanisha watu wa aina hii. Kila jengo na niche yake. Iwe Engineering, Military, Weaponry, Medicine, Robotics, Public Infrastructures nk Hizi niche zitakuwa zikishirikiana na ku-collaborate kutafuta solutions za mambo mbalimbali.

Na watu watakuwa wanakuja na Ideas, Problems za kila aina constantly na kutafuta solutions na experiments constantly. Na either Serikali au Private Investors wataamua kuwekeza kwenye ideas na solutions kama ni viable na zenye potential kubwa kitaifa. Na vilevile Serikali itakuwa inatoa maagizo na maombi ya solutions juu ya Matatizo, Changamoto mbalimbali au kwa Kiingereza Problems zitakazotakiwa kutafutiwa solutions ASAP au Gradually.

Nitaandika Thread ndefu kiundani kule jukwaa la Intelligence na Siasa tuone kama Nchi yetu ina mtu au watu niliowasema.
 
'Made in China 2025'

Afrika tuna mengi sana ya kujifunza kutoka kwa China on how to set plans and goals and achieve them.
Kwa aina ya viongozi tulionao sidhani kama wanaweza kuja na mipango kama hii wakaisimamia na kufanikiwa. Viongozi wetu ni wasanii sana. Hawana wanachoweza kufanya zaidi ya kuomba omba ughaibuni.

Inavyoonekana Viongozi wa Tanzania (CCM) wanataka Tanzania iwe taifa tajiri (wealth country) kama zilivyo nchi za Gulf zenye mafuta na siyo ziwe developed country kama Korea Kusini. Ukiwaeleza haya mambo uliyoandika hawawezi kukuelewa
 
Back
Top Bottom