Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naikumbuka hii race, 2018 nadhani. H2R, F16 na Redbull RB9, wali race 400m. H2R alimzidi RB9 kwa 0.04 sec.Mkuu Mad Max mbona hiyo gari ya formula one ilikalishwa na kawasaki h2r ninja pale Uturuki?.
Mkuu una uchambuzi wa hali ya juu..
Ahahahah nimekipemda sana hiki kipande though hapo kwenye watu zaid ya 20 naona kama umekuza mambo chief.Tukirudi kwenye issue ya kubadirisha tyre, kuna team ya watu zaidi ya 20 ambao wanabadirisha tyre zote nne kwa chini ya sekunde 3 kushuka chini.
View attachment 3004059
.
Wewe ulio observer kuna wengine hawaonekani ni wale wanaoleta mataili kutoka ndaniAhahahah nimekipemda sana hiki kipande though hapo kwenye watu zaid ya 20 naona kama umekuza mambo chief.
Hapo nime observe;
Katika kila tyre kuna watu 3.
1. Aliyeshuka mashine ya kufungua tyre
2. Wa kuchomoa tyre
3. Wa kupachika tyre kisha yule aliye fungua ndiye anafunga tena kwa mashine.
So katika tyre 4 za gari hapo maana yale kuna watu 3x4= 12.
Halafu kingine nilicho observe hapo kuna watu wawil (2) kila ubavu wanaishikilia gari wakati zoezi la ubadilishaji wa tyres linaendelea.
So jumla ya watu hapo inakua kama 14 tu.
But all in all, uchambuzi mzuri, na haka ka kipengele kiukwel kamenifurahisha sanaa
Okay kama na hao wanahesabika kama wabadilishaji , sawa.Wewe ulio observer kuna wengine hawaonekani ni wale wanaoleta mataili kutoka ndani
Ooh nitacheki. Kwa nnavojua wanatumia unleaded gasoline sema ina high octanes. Na mwisho wa race kila team lazima ipeleke sample ya wese FIA wakacheki. Msije kua mmetumia mafuta mengine yakawasaidia kushinda.Alafu nasikia katika hii ya F1 kuna mafuta yanatoa transparency flame.
Yani unakuta dereva anaungua ila nyie pembeni hamuoni moto mpaka anaanza kupiga kelele .
Zungumzia hii ipoje mkuu
Mbona nasikia wanasema katika kitu very secret ni hayo mafuta kila kampuni wana kua na additive zao special.Ooh nitacheki. Kwa nnavojua wanatumia unleaded gasoline sema ina high octanes. Na mwisho wa race kila team lazima ipeleke sample ya wese FIA wakacheki. Msije kua mmetumia mafuta mengine yakawasaidia kushinda.
Shukrani mkuu. Si unajua wengine wapo off-camera. 😂😂😂 Ila umetisha.Ahahahah nimekipemda sana hiki kipande though hapo kwenye watu zaid ya 20 naona kama umekuza mambo chief.
Hapo nime observe;
Katika kila tyre kuna watu 3.
1. Aliyeshuka mashine ya kufungua tyre
2. Wa kuchomoa tyre
3. Wa kupachika tyre kisha yule aliye fungua ndiye anafunga tena kwa mashine.
So katika tyre 4 za gari hapo maana yale kuna watu 3x4= 12.
Halafu kingine nilicho observe hapo kuna watu wawil (2) kila ubavu wanaishikilia gari wakati zoezi la ubadilishaji wa tyres linaendelea.
So jumla ya watu hapo inakua kama 14 tu.
But all in all, uchambuzi mzuri, na haka ka kipengele kiukwel kamenifurahisha sanaa
Hapana uko sahihi. Ni matairi tu katikati F1 ndio mnafanana ila ikija issues ya wese, engine, gari, etc kila team mnajijua kikubwa kuwe na limitations ambazo mnatakiwa mzifuate hapo ndio FIA anapokuja kukagua.Mbona nasikia wanasema katika kitu very secret ni hayo mafuta kila kampuni wana kua na additive zao special.
Maana ukiacha ufanisi wa dereva pia engine na mafuta ni kitu ambacho kinaangaliwa sana kama source win..
Au ipo vipi mkuu naomba kukosolewa hapa
Shukran mkuuHapana uko sahihi. Ni matairi tu katikati F1 ndio mnafanana ila ikija issues ya wese, engine, gari, etc kila team mnajijua kikubwa kuwe na limitations ambazo mnatakiwa mzifuate hapo ndio FIA anapokuja kukagua.
Kwahiyo ata wese haina maana kwamba wanaweka adharani majibu, ila FIA wanachukua sample wanacheki lab kisha wanajiridhia kwamba ipo ndani ya standards zetu.
FIA tuwaite kama TBS flani hivi.
Mfano: Mercedes Benz nadhani wanatumia Petronas (sisi tunawaita Engen),Mbona nasikia wanasema katika kitu very secret ni hayo mafuta kila kampuni wana kua na additive zao special.
Maana ukiacha ufanisi wa dereva pia engine na mafuta ni kitu ambacho kinaangaliwa sana kama source win..
Au ipo vipi mkuu naomba kukosolewa hapa
Huu mchezo napendaga kuuangalia ila sijuiagi vzr..hii mada imenifunza kdg...sasa nitaangalia kwa maelezo haya Mkuu..Ahsante sanaWengi tunazijua gari zinazotumika kwenye mashindano ya FIA, especially ya Formula 1. Magari na team kama Ferrari, Mercedes Benz, nk yanaonesha uwezo wao.
Vile vile madereva wa hayo magari, kama Lewis Hamilton, Max Verstappen nk wakionesha ubabe nyuma ya steering.
Ukichukulia poa, utasema vile ni vigari tu vya kawaida. Ila hapana aisee. Na ukichukulia poa zaidi, utasema ata mimi wakinifundisha kuendesha ile gari, ndani ya week naweza kuendesha kwa speed kali. Hapana kwa kweli.
Tukumbuke, kama ilivyo FIFA na Football, basi FIA (Fédération Internationale de l'Automobile) wao wanasimamia sheria na taratibu zoote za aya mashindano kuanzia viwanja, magari, constructors (team) na madereva.
Tuanze na race yenyewe:
Hii ndio fastest racing cars duniani. Kila weekend magari 20 yakiwa na team 10 (kila team inatoa magari 2) yanashindana, na mwishoni washindi 10 wa mwazo wanapewa points, namba moja akipata 25 points, wa pili 18, watatu 15 ivyo ivyo zinashuka hadi wa 10 anapata 1. Izo point unakua unazikusanya kila mechi (kama Ligi kuu ya Mpira) na mwisho wa msimu mshindi ni mwenye point nyingi.
Mfano, hadi leo May 2024, msimamo wa F1 kwa upande wa madereva ni huu hapa chini:
View attachment 3003986
Na msimamo wa F1 kwa upande wa team (constructors) huu hapa:
View attachment 3003987
Kuna makombe mawili kwa pamoja yanatolewa kila msimu. La kwanza la Dereva na la pili la Constructor (team). Kwahiyo dereva wa team Ferrari mfano akishinda, anapata point zake. Ila kampuni linapata point kutoka kwa madereva wote wawili.
Hadi leo L Hamilton na M Schumacher ndio wanaongoza kwa kushinda makombe ya dunia mengi zaidi (7). Ila debate bado ni kali kua nani ni dereva mkali wa wote katik F1 history. Wengi wanaamini ni Hamilton, kwakua anasupportiwa na statistics. Na ndio ilipelekewa apewe official cheo cha SIR.
Hii racing inafanyika siku tatu, Ijumaa, Jumamosi na Jumapili. Ijumaa ni siku ya Practice. Hapa dereva anaujua uwanja kujua corners challenge etc.
Jumamosi kutengeneza Grid. Yes. Kama unavyoonaga mnavyoanza anakua yupo wa kwanza wa pili hadi wa 20. Inaitwa Grid. Hii inatengenezwa siku ya jumamosi, mnashindana aliefast ndio atakaa mbele. Ila mnavyoshindana kila mtu anarace against time sio against rival driver.
View attachment 3004007
Jumapili ndio race yenyewe. Mnajipanga kwenye formation (grid), then Green light, then off we go.
Zaidi ya nchi 34 zimewahi host F1 race, kwa Africa ni South Africa tu miaka ya 90 aliwahi host. Kuna uwezekano Zanzibar, Kenya, Rwanda waka host miaka ya karibuni.
Kuangalia hii race ya siku tatu sio bei ndogo, ni kubwa. Bei zinatofautiana kutokana na jukwaa na aina ya race, China GP ikiwa ndio cheapest kwa $200 kwa weekend nzima.
Gari lenyewe:
Gari la F1 ni la siti moja lenye open cockpit na open wheels, likiwa na injini nyuma na aerodynamics wings kwote mbele na nyuma. Haya magari yako fast na very powerful.
View attachment 3004046
Baadhi ya sifa inayoyafanya magari ya F1 yawe special ni:
Aerodynamics ndio kila kitu kwenye aya magari. Yana wings za kutosha zinazopeleka downward force hadi ya 750kg katika speed ya 160km/h.
View attachment 3004011 Sasa ukichukulia uzito wake na downward force inayotengeneza, F1 inaweza kuemdeshwa juu ya celling bora nyumba yako (T&C zitahusika).
View attachment 3004013
Uzito haya magari sio mazito. Uzito unapimwa kwa gari n dereva akiwemo.
View attachment 3003920
Haya magari hayana engine displacement kubwa. Mfano, kwa mwaka 2024 wanatumia 1.6L V6 Hybrid engine. Ila engine zao zinatoa power kubwa knm, mfano Redbull RB 17 engine inatoa 1200+ hp.
Hizi chuma zina accerelation kubwa sana. On average zinaweza kutoka 0-100km/h ndani ya 2.4 sec.
Breki zake ni hatari. Mfano ikiwa kwenye speed ya 200km/h inaweza kupiga breki hadi ikasimama ndani ya sekunde 3 tu, ikiwa inecover urefu wa 65 mita.
Hii braking inapelekea diski kupata joto hadi la 1000°C.
View attachment 3004016
Ingawa ni Manual transmission, ila miguuni ina pedal 2 tu. Breki na Accerelation. Clutch ipo kwenye paddle shifters.
Maximum speed ya F1 kwenye straight line ni 370+ km/h. Ila kwakua kuna kona nyingi, mara nyingi speed ya kawaida inakuaga 150-250km/h. Magari yanauwezo wa kukata kona hadi kwenye speed kali, ila Monaco wana kona kali ambayo dereva aliewahi kupita kwenye iyo kona kwa speed kali alikua na 48km/h tu.
Engine ya Corolla inaweza kudumu hadi kilometa 500,000 ila Engine ya F1 inadumu kilometa 1,500 hadi 2,000 tu. Kwahiyo baada ya race kadhaa wanabadirisha engine.
Hii gari ni gharama sana. Inakadiriwa kua na bei ya $12-18 Million. Steering wheel tu peke yake inazidi $50,000 na engine ndio inafika hadi $8 Million.
Tyre za F1 zinatengenezwa na kampuni moja ya Pirreli. Kuna tyre za aina nne, hard, medium, soft na wet. Soft tyres ndio zipo fast ila tatizo zinaisha haraka kwahiyo utakua unaenda kubadirisha mara kwa mara, na kubadirisha means unapoteza muda.
View attachment 3004043
Weekend nzima unapewa set 13 ya tyres utakazo zitumia kwenye practice, grid na race.
Tukirudi kwenye issue ya kubadirisha tyre, kuna team ya watu zaidi ya 20 ambao wanabadirisha tyre zote nne kwa chini ya sekunde 3 kushuka chini.
View attachment 3004059
Dereva
Madereva wa F1 lazima wawe na nguvu za kutosha, stamina na focus saaaaana.
Huu ni mchezo pekee ambao una mixed gender (kama nimekosea sorry). Kwamba anaweza akaendesha mwanamke au mwanaume. Yaani hakuna F1 for men na F1 for women. Ingawa wanawake sio mara kwa mara tunawaona kwenye mashindano, ni wanawake watano (5) tu ndio waliowahi kushiriki kwenye GP. Sijajumlisha test drivers.
Dereva anaweza kuresist G-force hadi ya 7G wakati wa kukata kona.
View attachment 3004028Pilots wa jet wamekua trained kuresist hadi 9G. Hii G force inatengezwa pale wakati gari ina ongeza au kupunguza mwendo (Accerelation au deaccerelation).
View attachment 3004025
Kwa lugha nyepesi, gari inavyoondoka unahisi kama kuna nguvu inakuvuta kwa nyuma, iyo ndio G Force. Kwahiyo 1G ni kama ukiwa tu umelalia mgongo kwenye kitanda au gari likiwa linaondoka kwa 10m/s². Likienda 20m/s² una experience 2G na kuendelea.
View attachment 3004029
Nashindwa kukueleza vizuri, lakini angalia effect ya G force katika headrest ya gari la Oliver hapa chini.
View attachment 3004032
Sisi wa kawaida tunaweza ishia 4-5G kwa sekunde chache sana. Ikizidi izo sekunde au Gs tunaweza zimia.
Kuna sheria ya uzito. Ukiwa umevaa suti full na helmet angalau uwe na uzito wa 80kg, ila urefu na ufupi ni nyinyi na team yako.
Madereva wa F1 wanaandaliwa tokea utotoni. Wanaanza Kart racing wakiwa watoto kabisa.
View attachment 3004003Mfano L. Hamilton alianza kart racing akiwa na miaka 8 tu. Na akiwa 10 alishinda British Kart Championship.
Pia Russell na Verstappen wameanza tokea watoto sana.
View attachment 3004004
Mbali na mazoezi ya mwili na mind, wanapractise kwenye simulators ambazo ni copy ya race kabisa. Hii inasaidia dereva ajue gari na barabara.
View attachment 3004002
Dereva akirace full race mfano kwenye GP ya Monaco, uwanja wake una urefu wa 3.3 km na mnafanya complete 78 laps, kwahiyo roughly mtakua mmecover distance ya 260km (kama umbali wa Bagamoyo to Tanga) na Charles Lecrec alitumia masaa 2 na dk 24 kukamilisha race, na huku Lewis Hamilton akiongoza kwa fastest lap kwa kutumia dk 1 na sec 14 kukamilisha mzunguko mmoja (wa izo km 3.3).
View attachment 3004006
Huu uwanja wa Monaco, izo namba ni kona.
Kwenye F1 haukai kwa starehe, unakaa kibabe sana.
View attachment 3004019 View attachment 3003982
Unakaa ivyo kwa takribani masaa 2, na inabidi uwe unanyanyua shingo ili uone mbele.
View attachment 3003983
Dereva anapoteza hadi kilo 2 hadi 3 za uzito akikamilisha race moja. Hii inatokana na excessive sweating.
View attachment 3003995
Gari ina AC ila kwakua ni open cockpit, AC haina ubaridi sana. Na ukichangia joto la battery na engine iliopo mgongoni kwako, unaiva.
View attachment 3003997
Mfano mwingine kwenye race ya Qatar 2023, joto lilikua 36°C kwenye uwanja, na ndani ya gari ilikua 56°C. Ilipelekea madereva kadhaa kutomaliza race na mwingine kutapika huku ana race.
Kwakua ligi za mpira zimeisha, ebu jaribu kufuatilia F1. Utapenda.
Sawa swa mkuu nimekupata sanaMfano: Mercedes Benz nadhani wanatumia Petronas (sisi tunawaita Engen),
View attachment 3005781View attachment 3005782Redbull wanatumia Exxon Mobil. etc kwahiyo supplier wa mafuta ataweka "secret" additives kama ulivosema ila iwe ndani ya limitations za FIA