Madereva wa mikoani, tabia na utaratibu wa kupaki mabasi sehemu ya chakula chenye bei juu mnaumiza abiria wenye kipato kidogo

Madereva wa mikoani, tabia na utaratibu wa kupaki mabasi sehemu ya chakula chenye bei juu mnaumiza abiria wenye kipato kidogo

Safari ya ndege hata haina raha,ni huo unyama wa madereva tu na tamaa zao.
Ila kupanda Bus mpite mahali mpige menyu safi huko njiani mnapita,mikumi,gangilonga mafinga, huko kote vijijini raha tupu kuangalia yale mazingira.
Hii tabia ya kusema dk 10 ushuke,foleni ya chakula,ule,kwenda chooni ni unyama.
Safari ya basi, ni utalii pia, Abiria wafurahie safari yao, Siyo kupelepelekwa mputa mputa.
 
Zamani kuna njia ya Mtera pale bwawani magengeni,ile njia sidhani km kuna hotel maalum bus lisimame.
Bus ngoma ikizimishwa ipoe kuna magenge pale unakuta mpunga Samaki km wote maharage,kabichi ,mchicha ndo vinaipuliwa.
Mnakula kwa pozi hadi gari ipoze engine mshashiba.
Safari inaanza tena
 
Serikali yetu - mamlaka husika tunaomba mtusaidie sisi wanyonge na hii tabia ya madereva inayozidi kushamiri kila kukicha, hasa kwa wale ndugu zetu wanaosafiri mikoa ya mbali wanapata tabu sana kuhusu masuala ya chakula.

• Dar - - Mwanza
• Dar - - Mbeya
• Dar - - Kigoma
• Dar -- Arusha
• Dar -- Ruvuma

Kuna tabia na utaratibu wa mabasi waliojiwekea bila kuhofia abiria wao, sio rafiki kabisa, wanapaki mabasi yao sehemu ya chakula bei zao ziko juu sana bila kujali abiria mifukoni mwao/kipato walichonacho. Karibia vituo vyote wanavyopaki hawa madereva unakuta Chakula cha bei ya chini ni kuazia elfu Tsh7000/- hadi elfu Tsh 8000/- na kuendelea, na ukiangalia hicho chakula hakina hadhi ya kuuzwa bei kwa hiyo, halafu chakula kinakuwa ni kidogo ikiwa mtakuwa watu wawili hamuwezi kushiba.

Jana nilikuwa natoka Dar kuja Mbeya tulipofika sehemu ya chakula, niliongozana na mama mmoja mwenye watoto wa 3 alivyoambiwa chakula bei ya mwisho ni elfu Tsh7000 alikuwa mnyonge sana, na kiasi alichokuwa nacho taslimu alikuwa na elfu Tsh5000 tu, ikambidi anunue soda na biscuit, roho iliniuma sana.

1. Madereva mnadhani kila mtu anapesa ya kununulia hicho chakula cha bei ya juu?

2. Au sehemu mnazopaki kwa ajili ya watu kula ni za viongozi wa ngazi za juu huko serikalini


Ombi langu kwa Serikali tunaomba mtoe tamko/sheria kwa mabasi yote, yawe yanasimama kwenye mji ulio na huduma kamilifu ili abiria wote wapate huduma stahiki
Madereva na wahudumunwao wanakula free chochote wanataka.
 
Zamani kuna njia ya Mtera pale bwawani magengeni,ile njia sidhani km kuna hotel maalum bus lisimame.
Bus ngoma ikizimishwa ipoe kuna magenge pale unakuta mpunga Samaki km wote maharage,kabichi ,mchicha ndo vinaipuliwa.
Mnakula kwa pozi hadi gari ipoze engine mshashiba.
Safari inaanza tena
😀😀, Njia ya mtera Bado hakuna hotel mkuu, ila kuna kituo, basi huwa zinasimama, mama ntilie wanapika wali, pilau, samaki wakukausha, Ni maeneo rafiki sana.
 
hili ndilo tatizo kubwa la Tanzania hakuna mtanzana ana upendo na mwenzake na ukiwepo ni wa kinafk au kimaslay! kama wewe unacho usimkebei asiye nacho!
Sasa chukulia huyo ndo amepata kuongoza mamlaka fulani 😟,, Wananchi watateseka milele.
 
Madereva na wahudumunwao wanakula free chochote wanataka.
Hata kama mkuu, kile kitu haifai kabisa, Madereva anaweza kula popote pale au akapewa posho zuri kabisa Kulingana na sehemu aliyo paki basi,
 
Madereva sio wa kulaumiwa kwasababu nao hufuata tu maelekezo sio maamuzi yao. Ila watanzania tuna upumbavu wa kupoteza sana muda. Safari ya masaa 8 huwa inafika zaidi ya masaa 10 kwa sababu ya huu ujinga wa kusimama muda mrefu kula. Ingekuwa amri yangu gari zingekuwa zinasimama stendi tu kushusha na kupakia... yaani safari ni mchakamchaka. Kusema washushe bei ni ngumu sana kwasababu hao wanategemea abiria tu kwenda kula kwahiyo wakishusha wanaweza kutomudu gharama za uendeshaji.
 
Madereva sio wa kulaumiwa kwasababu nao hufuata tu maelekezo sio maamuzi yao. Ila watanzania tuna upumbavu wa kupoteza sana muda. Safari ya masaa 8 huwa inafika zaidi ya masaa 10 kwa sababu ya huu ujinga wa kusimama muda mrefu kula. Ingekuwa amri yangu gari zingekuwa zinasimama stendi tu kushusha na kupakia... yaani safari ni mchakamchaka. Kusema washushe bei ni ngumu sana kwasababu hao wanategemea abiria tu kwenda kula kwahiyo wakishusha wanaweza kutomudu gharama za uendeshaji.
Ingekuwa amri yangu gari zingekuwa zinasimama stendi tu kushusha na kupakia, yaani safari ni mchakamchaka
Mkuu safari siyo ubabe, safari ni utalii, safari iwe yenye amani, safari iwe salama ili kuhakikisha abiria wote wanafika salama sehemu husika.

Kusema washushe bei ni ngumu sana kwasababu hao wanategemea abiria tu kwenda kula kwahiyo wakishusha wanaweza kutomudu gharama za uendeshaji.
Yaweza kuwa upo sahihi au la! Kuuza sahani ya wali 5000, 7000, 8000 unaona sahihi,? Labda chakula ingekuwa cha maana kidogo kuhusu ubora, lakini ukiangalia chakula ni cha hovyo kupita kiasi,
 
😀😀, Njia ya mtera Bado hakuna hotel mkuu, ila kuna kituo, basi huwa zinasimama, mama ntilie wanapika wali, pilau, samaki wakukausha, Ni maeneo rafiki sana.
Kaka umepita lini njia hiyo. Pale Mlowa kuna jamaa wamejenga hotel nzuri tu za bei za kuruka
 
Tafuta tuu hiyo afu nane, watu wameshalamika sana, ila ukumbuke cheap is expensive... Utauziwa afu tatu kilomita mbili nyingi tumbo linaanza kuvuruga
Muongo wewe hakuna mahali wanauza vyakula au hasa hayo maziwa yaliyolala kama kwenye hizo hotel za Mabasi.
Sikia...kuna siku nilikunywa Maziwa sehemu flani njia ya Singida huko,ila kabla sjamaliza nikagundua yanamushkeli nikauchubua,sema nilikuwa nshachukua namba ya huyo mdada ili nimtongoze,Baada ya Muda tushafahamiana yule demu alinambia huko uwa hawamwagi kitu labda kiwe kimeharibika sana.
 
Mkuu safari siyo ubabe, safari ni utalii, safari iwe yenye amani, safari iwe salama ili kuhakikisha abiria wote wanafika salama sehemu husika.


Yaweza kuwa upo sahihi au la! Kuuza sahani ya wali 5000, 7000, 8000 unaona sahihi,? Labda chakula ingekuwa cha maana kidogo kuhusu ubora, lakini ukiangalia chakula ni cha hovyo kupita kiasi,
Umeshawahi fikiria gharama za uendeshaji wa hizo hoteli? Pale wanakula abiria tu. Hakuna mwananchi wa maeneo yake atathubutu kwenda kula pale. Vinginevyo stendi za mabasi ziwe na migahawa inayoweza kutoa huduma bora. Stendi zikiweza kuwa na hoteli kama 3 zitafanya kuwe na ushindani na walaji kunufaika. Kinyume na hapo kilio kitaendelea.
 
Umeshawahi fikiria gharama za uendeshaji wa hizo hoteli? Pale wanakula abiria tu. Hakuna mwananchi wa maeneo yake atathubutu kwenda kula pale. Vinginevyo stendi za mabasi ziwe na migahawa inayoweza kutoa huduma bora. Stendi zikiweza kuwa na hoteli kama 3 zitafanya kuwe na ushindani na walaji kunufaika. Kinyume na hapo kilio kitaendelea.
Umeshawahi fikiria gharama za uendeshaji wa hizo hoteli?
Swali fikirishi 🤔,


Hakuna mwananchi wa maeneo yake atathubutu kwenda kula pale
Kwa nini watu wa kawaida hawaendi kula hayo maeneo ?

Vinginevyo stendi za mabasi ziwe na migahawa inayoweza kutoa huduma bora
Hii ilikuwa inafanyika tangu mwanzo, lakini mamlaka ziliwatimua kufanya biashara ya migahawa maeneo ya stendi.( uongozi wa hovyo)

Stendi zikiweza kuwa na hoteli kama 3 zitafanya kuwe na ushindani na walaji kunufaika.
Hii jibu ni zuri, tatizo wanaojenga hotel wanawekeza mbali na stendi, kwa sababu wanajua kabisa biashara yao ni ya kiwango cha chini hivo abiria hawatanunua chakula kwenye hotel zao,
 
Serikali yetu - mamlaka husika tunaomba mtusaidie sisi wanyonge na hii tabia ya madereva inayozidi kushamiri kila kukicha, hasa kwa wale ndugu zetu wanaosafiri mikoa ya mbali wanapata tabu sana kuhusu masuala ya chakula.

• Dar - - Mwanza
• Dar - - Mbeya
• Dar - - Kigoma
• Dar -- Arusha
• Dar -- Ruvuma

Kuna tabia na utaratibu wa mabasi waliojiwekea bila kuhofia abiria wao, sio rafiki kabisa, wanapaki mabasi yao sehemu ya chakula bei zao ziko juu sana bila kujali abiria mifukoni mwao/kipato walichonacho. Karibia vituo vyote wanavyopaki hawa madereva unakuta Chakula cha bei ya chini ni kuazia elfu Tsh7000/- hadi elfu Tsh 8000/- na kuendelea, na ukiangalia hicho chakula hakina hadhi ya kuuzwa bei kwa hiyo, halafu chakula kinakuwa ni kidogo ikiwa mtakuwa watu wawili hamuwezi kushiba.

Jana nilikuwa natoka Dar kuja Mbeya tulipofika sehemu ya chakula, niliongozana na mama mmoja mwenye watoto wa 3 alivyoambiwa chakula bei ya mwisho ni elfu Tsh7000 alikuwa mnyonge sana, na kiasi alichokuwa nacho taslimu alikuwa na elfu Tsh5000 tu, ikambidi anunue soda na biscuit, roho iliniuma sana.

1. Madereva mnadhani kila mtu anapesa ya kununulia hicho chakula cha bei ya juu?

2. Au sehemu mnazopaki kwa ajili ya watu kula ni za viongozi wa ngazi za juu huko serikalini


Ombi langu kwa Serikali tunaomba mtoe tamko/sheria kwa mabasi yote, yawe yanasimama kwenye mji ulio na huduma kamilifu ili abiria wote wapate huduma stahiki
Halafu kuna tatizo lingine, kwamba...

Mkishakaribia hotelini, wanatangaza kwamba muda wa kuchimba dawa na chakula ni dakika 10. Kumbuka kwamba kwa msongamano wa kwenye bus, wale wanaokaa siti za katikati au nyuma, hadi wafanikiwe kushuka unakuta wameshatumia dk 5 tayari.

Technically, hadi wakachimbe dawa na wanunue chakula basi wanakuwa wameshatumia dakika zaidi ya 10, this is very unfair.

Inabidi wajirekebishe kwenye hilo swala la muda pia, kwa kuwazingatia back benchers.
 
Swali fikirishi 🤔,



Kwa nini watu wa kawaida hawaendi kula hayo maeneo ?
Kwasababu hawamudu bei.


Hii ilikuwa inafanyika tangu mwanzo, lakini mamlaka ziliwatimua kufanya biashara ya migahawa maeneo ya stendi.( uongozi wa hovyo)
Ulikuwa ni uamuzi wa hovyo sana. Na sio stendi tu hata pale Airport vitu ghali sana mgahawani. Yaani chakula ni bei rahisi ukiwa Dubai Airport kuliko JK Nyerere airport Dar.

Hii jibu ni zuri, tatizo wanaojenga hotel wanawekeza mbali na stendi, kwa sababu wanajua kabisa biashara yao ni ya kiwango cha chini hivo abiria hawatanunua chakula kwenye hotel zao,
 
Ulikuwa ni uamuzi wa hovyo sana. Na sio stendi tu hata pale Airport vitu ghali sana mgahawani. Yaani chakula ni bei rahisi ukiwa Dubai Airport kuliko JK Nyerere airport Dar.
😀😀, Kauli ya wazee, Waafrika watauana wao kwa wao, kwa sababu ya ukosefu wa maarifa.
 
Halafu kuna tatizo lingine, kwamba...

Mkishakaribia hotelini, wanatangaza kwamba muda wa kuchimba dawa na chakula ni dakika 10. Kumbuka kwamba kwa msongamano wa kwenye bus, wale wanaokaa siti za katikati au nyuma, hadi wafanikiwe kushuka unakuta wameshatumia dk 5 tayari.

Technically, hadi wakachimbe dawa na wanunue chakula basi wanakuwa wameshatumia dakika zaidi ya 10, this is very unfair.

Inabidi wajirekebishe kwenye hilo swala la muda pia, kwa kuwazingatia back benchers.


Kumbuka kwamba kwa msongamano wa kwenye bus, wale wanaokaa siti za katikati au nyuma, hadi wafanikiwe kushuka unakuta wameshatumia dk 5 tayari.
Hii inatokea sana tu, Abiria wengi wanaagiza chakula(supu) kwa sababu ya uchache wa mda inawabidi kuacha supu, ili asiachwe na Basi, .
 
Back
Top Bottom