Madhara ya kuoa Mwanamke ambaye hajasoma na Golikipa ni haya!

Madhara ya kuoa Mwanamke ambaye hajasoma na Golikipa ni haya!

Nakubaliana na baadhi ya maandiko yako ya nyuma ila kwa hili la leo nakupinga asilimia mia.
Kusoma na kuwa na akili ni vitu viwili tofauti, oa mwanamke mwenye akili sio mwenye elimu. Wanawake kibao wenye elimu hasa huko maofisini ni wachafu na malaya kupitiliza tunawaona.

Na mwanamke kutongozwa sio kitu Cha ajabu labda ajabu ni kulala na Kila anayemtongoza, kinachopelekea mwanamke kutongozwa ni muonekano na mazingira. Mwanamke mkurugenzi ni rahisi kutongozwa na wakurugenzi wenzake au watu wa Kariba yake, mwanamke anaweza akawa hajasoma ila akatongozwa hata na profesa.
Kuna watu wamesoma lakini ukiwaangalia weupe kabisa.
 
Pole sana kama bado unaamini kuwa pesa ya mwanamke kwenye ndoa inamsaada kwako kama mwanaume.

Ogopa sana mwanamke aliesoma na akawa na kipato kukuzidi mwanaume. Utaimba halelluyah moyoni peke yako huku ukisubiria kukata roho umuache ale bata na watoto wako ambao mpaka unafikia unakata roho utakua huna mahusiano nao mazuri.
 
2.Kibarua Cha Mwanamke hakina msaada kwa Mume au kwa familia.
Naam wengi wa waliooa wanakiri wazi kabisa pesa na marupurupu ya mwanamke hayana msaada kwa familia yao, watoto wao hadi wao wenyewe kifupi matumizi yao hayatambuliki na hayahojiki kabisa.
Kwa sisi watu wa 2000s ambao wengi tumekulia kwenye familia zenye mama wasomi, tutakupinga sana.

Hii sio kweli hata kidogo.
 
Asante kwa andiko.
Cha msingi ni kua hakuna universal condition ya mwanamke yupi ni pasua kichwa au la!

Awe msomi au asiye msomi kwa case zote kuna exception na wapuuuzi hawakosekani, watu wa imani watakuambia awe na hofu ya Mungu, ajitambue itasaidia kupunguza risk ya kua wa hovyo.

Pia wanaume tuwe na kiasi kua mkeo sio dada yako wala mama yako, akizingua ujue namna ya kuendelea na maisha na uone wewe bado ni wa thamani...ingawa inahitaji courage hasa.


Ila kwa maisha ya sasa kuna challenges unaziepuka ukioa au kuolewa na mtu mnayeendana elimu na mengineyo. Enzi za wazee wetu kwenda kuozeshwa kijijini case ilikua tofauti sana.
 
[emoji1][emoji1]
Siku ukipata Stroke au umestaafu au kufukuzwa kazi au kufa alafu umeacha watoto wadogo ndio utajua jinsi ulivyokuwa na mawazo mgando.

Pesa ya Mwanamke inaweza isikusaidie wewe lakini ikasaidia wàtoto wako.
Sisi watibeli ngoja niende mbali, sisi wakushi tuna namna yetu ya kusolve mambo.

Umezungumzia elimu ila hukuzungumzia biashara?

Je, Wanawake wenye elimu haba hawawezi biashara?

Je, Wanawake wenye elimu duni hawawezi kujisimamia?

Je, hakuna mifano ya wanawake waliofanikiwa wakiwa na elimu duni?

Kama ndio ni jukumu letu kuandaa mazingira sisi Wakushi ili wake zetu wafanye vizuri kwa miradi tutakayo ianzisha.

Una guarantee gani ukipata matatizo watoto wako watasaidiwa?
Je, hakuna mifano kwenye jamii ya watoto walio tangatanga huku mama zao wakiwa na kipato?

Ndio lengo lako kuoa mwenye kipato ili utelekezwe?

Mtibeli umepatwa na nini?
 
Kwenye taasisi ambazo kazi ni za mikataba miaka mitatu au mikataba ya muda mfupi,ma hr wanatumia sana hiyo kama njia ya kumpa mwanamke wako apate mkataba mpya hata kama ni mgumu vipi akaambiwe toa k nikuongezee contract Wala haruki,Kuna washikaji flani hivi walikuwa wanasimuliana namna wanagegeda wake za watu Kwa mfumo huo.kwa kifupi kama mke wako anabosi mwanamume kazi unayo,usijiwekee bima ndugu yangu.wewe endelea kujisifu mke wangu anafanya kazi benki,au ofisi fulani.wengi wa wanawake wanaofanya kazi ni wachepukaji wakubwa sana.mwanamke anapaswa kulea watoto tuu ,Kwa kifupi tunatakiwa kuwa Kama wapemba.ndoa ndoano
 
si tumeona baba na mama wakishirikiana au unataka maelezo gani?
Baba yako alitoa miongozo, baba yako alisimama kama Mwanaume.

Wewe umeona umbo la nje ila ukifatilia asilimia 90 utagundua dingi yako ndiye aliyehenyeka.

Swali la kujiuliza hakuna wanawake wenye elimu duni na haba walio simama kidete na familia zikasimama?

Kama ndiyo tunachohitaji kwa Mwanamke ni nini?
maana hili ndio Swala la msingi kuliko mengine yote?

Je, elimu yake tu ndio kigezo kama mtibeli anavyotuaminisha?

Je, Mwanamke mwenye kujitunza, heshima, ofu ya Mungu na mwenye upendo ndio anafaa kuwa Mke na baadae Mama?

Je, Mwanamke mwenye Mali na pesa tu ndiyo kiwe kigezo ila tabia sifuri?

Je, Mwanamke mwenye umbo na sura nzuri, tako kama haendi chooni ndio ana sifa ya kuwa Mke?

Unadhani mkeo mwenye elimu/pesa au Mali akiwa na tabia mbovu, unadhani hata watoto utakuwa nao na mahusiano mazuri?

Kama jibu ni hapana ipi faida Mtibeli anayoizungumzia?
 
Back
Top Bottom