Madhara ya Utawala wa Awamu ya Tano yameanza kulitafuna taifa; Nani wa kulaumiwa?

Madhara ya Utawala wa Awamu ya Tano yameanza kulitafuna taifa; Nani wa kulaumiwa?

Extent and level of extremism haijawahi kufikia ile ye Magufuli. Jamaa aliwafanya nchi nzima kama misukule. Alitumia utisho ambao kila mwanadamu anauongopa- Execution.

Ipi hiyo, basi utakuwa mtoto wa juzi unawakumbuka akina Ditopile wewe na akina Zombe na kule pemba 2001 na mwembe chai. Labda utakuwa mtoto mdogo kijana wa juzi. Unamkumbuka Omary Mahita na majambia?

Hukumbuki hata Ulimboka nini kilimtoa na yule mwandishi sijui nani na watu kutupiwa bomu mchana kweupe Arusha. You should be kidding. Tatizo lilikuwepo tena kubwa kuliko sema kulikuwa hakuna WHATSUP.

Hata hivyo hii ni tabia ya washindwaji, mshidwaji yeyote hua hakubali amechamsha lazima atafute wa kumwangushia zigo ili ajisikia yuko fiti fiti. Tabia hii imejikita mizizi kutokea mashinani mpaka ngazi ya taifa. Taifa ukiwauliza wanasingizia beberu ama sahivi mnajificha kwa Magufuli it's pathetic.
 
MALCOM LUMUMBA asante kwa maelezo yako mazuri. Kinachosikitisha ni kuwa pamoja na kwamba Hayati Magufuli aliyakuta matatizo mengi lakini tunaona nia na madhumuninya kuyapunguza au kupambana nayo ilikuwa ndogo au haikuwepo kabisa. Mwisho wa siku yanaendelea siku hadi siku.
Nia ya kutatua matatizo ilikuwepo, lakini mtazamo wa serikali ya awamu ya tano ulikuwa ni mdogo sana (Parochialism). Unapokuwa na mtazamo mdogo huku matatizo yako yakiwa makubwa ni lazima utakwama tu. Kuna mengi ya kuzungumzia kuhusu Tanzania lakini itoshe kusema kwamba tukimwangushia jumba Raisi Magufuli peke yake nadhani tutakuwa tunakosea sana......
 
Nia ya kutatua matatizo ilikuwepo, lakini mtazamo wa serikali ya awamu ya tano ulikuwa ni mdogo sana (Parochialism). Unapokuwa na mtazamo mdogo huku matatizo yako yakiwa makubwa ni lazima utakwama tu. Kuna mengi ya kuzungumzia kuhusu Tanzania lakini itoshe kusema kwamba tukimwangushia jumba Raisi Magufuli peke yake nadhani tutakuwa tunakosea sana......
Ni kweli usemacho. Tunamwangushia kwa sababu alikuwa kwenye position nzuri ya kuyatatua ukizingatia Katiba Yetu imemla mamlaka yote. He had all resources to correft the situation. Labda usema magenge ya ndani yalimzisi nguvu.
 
Lenu hili mlinywe. Hamna wa kumsusia. Mlinywe hivyo hivyo, hakuna namna nyingine.
 
Ndugu zanguni habari za asubuhi.

Ni shahiri dhahiri sasa tumeanza kuvuna tulichopanda.

Sio mkubwa wala mdogo. Mwenye cheo wala asiye na cheo, tajiri wala maskini sote tumeanza kuonja joto la Jiwe.

Hali ni tete. Sio polisi sio Raia. Sio mtuaji sio mteuliwa. Amani, Umoja, utulivu, heshima vimeanza kuteteleka.

Tatizo lilianzia Awamu ya tano. Ambapo utawala wa sheria, haki na kuzingatia misingi ya demokrasia, uwazi na usawa havikuzingatiwa kabisa.

Ni katika utawala wa awamu ya tano ndipo Tulishuhudia kwa kiwango kikubwa Mtanzania anayepigania haki au kuhamasisha umoja na maelewano alikuwa akipingwa na kupigwa hapa na pale. Dhulma ikawa kila mahali. Kwa matajiri na kwa Maskini.

Mimi binafsi naweza kuvilaum vyombo vyenye mamlaka na vilikuwa na uwezo wa kukinga yasitokee

Kwa mfano. Vyombo vya dola Polisi, Mahakama, Usalama na jeshi la nchi viliwezaje kuruhusu watu kuvunjiwa haki zao kwa maslahi ya wanasiasa wachache??

Kwa mfano umtufikirie kesi 147 zilizosemwa na Rais pamoja na Boss qa Takukuru kuwa zilibambikiwa na kusababisha uhasama mkubwa miongoni mwa jamii, kati ya jamii na polisi na hatimaye na serikali yao.

Mfano wa pili ni tukio baya kabisa kuwa kutoke ktk mfumo wa siasa zetu ambapo mwaka 2020 oktoba Uchaguzi ulivurugwa kuanzia mchakato wa utungwaji wa sheria ya uchaguzi na vyama vya siasa na hatimae mchakato wenyewe wa uchaguzi na hata upitishwaji wa wagombea. Najiuliza hili lilifanyika kwa faida ya nani? Usalama wetu tunaouamini kwa maslahi ya nchi hawa kuanticipate madhara ya matukio yale? Polisi je? vipi Mahakama?

Sasa tunaona madhara yake Tozo, maiamala, uhaba wa ajira, uchumi mbovu na sasa hali mbaya ya mufukoni mwa watu.

Tumeanza kuona watu wakipromote uhasama dhidi ya serikali yao. Tukio la Mauwaji ya juzi pale Salenda ni la kusikitisha. Tena likidaiwa kutekelezwa na Mtu anayedaiwa kuqa ni Kada wa chama cha mapinduzi. Hawa vijana wa Chama cha mapinduzi bila kumung'unya maneno walilelewa na kudekezwa vibaya chini ya mwamvuli wa MATAGA. Hili ni kundi kubwa lililokuwa linahisiwa kufanya uhalifu sehemu mbali mbali za nchi. Ilikuwa si ajabu Kutishiwa na vijana hawa kuwa watakupoteza au wanakwambia kabisa tutakubinya ukose mahali pa kwenda na hwakufanywa chochote na mtu yeyote. Sasa Chatu anamla aliyemfuga.

Sasa nini tufanye.

Tuepuke migogoro inayokwepeka. Mahakama zitende haki, Polisi watende haki. Wadhibiti uhalidu kweli kweli. Usalama wafanye kazi yao kweli kwelikweli. Wenye mamlaka tunawakumbusha tu kuwa Hali ikiwa mbaya nchi hii na wao hawataishi kwa amani.

Tumeona wale tuliowaita mabeberu sasa wanafungasha vilago. Matishio ya ugaidi kwa mujibu qa IGP sasa yameibuka tena.

Haya ni madhara ya utawala usiozingatia sheria, katiba na haki za binadamu.

Asalaam Ale ykum
Mninginio wa kipigo cha uchaguzi mkuu haujatoka, na naona kama wenzetu wamefika na wameharibikiwa kabsaaaaa. laaaaaaaa Magufuli baba lao poleni sana.
 
Ni kweli usemacho. Tunamwangushia kwa sababu alikuwa kwenye position nzuri ya kuyatatua ukizingatia Katiba Yetu imemla mamlaka yote. He had all resources to correft the situation. Labda usema magenge ya ndani yalimzisi nguvu.
Hebu nikuulize swali rahisi sana: Wewe ungekuwa ni Raisi Magufuli ungefanya mambo gani kwenye kipindi cha miaka mitano ya mwanzo ??? (Kiuhalisia kabisa)
 
Hebu nikuulize swali rahisi sana: Wewe ungekuwa ni Raisi Magufuli ungefanya mambo gani kwenye kipindi cha miaka mitano ya mwanzo ??? (Kiuhalisia kabisa)
Maovu yote aliyofanya yalikuwa ndani ya miaka mitano tu hakuhitaji miaka 20 kuhakikisha nchi nzima hakuna uhuru wa vyombo vya habari, hakuna bunge huru, hakuhitaji miaka 30 kuunda sheria mbovu za uchumi na haki za binadamu. Ula kwa Mujibu wako miaka hiyo hiyo mitano haikutosha kurekebisha maovu.
 
Maovu yote aliyofanya yalikuwa ndani ya miaka mitano tu hakuhitaji miaka 20 kuhakikisha nchi nzima hakuna uhuru wa vyombo vya habari, hakuna bunge huru, hakuhitaji miaka 30 kuunda sheria mbovu za uchumi na haki za binadamu. Ula kwa Mujibu wako miaka hiyo hiyo mitano haikutosha kurekebisha maovu.
Umezunguka sana lakini hujajibu swali: Wewe ndiyo ungepokea nchi kutoka kwa Jakaya Kikwete, unadhani ni kitu gani muhimu sana ambacho ungetufanyia watanzania ???
 
Umezunguka sana lakini hujajibu swali: Wewe ndiyo ungepokea nchi kutoka kwa Jakaya Kikwete, unadhani ni kitu gani muhimu sana ambacho ungetufanyia watanzania ???
Maelezo yangu yamejikita kwenye hoja yako ya msingi inayoashiria kuwa Hayati Magufuli alikuwa na muda mfupi. Ndicho nilichojibu
 
Maelezo yangu yamejikita kwenye hoja yako ya msingi inayoashiria kuwa Hayati Magufuli alikuwa na muda mfupi. Ndicho nilichojibu
Hoja yangu ya msingi siyo ufupi wa awamu ya Raisi Magufuli, bali ni mizizi ya matatizo mengi yanayoikumba nchi. Ni rahisi sana kung'amua nilichosema endapo tu utaweka siasa na hisia pembeni. Hata wangekuja wapinzani kuongoza nchi matatizo mengi huenda hata wao yangewasumbua: Sasa kukurahishia swali, ni matatizo gani ambayo wewe ungeanza kushughulika nayo endapo ungekuwa Raisi wa awamu ya tano ???
 
Hoja yangu ya msingi siyo ufupi wa awamu ya Raisi Magufuli, bali ni mizizi ya matatizo mengi yanayoikumba nchi. Ni rahisi sana kung'amua nilichosema endapo tu utaweka siasa na hisia pembeni. Hata wangekuja wapinzani kuongoza nchi matatizo mengi huenda hata wao yangewasumbua: Sasa kukurahishia swali, ni matatizo gani ambayo wewe ungeanza kushughulika nayo endapo ungekuwa Raisi wa awamu ya tano ???
😅😅shida ni utitiri wa matatizo
 
Tulikuwa wrong dhidi ya kiongozi muovu!? Tunamshukuru Mungu kwa kutuondolea yule kiongozi muovu bila damu kumwagika.
Watu mnashindwa ku kubali mlikuwa wrong dhidi ya Magufuli, sasa Magufuli hayupo na mlichotarajia hakiji ili kuendeleza u mbuni bado mna ji mbuni tu kichwa mchangani.
 
JPM hayupo tena! Vipi amekwambia ulipe tozo? Lawama za BWM alizibeba Kikwete?.... Mlizoea kumtupia lawama JPM sasa hakuna wa kumtupia lawama sio!? Kazi inaendelea! Hakuna miradi mipya,tozo kama zote,ufisadi,wizi,rushwa,ujambazi vimetamalaki! Na bado hapo... Kazi inaendelea! Mpaka mtubu na kuomba msamaha! SHAABASH!

Hivyo vyote vilikuwepo kipindi cha dhalimu, ama unadhani hatukuwa tunaona yanayoendelea?
 
magufuli anatoka familia yenye historia ya vichaaa.... sio kwa sababu ya madawa ya kulevya au ndumba... ni kuzaliwa hivyo.

usalama wa taifa walishindwaje kumjua MTU mmoja tu, je watawezaje kuijua tz yoteee?

magufuli aliharibu sana inji hii.
Binafsi kabla ya kuandika chochote au kutuhumu mtu flani sababu ya matendo yake lazima uwe na critical thinking,unatakiwa kufanya arguments za kutosha,unatakiwa kutuliza nafsi yako vya kutosha,unatakiwa kudhibiti emotions kwa kiwango cha juu sana,lazima uwe mtu ambae hana chuki na mtu yoyote,lazima uwe mtu mwenye uimara wa kudhibiti mihemuko ndo watu watakuelewa.

Kila mtu ni kichaa kwa jinsi ya maumbile yake,sema hatukujua na hatuwezi kujua kiwango cha ukichaa wako sababu hujapata nafasi ya kuwatumikia watu wakakutathimini akili yako na uwezo wako wa kuwatumikia, inawezekana wewe una kichaa zaidi ya uliyemtuhumu ila sababu hatujaona ukichaa wako hatuwezi kukufahamu.

Kihistoria sijui kama unaifahamu vizuri familia ya Magufuli,sijui hata kama unafahamu ukoo wa Magufuli, lakini sababu ya chuki zako binafsi unaweza ongea chochote utakacho labda sababu ya kufurahisha watu au ugomvi wako binafsi juu ya kitu flani.
 
Ndugu zanguni habari za asubuhi.

Ni shahiri dhahiri sasa tumeanza kuvuna tulichopanda.

Sio mkubwa wala mdogo. Mwenye cheo wala asiye na cheo, tajiri wala maskini sote tumeanza kuonja joto la Jiwe.

Hali ni tete. Sio polisi sio Raia. Sio mtuaji sio mteuliwa. Amani, Umoja, utulivu, heshima vimeanza kuteteleka.

Tatizo lilianzia Awamu ya tano. Ambapo utawala wa sheria, haki na kuzingatia misingi ya demokrasia, uwazi na usawa havikuzingatiwa kabisa.

Ni katika utawala wa awamu ya tano ndipo Tulishuhudia kwa kiwango kikubwa Mtanzania anayepigania haki au kuhamasisha umoja na maelewano alikuwa akipingwa na kupigwa hapa na pale. Dhulma ikawa kila mahali. Kwa matajiri na kwa Maskini.

Mimi binafsi naweza kuvilaum vyombo vyenye mamlaka na vilikuwa na uwezo wa kukinga yasitokee

Kwa mfano. Vyombo vya dola Polisi, Mahakama, Usalama na jeshi la nchi viliwezaje kuruhusu watu kuvunjiwa haki zao kwa maslahi ya wanasiasa wachache??

Kwa mfano umtufikirie kesi 147 zilizosemwa na Rais pamoja na Boss qa Takukuru kuwa zilibambikiwa na kusababisha uhasama mkubwa miongoni mwa jamii, kati ya jamii na polisi na hatimaye na serikali yao.

Mfano wa pili ni tukio baya kabisa kuwa kutoke ktk mfumo wa siasa zetu ambapo mwaka 2020 oktoba Uchaguzi ulivurugwa kuanzia mchakato wa utungwaji wa sheria ya uchaguzi na vyama vya siasa na hatimae mchakato wenyewe wa uchaguzi na hata upitishwaji wa wagombea. Najiuliza hili lilifanyika kwa faida ya nani? Usalama wetu tunaouamini kwa maslahi ya nchi hawa kuanticipate madhara ya matukio yale? Polisi je? vipi Mahakama?

Sasa tunaona madhara yake Tozo, maiamala, uhaba wa ajira, uchumi mbovu na sasa hali mbaya ya mufukoni mwa watu.

Tumeanza kuona watu wakipromote uhasama dhidi ya serikali yao. Tukio la Mauwaji ya juzi pale Salenda ni la kusikitisha. Tena likidaiwa kutekelezwa na Mtu anayedaiwa kuqa ni Kada wa chama cha mapinduzi. Hawa vijana wa Chama cha mapinduzi bila kumung'unya maneno walilelewa na kudekezwa vibaya chini ya mwamvuli wa MATAGA. Hili ni kundi kubwa lililokuwa linahisiwa kufanya uhalifu sehemu mbali mbali za nchi. Ilikuwa si ajabu Kutishiwa na vijana hawa kuwa watakupoteza au wanakwambia kabisa tutakubinya ukose mahali pa kwenda na hwakufanywa chochote na mtu yeyote. Sasa Chatu anamla aliyemfuga.

Sasa nini tufanye.

Tuepuke migogoro inayokwepeka. Mahakama zitende haki, Polisi watende haki. Wadhibiti uhalidu kweli kweli. Usalama wafanye kazi yao kweli kwelikweli. Wenye mamlaka tunawakumbusha tu kuwa Hali ikiwa mbaya nchi hii na wao hawataishi kwa amani.

Tumeona wale tuliowaita mabeberu sasa wanafungasha vilago. Matishio ya ugaidi kwa mujibu qa IGP sasa yameibuka tena.

Haya ni madhara ya utawala usiozingatia sheria, katiba na haki za binadamu.

Asalaam Ale ykum
Ustadhi c mwenzako sasa yuko ikuruu..c mlimshangilia sana ustadha..rekebisheni sasa sio kuanza kulaumu watu ambao hawapo. Mmekabidhiwaa kijiti sasa barakashiaaa kaz kwenu rekebisheni
 
Ustadhi c mwenzako sasa yuko ikuruu..c mlimshangilia sana ustadha..rekebisheni sasa sio kuanza kulaumu watu ambao hawapo. Mmekabidhiwaa kijiti sasa barakashiaaa kaz kwenu rekebisheni
the damage caused is beyond repair
 
Back
Top Bottom