Maelezo kwa ufupi juu ya clip ikionyesha wanajeshi katili wakiua raia

Maelezo kwa ufupi juu ya clip ikionyesha wanajeshi katili wakiua raia

Kwa muda wangu wa kuishi Duniani, sina mashaka wala wasiwasi wa uwepo wa siku ya Hukumu na maisha baada ya kifo. Sasa mna potoshwa na kudanganywa na yule muovu na mawakala wake ili muamini hakuna hiko kitu. Ile siku ipo bro, ile jioni ipo kaka na ni dhahiri kabisa.
Na iwe hivyo , tukutane asubuhi
 
Hii clip nimeiona kutoka kwenye uzi alioanzisha mdau anaitwa GoldDhahabu wenye kichwa cha habari Hawa wanajeshi katili ni wa wapi? .

View: https://streamable.com/ly7v6f

Kuna maelezo mengi tofauti na sehemu kubwa si sahihi.

Tukio linaonyesha raia ambao wamefungwa mikono na kuzibwa macho wakikokotwa na askari, pasipo raia hao kujua wanaelekea wapi au pengine wakifahamu wanaelekea mahala salama wanaangukia kwenye shimo lililoandaliwa tayari na kupigwa risasi vichwani, baada ya askari hao kumaliza kuwapiga risasi mmoja baada ya mwingine, askari hao wakiwa wameshatanguliza matairi ya gari kwenye shimo, wanawasha moto na kuteketeza miili hio.



Hili tukio lilitokea 16 April 2013 nchini Syria katika mji mkuu Damascus, askari wanao onekana kutekeleza unyama huo wanatokea kitengo cha intelijensia katika jeshi la Syria (Military Intelligence Directorate (Syria)), na specifically hao askari wapo katika kitengo kinachohusika na ukatili, utesaji na mauaji pasipo huruma. Yaani kwenye Syrian Military Intelligence kuna hiki kitengo kwa ajili ya utesaji, mauaji na ukatili wa kila aina unaoufahamu.

Syrian Military Intelligence ipo chini ya raisi, inaendeshwa na Bashar Al Assad mwenyewe, kitengo hiki kimekuwa kimetumika pia kwenye siasa hasa kuwakandamiza wale wanaotaka kuleta upinzani lazima cha moto utakiona.

Hii clip imevuja mwaka 2022, inasemekana kuna mtu alipata access ya laptop iliyokuwa na clip hii, akacopy na kuihifadhi, inasemekana ni askari wa Syria.
Aliyetambulika kwenye hii clip ni Major Amjad Yousef ambae anaonekana kuwapiga risasi raia hao pasipo huruma, askari huyu katili inasemekana amejiunga na jeshi mwaka 2004, baadae baada ya mafunzo akajiunga na branch 227 katika Syrian Intelligence Service kitengo maalumu kwa ajili ya utekaji, kutesa na kuua hasa wapinzani katika serikali ya Syria.

Kwa ufupi hao raia wanauliwa kikatili inasemekana hawana kosa, kilikuwa ni kipindi cha mapigano ambapo waasi walikuwa wanakaribia eneo hilo, hivyo askari hao walitaka kuonyesha mfano kwa yeyote ambae atajaribu kuwa upande wa uasi. Raia hao inasemekana waliishi karibu kabisa na eneo ambalo kulikuwa na upinzani.

Raia waliouawa wakati huo ni 41, waliouawa kwenye hilo shimo. Hata hivyo inasemekana waliouawa wengine ni wanakadiriwa 200 au 300 katika maeneo mengine

Baada ya clip kuvuja, Amjad alikamatwa na serikali ya Syria 2022, Amjad amekamatwa pasipo warrant na hajafikishwa mahakamani, wachambuzi wa mambo wanasema kukamatwa kwa Amjad ni kuzuia waliojihusisha na unyama huo waliopo ngazi za juu wasifahamike.

Serikali ya marekani ilitoa sanctions juu ya Amjad Yousef mnamo March mwaka huu 2023 , secreatry of state Anthony Blinken alisema vikwazo hivyo ni kwa ajili ya mauaji hayo yaliyofanyika.

Dah!... serikali katili sana hiyo.


Urusi na Iran wanaunga mkono serikali ya kinyama hivyo, anyway hata Putin ni mnyama kama Assad tu.

Yoda lee Vladimir cleef T14 Armata dudus Bwana Utam
 
Hii clip nimeiona kutoka kwenye uzi alioanzisha mdau anaitwa GoldDhahabu wenye kichwa cha habari Hawa wanajeshi katili ni wa wapi? .

View: https://streamable.com/ly7v6f

Kuna maelezo mengi tofauti na sehemu kubwa si sahihi.

Tukio linaonyesha raia ambao wamefungwa mikono na kuzibwa macho wakikokotwa na askari, pasipo raia hao kujua wanaelekea wapi au pengine wakifahamu wanaelekea mahala salama wanaangukia kwenye shimo lililoandaliwa tayari na kupigwa risasi vichwani, baada ya askari hao kumaliza kuwapiga risasi mmoja baada ya mwingine, askari hao wakiwa wameshatanguliza matairi ya gari kwenye shimo, wanawasha moto na kuteketeza miili hio.



Hili tukio lilitokea 16 April 2013 nchini Syria katika mji mkuu Damascus, askari wanao onekana kutekeleza unyama huo wanatokea kitengo cha intelijensia katika jeshi la Syria (Military Intelligence Directorate (Syria)), na specifically hao askari wapo katika kitengo kinachohusika na ukatili, utesaji na mauaji pasipo huruma. Yaani kwenye Syrian Military Intelligence kuna hiki kitengo kwa ajili ya utesaji, mauaji na ukatili wa kila aina unaoufahamu.

Syrian Military Intelligence ipo chini ya raisi, inaendeshwa na Bashar Al Assad mwenyewe, kitengo hiki kimekuwa kimetumika pia kwenye siasa hasa kuwakandamiza wale wanaotaka kuleta upinzani lazima cha moto utakiona.

Hii clip imevuja mwaka 2022, inasemekana kuna mtu alipata access ya laptop iliyokuwa na clip hii, akacopy na kuihifadhi, inasemekana ni askari wa Syria.
Aliyetambulika kwenye hii clip ni Major Amjad Yousef ambae anaonekana kuwapiga risasi raia hao pasipo huruma, askari huyu katili inasemekana amejiunga na jeshi mwaka 2004, baadae baada ya mafunzo akajiunga na branch 227 katika Syrian Intelligence Service kitengo maalumu kwa ajili ya utekaji, kutesa na kuua hasa wapinzani katika serikali ya Syria.

Kwa ufupi hao raia wanauliwa kikatili inasemekana hawana kosa, kilikuwa ni kipindi cha mapigano ambapo waasi walikuwa wanakaribia eneo hilo, hivyo askari hao walitaka kuonyesha mfano kwa yeyote ambae atajaribu kuwa upande wa uasi. Raia hao inasemekana waliishi karibu kabisa na eneo ambalo kulikuwa na upinzani.

Raia waliouawa wakati huo ni 41, waliouawa kwenye hilo shimo. Hata hivyo inasemekana waliouawa wengine ni wanakadiriwa 200 au 300 katika maeneo mengine

Baada ya clip kuvuja, Amjad alikamatwa na serikali ya Syria 2022, Amjad amekamatwa pasipo warrant na hajafikishwa mahakamani, wachambuzi wa mambo wanasema kukamatwa kwa Amjad ni kuzuia waliojihusisha na unyama huo waliopo ngazi za juu wasifahamike.

Serikali ya marekani ilitoa sanctions juu ya Amjad Yousef mnamo March mwaka huu 2023 , secreatry of state Anthony Blinken alisema vikwazo hivyo ni kwa ajili ya mauaji hayo yaliyofanyika.

Acha uwongo mkuu. Hapo sio Mabwepande?
 
Hivi hawa washkaji wana familia kweli huko nyumbani yaani watoto au mke aseee !! Watu huwa wanasema kufanya kazi mochwari ni kipengele ila hii kazi ni ya moto asee naona bora hata anayenyonga wafungwa ana nafuu ! Hii kazi hata ukiiacha lazima upate Post Traumatic Disorder.

Hiki kitengo hata kwetu hapa kipo kweli ?
Mzee unakuta ana watoto na Mke pisi tu.
Hayo wanayafanya mafichoni.
Hakuna aliyetegemea hii clip itoke.
Kwani hata wale waliofungwa kwa Mifuko..mbeleni huko ndio madude yanavuja kama hivi.

Hii Dunia kila kitu fanya kwa Staha,ila kwa siasa na Biashara,kazi usipokuwa makini kichwani.Unapotezwa sekunde tu.
Ukiachana na Special case ya Mapenzi.
 
Mwamba huyo hapa
6fab4807dafcfe74013ce211.jpeg
images (22).jpeg
 
Mzee unakuta ana watoto na Mke pisi tu.
Hayo wanayafanya mafichoni.
Hakuna aliyetegemea hii clip itoke.
Kwani hata wale waliofungwa kwa Mifuko..mbeleni huko ndio madude yanavuja kama hivi.

Hii Dunia kila kitu fanya kwa Staha,ila kwa siasa na Biashara,kazi usipokuwa makini kichwani.Unapotezwa sekunde tu.
Ukiachana na Special case ya Mapenzi.
Daah binadamu tuna roho mbaya asee ! Yaan jamaa anavyowachapa risasi hana hata habari yaan
 
Uko sahihi kabisa.Huku maofisini,Biashara kaa kwa akili pana sana hasa zikianza habari za upigaji wa fedha nyingi.
Dunia inaongozwa na wahalifu walio vaa suti . Kuingia tu madarakani kila mbinu ovu watu wana tumia sembuse sembuse kuua watu ndio liwe jambo la ajabu kwao ?
 
Unawezaje ku post kitu kama hiki Mungu wangu! Moderator , ondoa hii kitu kisha piga ban ya maisha kwa aliepost, sisi tulio view tupige ban ya mwezi mwezi itatosha.
 
Taja hizo nchi ambazo hazijafanya unyama wa namna hiyo ?
Nasubiria awataje taifa flani kubwa nimletee historia ya ukatili waliofanyiwa Patrice Lumumba na wenzie, au alichofanyiwa Che Guavara au walichofanyiwa wapiganaji wa Viet Conf.
 
We hata ukitukana ni sawa ila Maumivu ni yale yale. Kwa nchi za kiafrika bora uuliwe kuliko kusingiziwa u shoga. Fedheha kubwa sana katika jamii. Ebu badilikeni sister. Hamtendei haki wenzenu.
Wewe salama kweli au tipa linabinuliwa Hilo!?
 
Yesu anasema,"Watch Syria,because that is where ww111 will start."
 
Back
Top Bottom