Maelezo ya kina kuhusu Uber. Usafiri salama na wa bei ya chini kwa mtanzania

Maelezo ya kina kuhusu Uber. Usafiri salama na wa bei ya chini kwa mtanzania

Nimepanda uber mara mbili nimepata faraja sana juu ya teknolojia, nilitumia promo code iliyotolewa hapa na mdau ya elf 6500 nilipandia kinondon facebook mpaka sinza kwa Remmy nikawa na wasaa mzuri wa kumhoji dereva mambo mbalimbali zikiwemo na changamoto zake, tulivyofika mwisho wa safari kuangalia anaona natakiwa nisimpe kitu! nikamweleza akanielewa mwisho wa siku nikamtoa buku 2 akanywe japo maji![emoji16][emoji16][emoji16] kwa maana alinipa maelezo mengi sana ya kujitosheleza

Sent from my HUAWEI NMO-L31 using JamiiForums mobile app
 
Siku nikija Dar ntajaribu usafiri wenu
Nimependa maelezo yako
 
Nimepanda uber mara mbili nimepata faraja sana juu ya teknolojia, nilitumia promo code iliyotolewa hapa na mdau ya elf 6500 nilipandia kinondon facebook mpaka sinza kwa Remmy nikawa na wasaa mzuri wa kumhoji dereva mambo mbalimbali zikiwemo na changamoto zake, tulivyofika mwisho wa safari kuangalia anaona natakiwa nisimpe kitu! nikamweleza akanielewa mwisho wa siku nikamtoa buku 2 akanywe japo maji![emoji16][emoji16][emoji16] kwa maana alinipa maelezo mengi sana ya kujitosheleza

Sent from my HUAWEI NMO-L31 using JamiiForums mobile app
Hongera sana mkuu kutumia usafiri wa Uber, kimsingi Uber inalipia hiyo gharama yako ya safari ya kwanza,kwahiyo dereva hakutakiwa kujisikia vibaya maana Uber itamlipa hela yake. Ila kama ulivyosema kumtoa buku 2 ya maji sio vibaya, ni kama ulimpa tip(bakshishi)
 
Uber ndo habari ya mjini shida jf wamejaa watu na magari yao na pia wengine hawafahamu uber ni nini, ila kwa usafiri wa uhakika uber ni bora na nafuu kuliko bajaji na taxi
 
Habari wanaJamiiforums, Je umeshawahi kutumia usafiri wa Uber?
Kama bado soma hapa na bila shaka utashawishika kuujaribu.
Na kizuri zaidi utapata punguzo la tsh 6200, pale utumiapo Uber kwa mara ya kwanza.

Endapo safari yako ya kwanza itakuwa fupi,na nauli ikawa chini ya 6200 basi utakuwa umepata nafasi ya kusafiri buree bila gharama yoyote.Na ikiwa zaidi utalipa kile kinachoongezeka hapo kwenye 6200 tu.


Uber ni nini?
Uber ni application ya simu inayokuwezesha kupata usafiri wa bei ya chini na salama katika sehemu nyingi za mkoa wa Dar-es-Salaam, kwa kupitia simu yako ya mkononi. Usafiri huu ni wa kutumia magari madogo yanayoweza kubeba kuanzia mtu mmoja hadi watu wanne.

Kujisajili na Uber
Nenda Google playstore, search 'Uber' utaiona ina icon nyeusi, download kisha ifungue.
Fanya usajili kwa kutumia namba yako ya simu na email; pia utachagua neno la siri.

Kupata punguzo la Tsh6200 katika trip yako ya kwanza
  • Nenda Menu kwa kubonyeza mistari mitatu iliyoko juu kushoto,Kisha bonyezaPayments,kisha bonyeza Add promo code , andika ubertz5
  • Utaona maandishi ya kijani yakionyesha kwamba utapata punguzo la tsh6200 katika trip yako ya kwanza.
  • Nitatoa mfano, safari yako ya kwanzi ni kutoka posta hadi magomeni,na gharama yake ni shilingi 7200,basi utalipa sh1000 tu kutokana na hilo punguzo,lakini katika safari ya pili utalipa nauli kamili.
Jinsi ya kutumia Uber kuita usafiri.
  • Fungua app ya Uber, hakikisha umewasha GPS, itakuletea maandishi 'where to'.Hapo utajaza unapotaka kwenda,mfano 'Magomeni Mapipa'.
  • Itakuonyesha kiasi cha nauli inayokadiriwa, na utabonyeza 'Request uberX'
  • Hapo hapo,itakuonyesha jina na namba ya gari la dereva atakayekufata hapo hapo ulipo, na ndani ya dk5 atakuwa kashafika.
Malipo ya usafiri
  • Ukifika 'destination' yako dereva atabonyeza 'Stop trip' kwenye application iliyoko kwenye simu yake, na hapo hapo itaonyesha nauli kwenye simu yako na kwenye simu ya dereva
  • Unaweza kulipa kwa Cash(Taslimu) au kwa kutumia Kadi ya benki gharama ikawa inakatwa moja kwa moja
Umuhimu wa kutumia Uber
  • Ni gharama nafuu zaidi ukilinganisha na taxi za kawaida, kwa sababu bei inahesabiwa na mashine yenyewe kulingana na umbali wa sehemu unayoenda, na sio derevaa kujipangia bei kubwa.
  • Ni salama zaidi, hasahasa usiku, kwasababu dereva wa uber anakuwa amesajiliwa na endapo itatokea tatizo lolote mfano kusahau kitu kwenye gari, dereva anaweza kupatikana kwa haraka.
  • Inakusaidia kuokoa muda; mfano upo sehemu ambapo hamna taxi,bajaji wala bodaboda, unaweza kuita usafiri na ukakufata hapohapo kwa kutumia app hii.
  • Ni usafiri bora; magari ya Uber,yanakaguliwa kabla ya kuruhusiwa kutoa huduma, hivyo inakuepusha na kupanda magari mabovu.
Jaribu Uber leo, uone teknolojia inavyorahisisha mambo; na kupunguza gharama.

Angalia gharama za uber zilivyo nafuu
uber makadirio.PNG
 
nataka niwe dereva wa uber nafanyeje?
Uber haina magari, bali inaunganisha madereva na watu wanaohitaji usafiri. Kwahiyo ili usajiliwe kama dereva;inabidi uwe na gari(la binafsi au hata taxi), na leseni halali. Ukifika katika ofisi za Uber zilizopo Viva towers Posta, utaingizwa kwenye system na utapewa maelekezo zaidi. Karibu sana
 
Uber haina magari, bali inaunganisha madereva na watu wanaohitaji usafiri. Kwahiyo ili usajiliwe kama dereva;inabidi uwe na gari(la binafsi au hata taxi), na leseni halali. Ukifika katika ofisi za Uber zilizopo Viva towers Posta, utaingizwa kwenye system na utapewa maelekezo zaidi. Karibu sana
asante sana .ngoja nianze misele. ila hakuna wateja wakorofi? yaani nimemfikisha halafu asinilipe? au napokea cash kwanza?
 
asante sana .ngoja nianze misele. ila hakuna wateja wakorofi? yaani nimemfikisha halafu asinilipe? au napokea cash kwanza?
Ukimfikisha ndo anakulipa, usiwe na wasiwasi kuhusu wateja wakorofi. Unapomfikisha mteja, akikataa kukulipa/akishindwa kukulipa wala hautakiwi kubishana nae;tena unamwachia kabisa aende.Ila utareport directly Uber, nao watakulipa, then ndo watadeal na mteja kivyao
 
Ukimfikisha ndo anakulipa, usiwe na wasiwasi kuhusu wateja wakorofi. Unapomfikisha mteja, akikataa kukulipa/akishindwa kukulipa wala hautakiwi kubishana nae;tena unamwachia kabisa aende.Ila utareport directly Uber, nao watakulipa, then ndo watadeal na mteja kivyao
ok hapo sawa . uber wanachukua sh ngapi
 
Back
Top Bottom