Maelezo ya kina kuhusu Uber. Usafiri salama na wa bei ya chini kwa mtanzania

Maelezo ya kina kuhusu Uber. Usafiri salama na wa bei ya chini kwa mtanzania

Jaribu kutumia Uber leo ujionee teknolojia inavyokua na kurahisisha mambo
 
Je umeshawahi?
  • Kwenda kwenye sherehe ya usiku, na ukakosa usafiri wa kurudi?
  • Uko sehemu mvua inanyesha na unataka kwenda sehemu nyingine ila huna usafiri binafsi?
  • Unataka kwenda out na mpenzi wako lakini unapata stress kwa kutokuwa na usafiri wa uhakika?
  • Umechoshwa na jua kali na vumbi linalokupiga pale ukipanda bodaboda
  • Au umechoshwa na zile purukushani za kugombania daladala n.k
Kwa shida kama hizi za usafiri,suluhisho lake ni kutumia Uber
Na kizuri zaidi utapata punguzo la tsh 6200, pale utumiapo Uber kwa mara ya kwanza.

Uber ni nini?
Uber ni application inayokuwezesha kupata usafiri wa bei ya chini na salama katika sehemu nyingi za mkoa wa Dar-es-Salaam, kwa kupitia simu yako ya mkononi. Usafiri huu ni wa kutumia magari madogo yanayoweza kubeba kuanzia mtu mmoja hadi watu wanne.

Kujisajili na Uber
Nenda playstore, search 'Uber' utaiona ina icon nyeusi, download kisha ifungue.
Fanya usajili kwa kutumia namba yako ya simu, email na pia utachagua neno la siri.

Kupata punguzo la Tsh6200 katika trip yako ya kwanza
  • Nenda Menu kwa kubonyeza mistari mitatu iliyoko juu kushoto,Kisha bonyezaPayments,kisha bonyeza Add promo code , andika ubertz5
  • Utaona maandishi ya kijani yakionyesha kwamba utapata punguzo la tsh6200 katika trip yako ya kwanza.
  • Nitatoa mfano, safari yako ya kwanza ni kutoka posta hadi magomeni,na gharama yake ni shilingi 7200,basi utalipa sh1000 tu kutokana na hilo punguzo,lakini katika safari ya pili utalipa nauli kamili.

Zingatia

Unaweza kujisajili mara moja tu kwa kutumia hiyo promotion code, ukirudia kujisajili kwa namba nyingine kama baadhi ya watu wanavyopotosha mitandaoni, akaunti yako ya uber itafungiwa na hutaweza tena kutumia huduma za uber

Jinsi ya kutumia Uber kuita usafiri.
  • Fungua app ya Uber, hakikisha umewasha GPS, itakuletea maandishi 'where to'.Hapo utajaza unapotaka kwenda,mfano 'Magomeni Mapipa'.
  • Itakuonyesha kiasi cha nauli inayokadiriwa, na utabonyeza 'Request uberX'
  • Hapo hapo,itakuonyesha jina na namba ya gari la dereva atakayekufata hapo hapo ulipo, na ndani ya dk5 atakuwa kashafika.
Malipo ya usafiri
  • Ukifika 'destination' yako dereva atabonyeza 'Stop trip' kwenye application iliyoko kwenye simu yake, na hapo hapo itaonyesha nauli kwenye simu yako na kwenye simu ya dereva
  • Unaweza kulipa kwa Cash(Taslimu) au kwa kutuma Kadi ya benki
Umuhimu wa kutumia Uber
  • Ni gharama nafuu zaidi ukilinganisha na taxi za kawaida, kwa sababu bei inahesabiwa na mashine yenyewe kulingana na umbali wa sehemu unayoenda, na sio derevaa kujipangia bei kubwa
  • Ni salama zaidi, hasahasa usiku, kwasababu dereva wa uber anakuwa amesajiliwa na endapo itatokea tatizo lolote mfano kusahau kitu kwenye gari, dereva anaweza kupatikana kwa haraka
  • Inakusaidia kuokoa muda; mfano upo sehemu ambapo hamna taxi,bajaji wala bodaboda, unaweza kuita usafiri na ukakufata hapohapo kwa kutumia app hii.
Wadau waliotumia Uber wanasemaje:
Uber ni the best kwakweli madriver tax wa kawaida wanakuangalia kwanza umevaaje unaenda wapi ndo anakupa bei,bora kutumia Uber

Juzi hapa nimetumia UBER kutoka buguruni hadi kkoo mida ya saa nne usiku hivi. Dereva alikuwa kadada flani karembo around 26yrs ana kaPasso kananukia vizurii.Njiani full story aisee,hadi sikutamani kushuka.
Akawa ananiambia yeye anafanya kazi ya Uber part time, akiwa anatoka kazini kwake ndo anapiga trips kadhaa then anarudi nyumbani.
Cha kushangaza nauli ikasoma buku tano tu

Ubber naipenda sana hasa kwa wafanyabiashara ni ngumu kuchorewa mchezo wa kuibiwa....nipo nairob naitumia mno na bei ni poa nikiwa dar pia naitumia inarahisisha mambo.....mpaka umigie dereva wako akudanganye woi hiyo dereva yupo karib na ulipo muda wote

Nimetumia iko poa sana no Leo asbh

Uber imerahisisha sana maisha yangu

Nimetoka Ubungo stendi hadi Karume usiku wa saa saba kwa elfu nane

Ni kweli usafiri wa UBER ni rahisi ukilinganisha na Taxis nyingine. Mfano kutoka Ubungo kwenda Airport kwa UBER ni 15,000; Taxis nyingine ni 25,000 mpaka 40,000 kutegemeana na unavyojua kuomba punguzo. Toka Ubungo mpaka Bottle majengo pacha ni 12,000 Taxis nyingine hapo ni 30,000 hivi
 
Hivi UBER wana waiting charges?
Nakumbuka tulitoka kimara baruti tukaenda mlimani city tukamwambia atusubiri tufuatilie kitu chap chap then baada ya hapo tutamrudia atupeleke kariakoo. Kwa bahati mbaya tukapoteza muda mule ndani kama dk 45 hivi bila kutegemea tukamrudia akatupeleka kariakoo kupitia ubungo mataa na alipotufikisha kariakoo akadai Tshs 57000 ambayo ndio iliyokuwa ikimwonyesha kwenye app yake thou mim kwa mahesabu ya app yangu uki sum up route zote nilikuwa napata chini ya Tshs 57000
 
Kuhusu usalama wako;
Mkuu ili mteja atumie usafiri wa Uber lazima awe amejisajili kwa kutumia namba yake ya Simu, hivyo ni vigumu mtu kufanya uhalifu akijua namba yake ya simu imesajiliwa. Vilevile uber wana taarifa mbalimbali kama IMEI namba ya simu husika, hii inaweza kusaidia kumtrace mteja anapofanya uhalifu kama kuiba gari la dereva wa uber.

Kuhusu kujiunga na Uber kama una gari na dereva; hii unaweza ukafika ofisi za Uber, Viva towers Posta, ukapata maelezo zaidi
je kama mhalifu akiforge imei number na akasajiii lain kwa kitambulisho feki....hamuoni kwamba dereva atakuwa kwenye risk....add more security features please
 
Mkuu umesahau haya:-
1. Ukiita gari halafu usiitumie(ukaingia mitini) utachajiwa 3,000/=, yaani account yako itawekewa deni hilo. Siku nyingine ukiita gari inakupa nauli ya kawaida na ile penalt ya 3,000/=. Kama unatoka Mwenge to Ubungo 2,500/= bili itakuja 5,500/=

2. Ushindani unakuja sasa, naona kuna nyingine imeanzishwa inaitwa Taxify, uber boresheni zaidi huyu asiwapiku.
 
Habari wanaJamiiforums, baada ya kuona watu wanasambaza tricks za uongo kuhusu usafiri wa Uber nimeshawishika kuelezea kwa kina kuhusu usafiri huu.

Uber ni nini?
Uber ni application inayokuwezesha kupata usafiri wa bei ya chini na salama katika sehemu nyingi za mkoa wa Dar-es-Salaam, kwa kupitia simu yako ya mkononi. Usafiri huu ni wa kutumia magari madogo yanayoweza kubeba kuanzia mtu mmoja hadi watu wanne.

Kujisajili na Uber
Nenda playstore, search 'Uber' utaiona ina icon nyeusi, download kisha ifungue.
Fanya usajili kwa kutumia namba yako ya simu, email na pia utachagua neno la siri.

Kupata punguzo la Tsh6200 katika trip yako ya kwanza
  • Nenda Menu kwa kubonyeza mistari mitatu iliyoko juu kushoto,Kisha bonyezaPayments,kisha bonyeza Add promo code , andika tzaba17
  • Utaona maandishi ya kijani yakionyesha kwamba utapata punguzo la tsh6200 katika trip yako ya kwanza.
  • Nitatoa mfano, safari yako ya kwanza ni kutoka posta hadi magomeni,na gharama yake ni shilingi 7200,basi utalipa sh1000 tu kutokana na hilo punguzo,lakini katika safari ya pili utalipa nauli kamili.

Zingatia

Unaweza kujisajili mara moja tu kwa kutumia hiyo promotion code, ukirudia kujisajili kwa namba nyingine kama baadhi ya watu wanavyopotosha mitandaoni, akaunti yako ya uber itafungiwa na hutaweza tena kutumia huduma za uber

Jinsi ya kutumia Uber kuita usafiri.
  • Fungua app ya Uber, hakikisha umewasha GPS, itakuletea maandishi 'where to'.Hapo utajaza unapotaka kwenda,mfano 'Magomeni Mapipa'.
  • Itakuonyesha kiasi cha nauli inayokadiriwa, na utabonyeza 'Request uberX'
  • Hapo hapo,itakuonyesha jina na namba ya gari la dereva atakayekufata hapo hapo ulipo, na ndani ya dk5 atakuwa kashafika.
Malipo ya usafiri
  • Ukifika 'destination' yako dereva atabonyeza 'Stop trip' kwenye application iliyoko kwenye simu yake, na hapo hapo itaonyesha nauli kwenye simu yako na kwenye simu ya dereva
  • Unaweza kulipa kwa Cash(Taslimu) au kwa kutuma Kadi ya benki
Umuhimu wa kutumia Uber
  • Ni gharama nafuu zaidi ukilinganisha na taxi za kawaida, kwa sababu bei inahesabiwa na mashine yenyewe kulingana na umbali wa sehemu unayoenda, na sio derevaa kujipangia bei kubwa
  • Ni salama zaidi, hasahasa usiku, kwasababu dereva wa uber anakuwa amesajiliwa na endapo itatokea tatizo lolote mfano kusahau kitu kwenye gari, dereva anaweza kupatikana kwa haraka
  • Inakusaidia kuokoa muda; mfano upo sehemu ambapo hamna taxi,bajaji wala bodaboda, unaweza kuita usafiri na ukakufata hapohapo kwa kutumia app hii.
Duuuh aisee tumefika mbali kiasi hususani kwny ubunifu wa matumizi ya technology
 
kwa siye wa windows phone tunafanyaje kuipata hiyo app?
 
Mkuu umesahau haya:-
1. Ukiita gari halafu usiitumie(ukaingia mitini) utachajiwa 3,000/=, yaani account yako itawekewa deni hilo. Siku nyingine ukiita gari inakupa nauli ya kawaida na ile penalt ya 3,000/=. Kama unatoka Mwenge to Ubungo 2,500/= bili itakuja 5,500/=

2. Ushindani unakuja sasa, naona kuna nyingine imeanzishwa inaitwa Taxify, uber boresheni zaidi huyu asiwapiku.
Asante sana kwa kukumbushia hayo mawili mkuu.
Niongezee tu.
1.Ili kuepuka kuchajiwa hiyo 3000,unabidi ucancel request chini ya dakika 5 baada ya kuita gari. Ili kuzuia dereva kuingia gharama ya mafuta kukufata ulipo wakati hauna nia ya kusafiri.

2.Nakuhaidi Uber itaendelea kuboresha huduma, ili tuendelee kuwa bora zaidi kuliko hao washindani wetu
 
  • Thanks
Reactions: ARV
Vp huku kwa mtogole nikiita ndani ya dk5 inakua imefika?
Maeneo ya ndanindani bado ni changamoto,magari hayako mengi sana.

Wakati wa kuita usafiri, utapata nafasi ya kuona magari yaliyoko karibu nawe, kama yako karibu basi ndani ya dk5 utapata usafiri.

Na kitu kizuri kuhusu Uber utapata nafasi ya kuona gari likiwa linakuja kwenye ramani, na unaonyeshwa litatumia dk ngapi kukufikia
 
Hivi UBER wana waiting charges?
Nakumbuka tulitoka kimara baruti tukaenda mlimani city tukamwambia atusubiri tufuatilie kitu chap chap then baada ya hapo tutamrudia atupeleke kariakoo. Kwa bahati mbaya tukapoteza muda mule ndani kama dk 45 hivi bila kutegemea tukamrudia akatupeleka kariakoo kupitia ubungo mataa na alipotufikisha kariakoo akadai Tshs 57000 ambayo ndio iliyokuwa ikimwonyesha kwenye app yake thou mim kwa mahesabu ya app yangu uki sum up route zote nilikuwa napata chini ya Tshs 57000
Ni sahihi kabisa kuwa charged 57000.Nauli ya Uber hukokotolewa kwa kutumia Umbali uliotembea(km) na Dakika ulizotumia katika safari yako.Kwahiyo automatically dereva akibonyeza start trip program inaanza kuhesabu muda; pale mliposimama kwa dk45,app iliongezea charges kwenye nauli ya awali
 
Hivi UBER wana waiting charges?
Nakumbuka tulitoka kimara baruti tukaenda mlimani city tukamwambia atusubiri tufuatilie kitu chap chap then baada ya hapo tutamrudia atupeleke kariakoo. Kwa bahati mbaya tukapoteza muda mule ndani kama dk 45 hivi bila kutegemea tukamrudia akatupeleka kariakoo kupitia ubungo mataa na alipotufikisha kariakoo akadai Tshs 57000 ambayo ndio iliyokuwa ikimwonyesha kwenye app yake thou mim kwa mahesabu ya app yangu uki sum up route zote nilikuwa napata chini ya Tshs 57000
Nakushauri siku nyingine kama unahitaji kukaa sehemu muda mrefu,mwambie dereva aStop trip then kwenye safari inayofata ita usafiri upya.Ukimwambia asubiri gharama inakuwa kubwa sana
 
Uber ni nzuri please ileteni na mikoani huku, Arusha nawish iwepo uber maana nauli za tax za kutazamana, pia jitahidini app iwe na uwepesi wa kusoma zaidi, unaweza safiri mpaka mwisho wa trip halafu unakuta app bado haijasema trip imeisha inabidi ukae kwenye gari kwa dakika kadhaa so sometime kama unaharaka unakuta muda unapotea njian, ni app nzuri sana huwa naenjoy kila nijapo dsm maana hata kama mtu hulijui jiji unaweka tu mtaa unaoenda na unaita usafiri wako
 
Back
Top Bottom