Membensamba
Senior Member
- Nov 4, 2010
- 157
- 10
Watanzania walio wengi sasa, hata wale wa ccm, tofauti na siku za nyuma wanaonekana kuwa na mwamko wa kutamani katiba iandikwe upya. Nasema IANDIKWE UPYA sio hii iliyopo itiwe viraka. Kwangu mimi hii ni dalili ya kukua kutoka kwenye hatua moja ya kidemokrasia na mwamko wa kisiasa hadi nyingine. Lakini pia nadhani ni dalili kubwa ya mabadiliko ya mazingira ya kisiasa, kiuchumi, na kila nyanja. Watu wameanza kugundua sasa kuwa shuka ambayo wamekuwa wakijifunika haiwatoshi tena, kwani wamerefuka zaidi, tena shuka hii imechakaa. Wanataka mpya.
Katika hali hii nadhani think tanks wa nchi hii ni wakati muafaka kuijuza jamii ni kwa nini tuwe na katiba mpya, kwa nini tunadhani hii ya sasa imepitwa na wakati, na katiba mpya tunadhani izingatie mambo gani tunayodhani yanahitajika sasa. Nawaita akina political analysts, wanamageuzi, na wadau wengine wote tuchangie hoja hii muhimu. Hebu tulikoke hili jiko la mabadiliko vichwani mwa watz. Badala ya kusema tu tuwe na katiba mpya, tupendekeze pia ni kwa nini tunaihitaji, na iweje. Hii itasaidia kusensitize umma.
Napendekeza tuanze na maeneo ambayo tunadhani katiba mpya itahitaji kucover. Kwa upande wangu nitaje machache:
1. Muundo wa muungano na mgawanyo wa madaraka
2. Ukubwa wa madaraka ya raisi, mf. asiteuwe baadhi ya watu katika nafasi inayotakiwa kuwa huru kama Mkurugenzi wa TAKUKURU, Tume ya taifa ya uchaguzi, Wakuu wa mikoa na wilaya nk.
3. Bunge liwe la uwakilishi wa wananchi kwa 100% pasiwepo viti maalum wala viti vya kuteuliwa na raisi, tena wabunge wasifungwe na vyama vyao katika kuibana serikali, wawe huru, kusiwepo na uwezo wa chama kilichoshika dola kuwashinikiza wabunge wao kukubaliana na matakwa ya serikali palipo na maslahi ya taifa.
4. Mfumo wa uwajibikaji kwenye utendaji wa mihimili mikuu ya dola
5. Mfumo huru wa kupata viongozi, yaani tume huru ya uchaguzi, uwezekano wa kupinga matokeo ya urasi, openness and transparency kwenye uchaguzi.
Tafadhali ongeza, kosoa jadili challenge, ali mradi tupanue hoja. Let's brainstorm friends.
Katika hali hii nadhani think tanks wa nchi hii ni wakati muafaka kuijuza jamii ni kwa nini tuwe na katiba mpya, kwa nini tunadhani hii ya sasa imepitwa na wakati, na katiba mpya tunadhani izingatie mambo gani tunayodhani yanahitajika sasa. Nawaita akina political analysts, wanamageuzi, na wadau wengine wote tuchangie hoja hii muhimu. Hebu tulikoke hili jiko la mabadiliko vichwani mwa watz. Badala ya kusema tu tuwe na katiba mpya, tupendekeze pia ni kwa nini tunaihitaji, na iweje. Hii itasaidia kusensitize umma.
Napendekeza tuanze na maeneo ambayo tunadhani katiba mpya itahitaji kucover. Kwa upande wangu nitaje machache:
1. Muundo wa muungano na mgawanyo wa madaraka
2. Ukubwa wa madaraka ya raisi, mf. asiteuwe baadhi ya watu katika nafasi inayotakiwa kuwa huru kama Mkurugenzi wa TAKUKURU, Tume ya taifa ya uchaguzi, Wakuu wa mikoa na wilaya nk.
3. Bunge liwe la uwakilishi wa wananchi kwa 100% pasiwepo viti maalum wala viti vya kuteuliwa na raisi, tena wabunge wasifungwe na vyama vyao katika kuibana serikali, wawe huru, kusiwepo na uwezo wa chama kilichoshika dola kuwashinikiza wabunge wao kukubaliana na matakwa ya serikali palipo na maslahi ya taifa.
4. Mfumo wa uwajibikaji kwenye utendaji wa mihimili mikuu ya dola
5. Mfumo huru wa kupata viongozi, yaani tume huru ya uchaguzi, uwezekano wa kupinga matokeo ya urasi, openness and transparency kwenye uchaguzi.
Tafadhali ongeza, kosoa jadili challenge, ali mradi tupanue hoja. Let's brainstorm friends.