Maendeleo mapya: Mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Uzalendo

Watanzania walio wengi sasa, hata wale wa ccm, tofauti na siku za nyuma wanaonekana kuwa na mwamko wa kutamani katiba iandikwe upya. Nasema IANDIKWE UPYA sio hii iliyopo itiwe viraka. Kwangu mimi hii ni dalili ya kukua kutoka kwenye hatua moja ya kidemokrasia na mwamko wa kisiasa hadi nyingine. Lakini pia nadhani ni dalili kubwa ya mabadiliko ya mazingira ya kisiasa, kiuchumi, na kila nyanja. Watu wameanza kugundua sasa kuwa shuka ambayo wamekuwa wakijifunika haiwatoshi tena, kwani wamerefuka zaidi, tena shuka hii imechakaa. Wanataka mpya.

Katika hali hii nadhani think tanks wa nchi hii ni wakati muafaka kuijuza jamii ni kwa nini tuwe na katiba mpya, kwa nini tunadhani hii ya sasa imepitwa na wakati, na katiba mpya tunadhani izingatie mambo gani tunayodhani yanahitajika sasa. Nawaita akina political analysts, wanamageuzi, na wadau wengine wote tuchangie hoja hii muhimu. Hebu tulikoke hili jiko la mabadiliko vichwani mwa watz. Badala ya kusema tu tuwe na katiba mpya, tupendekeze pia ni kwa nini tunaihitaji, na iweje. Hii itasaidia kusensitize umma.

Napendekeza tuanze na maeneo ambayo tunadhani katiba mpya itahitaji kucover. Kwa upande wangu nitaje machache:

1. Muundo wa muungano na mgawanyo wa madaraka

2. Ukubwa wa madaraka ya raisi, mf. asiteuwe baadhi ya watu katika nafasi inayotakiwa kuwa huru kama Mkurugenzi wa TAKUKURU, Tume ya taifa ya uchaguzi, Wakuu wa mikoa na wilaya nk.

3. Bunge liwe la uwakilishi wa wananchi kwa 100% pasiwepo viti maalum wala viti vya kuteuliwa na raisi, tena wabunge wasifungwe na vyama vyao katika kuibana serikali, wawe huru, kusiwepo na uwezo wa chama kilichoshika dola kuwashinikiza wabunge wao kukubaliana na matakwa ya serikali palipo na maslahi ya taifa.

4. Mfumo wa uwajibikaji kwenye utendaji wa mihimili mikuu ya dola

5. Mfumo huru wa kupata viongozi, yaani tume huru ya uchaguzi, uwezekano wa kupinga matokeo ya urasi, openness and transparency kwenye uchaguzi.

Tafadhali ongeza, kosoa jadili challenge, ali mradi tupanue hoja. Let's brainstorm friends.
 
Napenda kuwambia WaTanzania wenzangu kuwa ninaunga mkono moja kwa moja madai ya msingi ya Chama cha Chadema kuhusiana na ukarabati au utungwaji upya wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na pia uundwaji upya wa tume ya Uchaguzi ya Taifa ,Ninachowataka viongozi hawa wasitegemee Chama kingine wao kama Chama wasonge mbele na madai haya bila ya kurudi nyuma ,au kusimama kama ilikuwa mwendo mdundo wakati wa kampeni za Uchaguzi sasa ni wakati mwendo mruko juu ya kuwashawishi wananchi ili kuungwa mkono,na wasingojee au kusubiri kwani tabia iliyojengwa ndani ya utawala wa CCM ni wa kusema muda hautoshi, hivyo tuna kipindi cha miaka mitano katika kurekebisha na kuunda upya mambo haya nadhani tunahitaji kama mwaka mmoja au miezi sita tu ikiwa tutatumia wataalamu kutoka nje na kuipitisha Katiba.

Je wewe :angry:
 
hivi jamani kama si chadema haitaanzisha move hii ..... asasi gani au chama gani chenye nguvu ya kupush hii motion ya kupata katiba mpya kabisa wala si kukarabati kwa vile tuliyonayo hata watu wa nje wanasema ni "Obsolete" nani tena atathubutu.. wajameni ... tuwaunge mkono chadema...tukipata hii twaweza kuendelea na kazi nyingine

kwa maoni yangu ..... Death penalty is not friendly with the modern life and progressive life... scrap this Act... soon

Wewe unafikiri ipi haifai..??????
 
Maalim Mwiba kulikoni? Hongera kwa wazo zuri ambalo naona linaitakia mema Tanzania.

Uongozi wa CHADEMA wanatakiwa wakutane na Muungano wa Asasi za Kiraia ili kuona namna watakavyo-push agenda ya madai ya Katiba Mpya kwa kushirikiana. Ni rahisi sana kuzitumia AZAKI kupeleka agenda kwa wananchi kwa kuwa AZAKI zimesambaa nchi nzima na zinajihusisha na mambo tofauti japo common goal ni kuwasaidia wanyonge na kusimamia haki. Kwa kuwa swala hili linagusa vyama vyote vya siasa, siyo vibaya ku-reach out ili kupata support ya vyama vingine ambavyo vina nia ya kutaka mabadiliko.

Pili, Wabunge wa CHADEMA kwa kushirikiana na wabunge wa upinzani ambao wako tayari, waandae Hoja Binafsi ya kuitaka Serikali ianzishe mchakato wa mabadiliko ya katiba. Ili kuweka uzito, watumie hukumu ya Mahakama ya Rufani kuhusu mgombea binafsi, pia kasoro zote zilizojitokeza wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka huu na pia mapendekezo ya Tume ya Nyalali ya kufuta baadhi ya sheria kandamizi.

Iwapo, Mama Makinda na CCM yake watagoma, hapo ndipo watakuwa wametoa plat form nzuri ya mahali pa kuanzia ili kupeleka agenda ya madai ya Katiba Mpya kwa wananchi. Hili la hoja binafsi inabidi lianze mapema sana ikiwezekana Bunge la Januari au April mwakani. Lengo la kuanza mapema ni kuhakikisha kwamba within the first two yrs kiwe kimeeleweka. CCM ni wajanja sana, hoja ikichelewa kwenda wanaweza kuanza kujitetea kwamba mchakato wa mabadiliko ya Katiba unahitaji muda mrefu sana, so wanaweza kusema watabadilisha after 2015.

Wananchi wana kiu kubwa sana ya mabadiliko, iwapo mjadala utazimwa bungeni then ni rahisi sana kuupeleka kwa wananchi. Hoja za Buzwagi na EPA ziliwatesa sana na ziliwaweka CCM kwenye defensive mode miaka yote 3. Kwa hiyo wanaweza kuwa makini sana kwenye kujibu hoja binafsi, na sidhani kama wako tayari kuwa kwenye defensive mode tena kwa kuwa inawagharimu sana.

Wananchi wameishatuma salaam kupitia uchaguzi wa mwaka huu. Watu kukesha wakilinda kura ni dalili kwamba hawana imani na tume ya uchaguzi, ili kuepusha nguvu ya wananchi iliyoonyeshwa Ubungo, Arusha, Mwanza, Mbeya na kwingineko tunahitaji kuwa na tume huru.
 
nilichasema kwenye thread hoja itashindikana mjengoni kwa ajili ya collective responsibility... dawa ni push ya popular party pamoja na wananci kushinikiza serikali ...kubadili katiba
 
msaada sheli jamani,naomba wataalamu mnidadavulie kwa umakini kidogo,hivi katiba ya sasa,mapungufu yake ni nini hasa?
kwanza nijihami kidogo,si maanishi haina mapungufu,nadhani yapo,ila sijui hata moja.nipeni shule hapo wapendwa
 
msaada sheli jamani,naomba wataalamu mnidadavulie kwa umakini kidogo,hivi katiba ya sasa,mapungufu yake ni nini hasa?
kwanza nijihami kidogo,si maanishi haina mapungufu,nadhani yapo,ila sijui hata moja.nipeni shule hapo wapendwa

Ili watu wengine wadadvue nawe uelwe ni vema ukijipa Head Start kwa kuisoma kwanza.

http://www.tanzania.go.tz/images/katibamuungano.pdf

Baada ya kuisoma bila shaka utakuwa na maswali ya moja kwa moja.
 
Sitaki kuamini hivyo...lakini Makyembe na Sitta kuingizwa kwenye baraza la mawaziri haijakaa vizuri.....

Mara ya kwanza nilifikiria itakuwa pigo kwa mafisadi kwamba itakuwa message sent kwamba JK yupo pamoja na kundi la anti-mafisadi (Sitta, Makyembe na wengine) lakini on second thought ndio ni kawa na mawazo kama yako...any way let us wait and see....
 
Watanzania kama kweli tunahitaji mabadiliko lazima tusimamie kidete mabadiliko ya katiba. Tunatakiwa kufahamu kuwa kiburi kilichoko ndani wa viongozi wa chama tawala ni kwa sababu katiba inawalinda. Uhuru wa kuongea utulinde na ikiwezekana tuandamane nchi nzima ili vilio vya walalahoi visikike.
 
Naunga mkono hoja lazima ibadilishwe kwa gharama yeyote ile hata ikibidi kuingia barabarani tuingie tuu,watu wanaviburi kweli anadhani anaendesha nchi kama kampuni binafsi inaudhi kweli
 
Sitta abaki benchi kupambana na ufisadi na kusaidia kusukuma mbele wazo la kubadili katiba na kuwa na tume huru
 
Mkubwa uko sahihi kabisa! Mimi nashangaa kwa nini Vyama pinzani vinashangaa kushindwa kila uchaguzi!!.. Hivi kweli itoke siku Yanga waandae mechi na Simba, halafu uwanja uwe wa Yanga... Refa atafutwe na Yanga... Obvious washabiki watakuwa wa Yanga... Halafu Simba ipate nafasi ya kushinda!!!!!? No way!!!... Mazingira ya kisiasa kwa vyama pinzani ni mabaya zaidi ya mno!!! Na hii yote ni kwasababu ya KATIBA FEKI!!!
 

Mimi nakuunga mkono mia kwa mia! Hapa kinachotakiwa ni kufanya kweli na sio kuendelea kurumbana. Strategies ziwepo...well organized plans then tunaingia uwanjani tukiwa full combat...!
 

Hapo mkuu umenena haswa!!!
Kwa hiyo umetangaza vita, mapambano ya kudai katiba mpya.
Basi kwa njia hiyo ebu tuige wenzetu Wakenya walifanyaje mpaka katiba mpya ikapatikana. Kwanza inahitajika taasisi zisizo za kiserikali (Km; Kama yule mama Ananilea Nkya na taasisi yake) Wanasheria (Tanzania Law Society) na wengineo pomoja na political parties. Wafanye kwa kushirikisha wananchi wenye nia njema na Watanzania, makongamano, midahalo na shughulizingine zenye mwelekeo wa kuelimisha jamii NA KUHAMASISHA juu ya kuwa na KATIBA bora ya kumkomboa Mtanzania toka lindi la umasikini. Uzuri wake ni kwamba Watanzania wa sasa wameanza kuamka, wataelewa ni kitu gani tunatakiwa kufanya.Midahalo mingi wakati wa uchaguzi mbona watu wengi tuu walihudhuria. Mbona hamasa za AIDS na Maralia zinaeleweka? Tusianze kukata tamaa kabla hatujaanza ebu wale ndugu walio mbele (politicians and non govmental org's na wanasheria) watoe dira.THINGS WILL FALL IN PLACE. (BOMAS OF KENYA)
 
Ndg zetu Wakenya wanaotutakia mema Watanzania hebu tupeni ushauri na maelekezo!!!
 

Hapo umenena Ndg Yangu Silver25. KATIBA MPYA NDILO JIBU LA UMASIKINI WETU. Tusiyumbishwe na siasa za kifisadi, malengo yetu yawe ni katiba mpya. Sio kuwa na baraza la mawaziri hamsini. Yaanai mtu anajipangia tu anataka wakubwa wenzie wangapi!
Jibu la yote hayo ni katiba definitive self explanatory on the size and type of goverment we should have. VIVA KATIBA MPYA.
 
Mi naona kuna haja ya Wananchi Watanzania Wazalendo na wenye uchu wa Maendeleo Tanzania, tunge andamana kila mtu Mkoani kwake kwa siku moja kwamfano Dar Jtatu, basi Tanzania nzima J3

MAANDAMANO NDO SULUHISHO LA KSTAKABALI WA KATIBA MPYA
 
...Bila ya kutaja matatizo ya katiba yetu, ningependa kueleza
sema ni nini tatizo la hiyo Katiba!

Hivi unawezaje kuwa na theme ya kudai kubadilisha Katiba lakini huwezi kusema jack squat about what's wrong with the Katiba????

Kila mtu katiba ibadilishwe katiba ibadilishwe katiba ibadilishwe... NINI KIBADILISHWE? MTU HAJUI, HAJAWAHI KATA KUISOMA
 
Mkakati wa kudai Katiba mpya ya nchi ya Tanzania.

Wadau, baada ya kipindi cha uchaguzi kumalizika, kila mtanzania mwenye nia njema na nchi hii, atakubaliana na mimi kuwa kwa sasa tunaanza kudai katiba ili yale yaliyo tusibu kwenye uchaguzi ulioisha, yasije tukuta tena, make bado nasikia kizungu-zungu cha tume ya uchaguzi kututajia madudu badala ya kutoa hali halisi na hatimaye kuwa na kiongozi aliye chomekwa na tume ya uchaguzi ya ccm.

Naomba tuchangie mapendekezo ya hatua za kuchukua ili tuwapelekee watu wetu ambao wamesha onja harufu ya mjengoni ili kwamba Bunge lijalo waanzishe mchakato.
  1. Maandamano ya amani ya kudai Katiba mpya, itakayo ainisha mambo muhimu likiwemo
  • Muundo wa muungano- Sio mtu kutoka Zanzibar anakuwa mbunge wa Jamhuri wakati mtu kutoka bara, haruhusiwi hata kutembelea Zanzibar.au kuwa mbunge huko Zanzibar.
  • Mzanzibar anakuwa waziri wakati mbara hawezi kuthubutu, kwanini kunakuhongana?
  • Idadi ya uwakilishi kwenye bunge, mfano jimbo la ubungo, mbunge ni mmoja anayewakilisha watu zaidi ya laki moja, wakati Zanzibar mbunge mmoja anawakilisha takribani watu 5,000. Huu uwiano unanipa kichefuchefu!!!!!!!!!!
  • Wanafunzi wanao lipiwa kutoka Zanzibar kusomea vyuo vya bara, wao wanalipiwa moja kwa moja na serikali, wakati wa bara wanashinda wanakimbizana na fomu za mikopo ya HESLB na wanakosa muda wa ku-concentrate na masomo.
  • Kodi ya kuagiza kama magari kupitia Zanzibar kuwa tofauti na ile ya bara, wakati wanadanganya kuwa tuliungana!!!!!


BILA KUANZA HUU MCHAKATO TUME ITAKUWA KILA MWAKA INATUTANGAZIA RAIS FEKI.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…