Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Mbona mnatumia nguvu nyingi sana kujiita Rais wa wanyonge ,,kwa iyo wasiokuwa wanyonge hawana Rais hapo ndipo mnapoleta matabaka Rais wa wanyonge na je wale wenye nguvu hawana. Kama Mazuri yapo yaacheni yajitangaze yenyewe. Ngumu kumeza
 
Ujinga ni mjukuu wa uoga yule aliyemzaa chuki ambae ni binamu yake na unafiku

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengi hawakumwelewa Rais Magufuli alisitisha safari za nje ya nchi na kuwataka watanzania kuachana na utegemezi wa misaada ya wazungu.

Ikumbukwe hata mchicha na matunda tuliletewa kutoka Afrika ya kusini na sukari ilitoka Brazil.

Najaribu kufikiria yale mafungu ya wabongo yaliyokuwa yanapishana angani daily kama yasingezuiwa hiyo importation ya Corona kutoka Ulaya na uchina ingekuwa kubwa kiasi gani?

Je, mahitaji yetu ya kibajeti yaliyowategemea wazungu kwa asilimia 60 leo hii tungeyapataje?

Je, matibabu ya viongozi na watu mashuhuri yaliyotegemea India na Ulaya kwa 90% leo wangeendaje?!

Maswali ni mengi sana kwa kweli lakini naishia hapo.

Mungu mbariki Kiongozi huyu uliyemchagua Dr Magufuli.

Maendeleo hayana vyama!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…