Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Rais Dk. Magufu ana nia ya kweli kulijenga taifa imara. Wiki mbili sasa nipo Arusha asilimia kubwa ya wakazi wa Arusha wanaanza kumkubali hasa ile yotuba yake ya Ijumaa tar20 bungeni. Kila la kheri Rais wetu mpendwa.
Hata usipoangalia historia ya utendaji wa Rais Magufuli, ukimwangalia usoni utagundua ana maanisha kwa vitendo kile anachokisema.
 
Kama Magufuli ataendelea hivyo basi watakaoumia ni CCM na sio wapinzani.
CCM miaka yote inawekwa madarakani kwa rushwa na pesa za rushwa zinapatikana kupitia mikataba feki na kufanya manunuzi kwa bei ya kuruka.
Pesa nyingi zinazoiweka CCM madarakani ni zile za kuchota kwenye mashirika ya umma kinyemela.

Sasa kama Magufuli atagoma kufanya huo ushetani uliofanywa na watangulizi wake basi ni dhahiri CCM itaporomoka huku Magufuli akibakia na kura zake mkononi na UKAWA watapaa kwa kasi kwani wabunge wengi walioko CCM wanaingia madarakani kwa mahela ya wizi wanayochoteana huko juu. Ndio maana walinunua masanduku ya ziada ya kura na kupiga kura kabla na kuzigawia kila majimbo .

Hivi leo Magufuli akisema anataifisha Majumba waliyogawana huku serikalini watakaolia ni UKAWA CCM .
Leo Magufuli akisema anawatimua kazi hao wafanyakazi wenye Vyeti feki watakaoumia ni CCM mana watoto wao wengi ndio wamefoji vyeti na wameajiriwa kwenye mashirika na idara mbalimbali. UKAWA watashangilia kuona kuwa walichokua wanakipigania kinatekelezwa.

Amini usiamini baada ya miaka miwili maadui wakubwa wa Magufuli watakua wapo ndani ya CCM.

Vigogo wengi wa CCM ndio wanaomiliki majumba na biashara nyingi za malori.
Leo hii Magufuli akitengeneza Reli na kuboresha usafirishajo wa treni watakaolia na kufilisika ni wanachama na vigogo wa CCM na sio UKAWA.
Leo hii pakiwa na katiba na sheria bora watakaoumia ni CCM maana walishazoea ulaghai na uovu .

Jambo lolote jema litakalofanywa katika hili taifa litawaumiza sana CCM na mabosi wao waliokua wanawakuwadia mali za watanzania. UKAWA hawajawahi kunufaika na mikataba feki na wawekezaji.
Mirija ya unyonyaji ilikua inatumiawa na CCM na watoto wao.

Leo hii kuna wabunge,waandishi wa habari na wanachama wa CCM wanaojifanya sana kumuunga mkono Mh.Magufuli lakini wamelenga madaraka ya uwaziri na sio maemdeleo kwa wananch .Hawa ni wanafiki na wote wako CCM na sio UKAWA.
Hata Kikwete walimsifu na kutoa kila tamko jema juu yake huku wakilenga madaraka na walipopata wakageuza nchi kuwa shamba la bibi.
Baada ya kipindi hiki cha mgao wa vyeo ndani ya serikali ukipita basi hawa apambe watapukutika sana

Unaona mbali sana. Great!
 
Mwandishi Mwingereza aitwaye Lewis Carroll aliwahi kusema, ''If you don't know where you are going, any road will get you there''.

Wakati wa kampeni za uchaguzi Mkuu, tuliwasikia UKAWA wakimponda mgombea Urais wa CCM kama hana lolote kwa sababu CCM ni ile ile. Kuna wengine walidiriki kusema CCM imeishiwa pumzi na iwekwe kando. Wengine wakasema kama CCM ni kitanda chenye kunguni kama Dk. Magufuli anavyosema, basi wao hawataki kuhangaika kuwauwa kunguni bali watakichoma moto na kununua kitanda kingine.

UKAWA walicheka na kumdhihaki Rais Magufuli aliposema amepania/kudhamiria kuleta mabadiliko bora pindi atakapoingia madarakani kwa kubana matumizi ya serikali, kuongeza mapato ya serikali, kuboresha mfumo wa utendaji na ufanisi, kupitia kodi na ushuru unaowaumiza wakulima, wafugaji na wavuvi, kupitia upya baadhi ya sheria zinazoleta kero kubwa kwa wananchi, kuunda serikali ndogo, kupunguza au kumaliza kero za watumishi wa umma na kupendekeza muundo wa kitaasisi ili kutekeleza kwa ufanisi ahadi zake.

Two weeks down the line, UKAWA kwa sasa wameanza ''kudandia treni'' ya Rais Magufuli kwa mbele wakati huo huo baadhi yao hawajatuambia kama wanamtambua ni Rais wa Tanzania.

Eti wanadai wameanza kumkubali Rais Magufuli kwa sababu ameanza kutimiza Ilani ya UKAWA! Wamesahau ni wiki mbili zilizopita walikuwa wanasema Rais Magufuli hana lolote jipya katika mchango wa mabadiliko bora nchini. Kuna wengine kwa sasa watadai Rais Magufuli ni UKAWA. Wanachofanya kwa sasa ni kutaka kuhalalisha hii dhana ya kuitwa nyumbu na bendera fuata upepo!

Kabla ya viongozi wa UKAWA kuanza 'kudandia treni' ya Rais Magufuli kwa mbele, lazima wawaombe radhi Watanzania kwa kutaka kuliangamiza taifa kupitia mgombea wao wa Urais wa Tanzania ambaye walituletea na kuanza kutuuzia kwenye gunia wakati wanafahamu ni mra rushwa, fisadi na hafai kuwa Rais wa Tanzania.

Mtu muungwana ni yule anayeomba radhi na pia taifa la waungwana ni lile linalosamehe baada ya kuombwa radhi.

UKAWA kabla hamjaungana na juhudi za Rais Magufuli, lazima muombe radhi kwa wapiga kura wengi, otherwise, endeleeni kusimama na Lowassa mwenye mabadiliko fake yakisaidiwa na Ilani yake ya Uchaguzi yenye vipao mbele vitatu, 1)Elimu, 2)Elimu na 3)Elimu.

Kwa wale wanaoamini uwepo wa Mwenyezi Mungu, kwa sasa wanasema Mwenyezi Mungu bado analipenda Taifa letu kwa kutuletea Rais Magufuli.

Utamkubali wewe huyo makofuri wako siye rais wetu ni lowasa
 
Nakumbuka UKAWA walisema wakipunguza Safari tu watoto wanaweza kusoma bure hadi Chuo kikuu.Halafu acheni utahahira bila upinzani msingekuwa na Magufuli.Na ameanza Kweli kushughulikia vile vitu vilivyokuwa vikipigiwa kelele na UKAWA.Hii ni mafanikio kwa UKAWA na sasa kibao kimebadilika CCM ndo WATAISOMA no make ndo walikuwa wafaidika wa hizi Safari. Nia ya ukawa Pamoja na Elimiu,ilikuwa ni kuhakikisha serikali inapunguza matumizi yake,huduma Za afya,Maji n,k.Sasa Magufuli kaanza navyo.Watu walikuwa wakiwa beza sasa wanaamini UKAWA kelele zao hazikuwa Za bure.

Mkuu tanzania kwa sasa inaongozwa na ilani za ukawa wapende wasipende
 
Rais Magufuli siyo Rais Kikwete.

Dhama za utawala wa Rais Magufuli ni tofauti na Rais Kikwete.

Jaribu kuangalia utendaji wa Rais Magufuli kuanzia siku aliyoteuliwa kuwa Naibu Waziri.

Angalia jinsi alivyoweza kupitia mchakato wa kuteuliwa kuwa mgombea Urais.

Rais Magufuli hakuwaahidi watu mbali mbali vyeo kabla ya kuchaguliwa kuwa Rais. Hana makundi ndani ya CCM na serikalini. Makundi ni sumu katika utendaji na mafanikio katika kufikia malengo.

Kama huyaoni makundi ndani ya ccm basi wewe ni kipofu
 
Tukubali bila ya upinzani tusingrmpata Magufuli, bila upinzani tusingekuwa tunamsifu Magufuli leo , bila upinzani tusingefika hapa! Upinzani uendelee kuwepo ili kuwe na ushindani na wananchi wafaidike
 
Huyooo! zasiku wewe kambi kuyuu ya NYUMBU wa LOLIONDO hahaha mwakahuu matunduyote yameziba na yule mdoli wenu anaanza kupotea

Tuna wabunge wa majimbo takriban 40 nyinyi na kiongozi wenu mkuu ndio mwakilishi wenu, chama kizima mbunge mmoja teeeeeeeh, teeeeeeh, teeeeeeh😆
 
Hahaha wanatafuta imani ya watu
Sidhani kama wataipata tena imani kubwa kama waliyoipata kabla ya ujio wa Lowassa na genge lake ndani ya CHADEMA.

Mbowe aliwachuuza wana CHADEMA wengi kwa kumkaribisha Lowassa na kumpa tiketi ya kugombea Urais.

Kuna watu wengi sana ambao waliweka imani zao kwa CHADEMA kwa sasa hawawezi kumsamehe Mbowe kwa kuwachuuza!
 
Tukubali bila ya upinzani tusingrmpata Magufuli, bila upinzani tusingekuwa tunamsifu Magufuli leo , bila upinzani tusingefika hapa! Upinzani uendelee kuwepo ili kuwe na ushindani na wananchi wafaidike
Hakuna mwenye fikra pana anayesema upinzani lazima ufe lakini vile vile siamini kama upinzani ndiyo umewezesha Rais Magufuli kuteuliwa kuwa mgombea Urais kwa tiketi ya CCM.

Ninaamini wapinzani wamefanya kila linalowezekana kuhakikisha Dk. Magufuli hachaguliwi kuwa Rais wa Tanzania.
 
Wakimtambua JPM watakuwa washamsaliti LOWASA
Wakimtambua lini wakati bungeni walikuwa wanajadili hoja za kutengua kanuni ili wawakaribishe wageni ambao siyo wabunge wa JMT wakati wa hotuba ya ufunguzi wa bunge la 11.

Kwa sasa wamehamisha magori kwenye hoja ya Rais wa Zanzibar!

Kwa ujumla, UKAWA hawafahamu kile wanachokisimamia kwa sasa kwa sababu wengi wao hawakutegemea kama baada ya uchaguzi wataendelea kuwa wapinzani. Wengine walianza kumuita Lowassa ni Rais wakati hata wananchi hawajapiga kura.
 
nasema kusanyeni kodi haraka
nasema msisamehe kodi
nasema nafuta safari za nje zinatumia gharama nyingi
nasema hela ya sherehe wa uzinduzi wa bunge nunua vitanda peleka kule pesa hakuna hapa
nasema tupungunze matumizi ya pesa kama peni elfu kumi acheni utani mishahara inatungojea hapo mbele
au tufute sherehe za uhuru tujazie halafu tuwakwepe na kina sharif hamad sio
sasa tangazeni kila tv nabana matumizi ya pesa za umma sawa,ndio mkuu

nimesahau kipi?
 
Fikra mgando kama zako ni hatari hata katika mipango yako ya kujiletea maendeleo.
 
Nakumbuka UKAWA walisema wakipunguza Safari tu watoto wanaweza kusoma bure hadi Chuo kikuu.Halafu acheni utahahira bila upinzani msingekuwa na Magufuli.Na ameanza Kweli kushughulikia vile vitu vilivyokuwa vikipigiwa kelele na UKAWA.Hii ni mafanikio kwa UKAWA na sasa kibao kimebadilika CCM ndo WATAISOMA no make ndo walikuwa wafaidika wa hizi Safari. Nia ya ukawa Pamoja na Elimiu,ilikuwa ni kuhakikisha serikali inapunguza matumizi yake,huduma Za afya,Maji n,k.Sasa Magufuli kaanza navyo.Watu walikuwa wakiwa beza sasa wanaamini UKAWA kelele zao hazikuwa Za bure.
Hakuna anachokifanya Rais Magufuli kiko nje ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM na ahadi zake za hapo kwa hapo.

Kama anachokifanya kinakuwa pia kiliahidiwa na UKAWA basi inaonyesha it's a pressing issues to our nation.

Rais Magufuli ni CCM na ataendelea kuitumikia serikali ya CCM iliyopewa ridhaa ya kutawala na wapiga kura wengi.

Nani amesema bila upinzani asingepatikana Rais Magufuli?
 
Back
Top Bottom