Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Mkuu ni kweli usemacho Mhe JK alipolizinduwa Bunge la tisa hotuba yake ya kwanza kuhutubia Bunge alisema "watu wanasema Mimi mpole nasema nitakuwa mkali" lakini hakuwa mkali mpaka tumemsikia Mhe Mnyika alisema Rais ni dhaifu na Serikali dhaifu.
# SASA KAZI TUU #
Kuna baadhi ya watu bado wanadhani anachokifanya Rais Magufuli ni nguvu za soda!

Kama hawawezi kuisoma historia yake katika utumishi wa Umma, wataendelea kudhani ni nguvu za soda.
 
Magufuli kawaweka UKAWA kwenye wakati mgumu sana, kwa sasa hawajua washikie ajenda gani, ya ufisadi isharudi CCM siku nyingi, i kama wamekata tamaa hivi, mie sioni hata haja ya uchaguzi wa Raisi 2020, soon CHADEMA itakuwa kama NCCR na Lowassa kuwa kama Mrema
Ajenda zilizobaki kwa sasa kama ile inayoendelea Mwanza!

Chama kimekuwa cha wanaharakati badala ya wanasiasa wanaojiandaa kuongoza nchi.
 
Magufuli atatusaidia kuufuta upinzani..

Ni kazi yetu watanzania kuufuta upinzani wa makelele, fujo na vioja na kuujenga upinzani wa hoja.
Upinzani ni muhimu sana kuwepo lakini lazima upinzani uwe wa hoja.
 
Hakuna cha maana ulichoandika zaidi ya mipasho nadhani umesahau kwamba kampeni zimeisha sasa ni kujenga nchi.
 
Kama Magufuli ataendelea hivyo basi watakaoumia ni CCM na sio wapinzani.
CCM miaka yote inawekwa madarakani kwa rushwa na pesa za rushwa zinapatikana kupitia mikataba feki na kufanya manunuzi kwa bei ya kuruka.
Pesa nyingi zinazoiweka CCM madarakani ni zile za kuchota kwenye mashirika ya umma kinyemela.

Sasa kama Magufuli atagoma kufanya huo ushetani uliofanywa na watangulizi wake basi ni dhahiri CCM itaporomoka huku Magufuli akibakia na kura zake mkononi na UKAWA watapaa kwa kasi kwani wabunge wengi walioko CCM wanaingia madarakani kwa mahela ya wizi wanayochoteana huko juu. Ndio maana walinunua masanduku ya ziada ya kura na kupiga kura kabla na kuzigawia kila majimbo .

Hivi leo Magufuli akisema anataifisha Majumba waliyogawana huku serikalini watakaolia ni UKAWA CCM .
Leo Magufuli akisema anawatimua kazi hao wafanyakazi wenye Vyeti feki watakaoumia ni CCM mana watoto wao wengi ndio wamefoji vyeti na wameajiriwa kwenye mashirika na idara mbalimbali. UKAWA watashangilia kuona kuwa walichokua wanakipigania kinatekelezwa.

Amini usiamini baada ya miaka miwili maadui wakubwa wa Magufuli watakua wapo ndani ya CCM.

Vigogo wengi wa CCM ndio wanaomiliki majumba na biashara nyingi za malori.
Leo hii Magufuli akitengeneza Reli na kuboresha usafirishajo wa treni watakaolia na kufilisika ni wanachama na vigogo wa CCM na sio UKAWA.
Leo hii pakiwa na katiba na sheria bora watakaoumia ni CCM maana walishazoea ulaghai na uovu .

Jambo lolote jema litakalofanywa katika hili taifa litawaumiza sana CCM na mabosi wao waliokua wanawakuwadia mali za watanzania. UKAWA hawajawahi kunufaika na mikataba feki na wawekezaji.
Mirija ya unyonyaji ilikua inatumiawa na CCM na watoto wao.

Leo hii kuna wabunge,waandishi wa habari na wanachama wa CCM wanaojifanya sana kumuunga mkono Mh.Magufuli lakini wamelenga madaraka ya uwaziri na sio maemdeleo kwa wananch .Hawa ni wanafiki na wote wako CCM na sio UKAWA.
Hata Kikwete walimsifu na kutoa kila tamko jema juu yake huku wakilenga madaraka na walipopata wakageuza nchi kuwa shamba la bibi.
Baada ya kipindi hiki cha mgao wa vyeo ndani ya serikali ukipita basi hawa apambe watapukutika sana


Na iwe hivyo kabisa ili mageuzi aliyoahidi kuyafanya serikalini na ndani ya CCM yaweze kufanyika kiuhalisia ili chama hiki kilichowekewa misingi na BABA YETU WA TAIFA kirejeshe heshima yake.
Naamini pia kitajenga wanachama wapya wenye uchungu na nchi yao na ambao hawatafanya siasa za uchumia tumbo bali siasa za kizalendo zinazokubali kukosolewa na kutenda yale ambayo yanatokana na sauti za watanzania kupitia vyama vyote vya siasa, ndio maana ya kuwa na serikali sikivu.
 
Sijaelewa unachokimaanisha?
Unamaanisha maisha ya watanzania yamekuwa mazuri baada ya magu kuingia?
 
Hivi haya anayoyatekeleza Magufuli yalikuwa yanapigiwa kelele na kina nani???

Magufuli sio raisi wa CCM ni raisi watanzania wote, alisema PEOPLES' POWER impe pia kura zake ili aje ayafanye hata hayo wanayoyasema, ndio maana yupo hapo unapomwona leo.

Kama wewe hukumpa wenzako walimpa kwa imani hiyo, usishangae kwa yanayoendelea yapo ndani ya ahadi zake na ilani ya CCM.
 
Wakati tuki furahia haya ya nagufuli , tuna muomba amalize ya zanzibar maalim aapishwe amsaidie naye aondoe uoza huko znz..seif hataki mzaha na kazi ...mpe haki yake Tanzania kwa ujumla ibadikike

inshallah atapewa tu, tuwaombee uzima tu
 
Ndio mahana nimepata jibu la mvua zilizonyesha tangu alipoteuliwa mpaka kuapishwa mungu anampango na watanzania kuusu mateso tuliyopitia kwa uongozi uliopita sasa katuletea Neema tunakushukuru sana mungu kwakutujua cc watanzania dhid ya utawala uliopita
 
NAONA KWA MBALI MH MAGUFULI AKIANGUSHWA NA WALIOMUWEKA, TUNGESIKIA MAANDAMANO YA KUMPONGEZA KAMA ILIVYOKUWA MIAKA ILIYOPITA LAKINI HILI NASHAURI TULIFANYE SISI UKAWA

Kwenye twitt za kenya wanapendekeza wamwombe ahamie kenya au hata kwa kumteka Mh Magufuli ili akagombee urais kenya kwani alichokifanya siku 20, rais wao hajafanya miaka 3.

Tafikiti pia zinaonyesha kama ungefanyika uchaguzi kumchagua rais wa EA, MH magufuli angeshinda kwa kishindo..... na wengine wameenda mbali zaidi kwa kutaka nchi za EA ziunganishwe na BW Magufuli awe rais wetu

Binafsi simpongezi najua anafanya kile anachopaswa kukifanya na au matajario ya watanzania kwake

wana UKAWA tunashuhudia zaidi ya mabadiliko. Nimeamua kutoa langu la rohoni baada ya kusikia makontena zaidi ya 300 yamepitishwa bandarili bila kulipiwa ushuru.........................

hayo sijui ni kwa kipindi gani ...............................................

na mangapi hayajajulikana....................................................

Naamini ukwepaji kodi huu ni madeal ya wenye lumumba.................

kwani hatujasahau zile pembe za tembo zilizokamatwa na baadae ikajulikana kampuni iliyosafirisha ni vigogo wa lumbumba

tunasikia pia makampuni makubwa ya ukwepaji kodi yamefilisika kisa wanaogopa kuumbuliwa na msukuma huyu


Je lumumba watakuwa tayari kuona mirija yao ya pesa inakatwa?

Lazima wamamwonya kuwa sisi ndio tuliokuweka hapa na tunaweza kukuondoa......

NAKUMBUKA miaka michache wana lumumba walikuwa wakiandamana kwa namna ya kumpogeza lkn hayakuwa mambo mazito kama anayofanya mzee wa hapa kazi tu..............................................

Ndio maana nikatangulia kusema
"KWA MBALI NAMWONA MAFUGULI AKIANGUSHWA NA WALE WALIOMUINGIZA MADARAKANI".....

Kwani anakazi kubwa..... kwa miaka mitano haitoshi kupitisha fagio la chuma .........................

system imekufa bado hajaenda huko kwenye halmashauri.....................................................


MIMI MWANA MABADILIKO NAMWUUNGA MKOMO MH MAGUFULI NA NAMWOMBEA DUA................

Napendekeza tujadiliane tuandae MAANDAMANO YA KUMPONGEZA MWANA MABDAILIKO, KUMUUNGA MKONO MH MAGUFULI NI kuunga Mkono kauli yake "SERIKALI YA MAGUFULI"

na si serikali ya magamba
 
Kwa tathmini Fupi tu Jeshi LA watu Wanne (Raisi, Waziri mkuu, spika na makamu WA raisi) linatosha. Hili Jeshi limeonyesha uwezo mkubwa Kwa Kipindi hiki kifupi Kwa kuweza kufukunyua Madudu yaliyolindwa na team Kubwa Ya Utawala uliopita.

Kwa Haya machache napenda kutoa Maoni yangu kuwa Hakuna haja Ya mh. Raisi kuteua mawaziri.

Haya Ndio maoni tangu.
 
Mkuu nchi kubwa hii!!
Jambo muhimu ni kuwa na mawaziri wenye muono ule ule wa Magufuli!
 
Back
Top Bottom