kigogo warioba
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 6,048
- 9,398
hiyo tuzo ya uchapaji kazi bora imetolewa na taasisi gani?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa moyo wangu wote na kwa furaha ninamshukuru sana Mh Rais Magufuli kwa kuwa mchapa kazi bora kwa mwaka 2016. Amekuwa mfano wa kuigwa na kauli yake hapa kazi tu imeonyesha njia kwa kila kaya ndani ya taifa hili.
Wakati unaingia madarakani mnyonge hakuwa na haki kwa hakika wenye pesa walilitesa taifa ila kwa imani yako mbele ya Mungu wako na kanisa lako na kwa watanzania wote leo sauti ya mnyonge inanguvu kama radi.
Baba tunamshukuru Mungu pamoja na wazee waliokupotisha nec ili uwe kiongozi wa taifa hili. Mimi nasema hawakukosea wala haikuwa kwa bahati ila ukweli nikwamba Mungu alukuchaguwa tangu tumboni mwa mama yako kuliokowa taifa la tanzania. Hakika nasema wewe ndiwe yule ulitabiriwa nakatika wewe Tanzania lazima isimame. Yapo mengi mabaya yanasemwa juu yako ila nina amini mbele ya alie kuleta duniani na alie kuchaguwa ni sawa na wanajilisha upepo.
Tunakushkuru sana mh Rais nikikutakia Merry Chrismas and happy new year. Asante sana Mh Rais
Haijanyooka bado! Chochea tanuru la moto mara saba zaidi kama alivyofanya mfalme Nebukadneza wa Babiloni wakati ule akihangaika na wale vijana watukutu kutoka Uyahudi ya kale.Hakika yametimia Hongera Mzee Magufuli nchi umeinyoosha bila kujali uraia wa MTU kuwa huyu Chadema Yule CCM Na yule pale CUF.Mbwembwe za Wana CCM kwisha kabisa CCM mbele Kwa mbele Kimyaaaa kina mama hakuna miluzi wa vigeregere wote Ukame mifukoni.Nadhani nchi itanyooka sasa hata Mashati ya kijani hayavaliki hayanunuliki mifuko imekauka heshima ya serikali kuwa ndio mshika Hela imerudi.Viva Magufuli.
Mbona mie navaa mkuu!Hakika yametimia Hongera Mzee Magufuli nchi umeinyoosha bila kujali uraia wa MTU kuwa huyu Chadema Yule CCM Na yule pale CUF.Mbwembwe za Wana CCM kwisha kabisa CCM mbele Kwa mbele Kimyaaaa kina mama hakuna miluzi wa vigeregere wote Ukame mifukoni.Nadhani nchi itanyooka sasa hata Mashati ya kijani hayavaliki hayanunuliki mifuko imekauka heshima ya serikali kuwa ndio mshika Hela imerudi.Viva Magufuli.
Hakika yametimia Hongera Mzee Magufuli nchi umeinyoosha bila kujali uraia wa MTU kuwa huyu Chadema Yule CCM Na yule pale CUF.Mbwembwe za Wana CCM kwisha kabisa CCM mbele Kwa mbele Kimyaaaa kina mama hakuna miluzi wa vigeregere wote Ukame mifukoni.Nadhani nchi itanyooka sasa hata Mashati ya kijani hayavaliki hayanunuliki mifuko imekauka heshima ya serikali kuwa ndio mshika Hela imerudi.Viva Magufuli.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli , leo mchana amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kukutana na hali ya kumsikitisha.
Rais amesikitishwa na kuhuzunishwa na hali ya huduma kwa wagonjwa hususan wanaolala chini. Pia amekasirishwa na hali ya kutokujali wala kushughulikia vifaa vya kufanyia kazi ambapo amekuta mashine muhimu za uchunguzi wa magonjwa kama vile MRI na CT-SCAN zikiwa hazifanyi kazi kwa muda wa miezi miwili sasa, ilihali mashine kama hizo katika Hospitali za binafsi zinafanya kazi na wagonjwa wanaelekezwa kwenda kutafuta huduma huko?. Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amesema na kutoa maelekezo yafuatayo :
Rais amevunja Bodi ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambayo ilishamaliza muda wake na amemteua Prof. Lawrence Mseru , kukaimu nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa Muhimbili kuanzia kesho tarehe 10 Novemba, 2015.
Dkt. Hussein L. Kidanto ambaye ndiye anayekaimu hivi sasa, amehamishiwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambako atapangiwa kazi nyingine.
Balozi Sefue pia amesema, Rais ametoa wiki moja na kwa vyovyote si zaidi ya wiki mbili kwa uongozi mpya wa Muhimbili kuhakikisha kuwa mashine zote za uchunguzi wa magonjwa ambazo hazifanyi kazi zinafanya kazi na kuhudumia wananchi kama ipasavyo.
Tayari Wizara ya Fedha imetoa shilingi bilioni 3 kwa ajili ya kazi hiyo na kulipa madeni ya ukarabati wa mashine za uchunguzi wa magonjwa nchini.
Hata hivyo Katibu Mkuu Kiongozi amesema kuanzia sasa hospitali zote nchini zinatakiwa kutenga fedha kutoka kwenye mapato yao wenyewe na kuhakikisha mashine na vifaa vyote vya kazi vinafanya kazi wakati wote (Regular Maintenance).
Balozi Sefue pia metumia nafasi hii kuwaagiza watendaji na viongozi wote katika sehemu za kazi kuhakikisha wananchi wanahudumiwa ipasavyo na kazi za umma zinatekelezwa ipasavyo.
Hakutakuwa na huruma kwa watumishi wa Umma wasiojali wananchi na mahitaji yao. Amesisitiza Balozi Sefue.
Mwisho
Imetolewa na;
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu ? Dar es Salaam.
9 Novemba, 2015
Na alihusika kwenye uchapaji viboko wa yule mdadaHiyo handryting utakuwa unatokea kanda maalumu Tarime/Rorya