Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Kwa kweli jpm anajitahidi Sana kutoa speech zilizoja hisia Kali na mifano na mikakati mpaka raha. Ukimsikiliza huchoki na akukaribia kumaliza unatamani aendelee. Jpm ni zaidi ya maraisi wote duniani. JK alikuwa akitoa speech nasinzia kabisa zilikuwa hazina mvuto kabisaaa
Unafiki mtupu, speech nzuri zaidi na za Mbowe
 
Tuwe wakweli na tusifuate ukabila kuwa fulani ni Msuk......mwenzangu, JPM hawezi kumzidi JK kwa speech hata kwa sekunde na yupo mbali sana. Nina uhakika pamoja na 2 years of my experience nitamzidi mbali nikipambanishwa nae
Mazwazwa ya CCM achanayo mkuu
 
Kwa kweli jpm anajitahidi Sana kutoa speech zilizoja hisia Kali na mifano na mikakati mpaka raha. Ukimsikiliza huchoki na akukaribia kumaliza unatamani aendelee. Jpm ni zaidi ya maraisi wote duniani. JK alikuwa akitoa speech nasinzia kabisa zilikuwa hazina mvuto kabisaaa
Wasukuma jamani!!!!
 
tutampima kwa matokeo kama vifaa vya kutosha mahospitalini, madawa ya kutosha, wafanyakazi wa kutosha hasa elimu na afya, vitendea kazi vya kutosha mashuleni, wanafunzi wenye sifa elimu ya juu wote wanapata mikopo, barabara nzuri, maji salama, umeme wa uhakika, uchumi wa mtu mmoja mmoja umekua n.k hatutampima kwa ziara maofisini
Mkuu uliona mbali sana....
 
wewe jamaa akili zako ni ndogo
Watu hawakufikiria ipasavyo. Mimi binafsi sikuweza kutoa hitimisho juu ya haya yaliyokuwa yanasemwa ila nilimpa muda fulani ili kumpima kama kweli anaweza kumudu majukumu ya kuisogeza Nchi sehemu moja kwenda sehemu nyingine...
 
Rais tuliyemuwaza kwa muda mrefu sasa yuko nasi.
Tumpe ushirikiano tu.
Kimsingi kafanya mengi tuliyoyaona kama changamoto kwetu.
Ufisadi umekuwa msamiati tu,
Elimu bure,
Nidhamu kazini,
Huduma nyingi za kijamii zimekuwa bora!
Hakika Kwa sasa Rais yupo, serikali ipo,
Wananchi nasi tupo.
We are proud of having JPM.
 
Na mwaka huu kitawashuka tu,mtajibeba nakwambia maana si kwa kuchanganyikiwa huko!
 
Utawala huu lazima tuzame shimoni [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Viongozi wenye maono makubwa LA kuitaka taifa lijitegemee kwa wananchi wake kufanya kazi za kizalendo na kusimamia taifa linaondokana na unyang'anyi wa rasirimali za taifa kwa manufaa ya watu wengi ambao ni maskini na kujenga uchumi imara.

RAIA namba moja Hayati JK Nyerere na JP Magufuli nyie ni wazalendo wa kiwango cha juu. Nyerere alikuwa mzalendo aliyeisababishia taifa hili kuheshimika kitaifa; kikanda na kimataifa. Rais aliyechukia rushwa na kuishi maisha halisi ya kitanzania.

Aliwachukulia shida za watanzania na kuziwekea mikakati. Katika utekelezaji wa kazi za kizalendo kwa taifa hili wasaliti walikuwepo. Hii inatokana na ukweli kwamba kila palipo na jema shetani huingiza fitina.

Lakini Hayati JK Nyerere alisimama na imani ya kizalendo na kusimamia rasilimali za taifa hili ziwanufaishe watanzania.

Hakika raia namba moja hayati JK Nyerere utabakia mzalendo wa kiwango cha juu katika historia ya taifa hili.

Hivi karibuni taifa la Tanzania limepata raia namba moja mhe. Daktari JP Magufuli. Kiongozi anayeishi kwa maneno yake. Anayechukizwa na rushwa; anayependa watanzania wasinyanyaswe katika taifa lao; anayefanya jitihada mbalimbali kulinda rasilimali za taifa hili kwa manufaa ya Tanzania.

Anamaono ya kulifikisha taifa hili katika uchumi wa kati kwa kutumia vyema rasilimali za taifa hili na kuhamasisha watanzania tufanye kazi kwelikweli tujenge taifa letu.

Anachukizwa na ufisadi; uzembe na ulevi wa madaraka. Anatamani watu wote tuitumikie taifa hili kwa maendeleo ya vizazi vya sasa na badae. Katika jitihada anazochukua kumejitokeza wasaliti pia.

Kama ilivyokuwa kwa Nyerere watu wenye maslahi binafsi wanamuona kama kiongozi anayetishia maslahi yao hivyo kutengeza porojo kila kukicha.

Mhe. Dr. JP Magufuli hakika wewe ni mzalendo unayefuata nyayo za Hayati Nyerere. Piga kazi taifa hili na wananchi wako viva Magufuli.
 
Mh Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania kweli wewe ndio Rais wa pekee ktk taifa hili haujawahi kutokea hata baada ya kuondaka baba wa taifa Mwl Nyerere. Kiukweli hutembei kwa nguvu zako tu? Ila hata hayati baba wa taifa kule aliko anakumbuka maneno yake ya mwisho "Nawaombea watanzania"

Ndugu zangu huyu Rais hatokuwepo huyu rais ni wa maajabu. Dr Magufuli hakika amekuwa rais wa mfano ktk taifa na duniani hakuna kiongoz amewahi kuwa na speed ya maendeleo na mipango ina speed kama yahuyu Rais. Unaweza kusema alijuwa njia before hajawa Rais ama alikuwa na pla B kabla yakuwa Rais. Ninani atasimam aseme sinaguswa na speed ya maendeleo ya huyu Rais?
Ninani atasemamm sijaguswa na matendo mema yahuyu kiongozi?
Kwakweli huyu Rais amejitoa kwa dam kuikomboa tanzania semeni yote mwaweza sema ila Mh Rais anania njema kulikomboa taifa hili.

Ilifika mahali watu waliona wao ndio wenye haki yakuishi wengine wakiwa hawana hiyo haki. mh rais amegawa haki hiyo kwa wote.
Mungu anapenda watu wanatoa haki kama huyu Rais kwa hakika ni rais wakarne na amini vizazi kwa vizazi watamsoma alikiwepo Rais Dr Magufuli.. Nakupenda sana Mh Rais nakuombea ufanye mengi zaid ya haya na nina iman wewe ni wakipekee sana.
 
kuna muda unaweza kuumia ukitafakari kwa kina baadhi ya kauli za viongozi ukilinganisha na matendo yao.
 
Mh Rais ametengeneza kitu hatujakielewa ila at last umefika wakati kila mtanzania ni usalama wa taifa. Majambaz wote na majizi ya rasilimali yote hayana pakujificha..
Explain more mkuu.
 
Back
Top Bottom