Na Emmanuel J. Shilatu
1. Watoto wetu wasingesoma elimu ya msingi mpaka sekondari bure na wangeendelea kutumikishwa majumbani, kuwa Watoto wa mitaani kama ilivyo awali. Juhudi za Rais Magufuli zimemkomboa Mzazi/mlezi na mzigo wa ada na michango na ameokoa kizazi na vizazi dhidi ya mapambano ya adui ujinga.
2. Nidhamu na uwajibikaji kwa Watumishi wa umma usingeimarika na dharau, matusi, uvivu, rushwa na ufisadi ungeendelea kutamalaki kama awali. Juhudi za Rais Magufuli zimeirejesha Tanzania kwenye nidhamu ya kazi.
3. Suala la ujenzi wa flyovers lingeendelea kubaki kwenye makaratasi tofauti na hali ilivyo sasa ambapo Watanzania tunashuhudia flyover ya Tazara. Hizi ni juhudi za kiuwezeshi zinazofanywa na Rais Magufuli katika kupambana na foleni nchini.
4. Ujenzi wa reli ya kisasa kwa standard gauge inayotumia umeme usingekuwepo. Bila ya juhudi hii ya Rais Magufuli, Watanzania tungeendelea kutumia muda mrefu njiani, gharama za usafiri na usafirishaji zingeendelea kuwa juu.
5. Watanzania tungemiliki lini tena ndege za kisasa aina ya dreamliner 787-8 ama ndege ya Bombadier kwani shirika letu la ndege lilishakuwa juu ya mawe. Juhudi za Rais Magufuli zimemrudisha "Twiga" (ndege) angani na leo hii anaonekana mpaka nje ya mipaka ya Tanzania huku akitengeneza faida ya Tsh. Bilioni 4.5
6. Watuhumiwa wakubwa 'Mapapa' ya rushwa na ufisadi wasingepandishwa Mahakamani. Uonefu, upigaji na matabaka ndani ya jamii yangeendelea kukua. Juhudi za Rais Magufuli zimesaidia Leo hii Tanzania imepanda kwa nafasi 13 katika mwaka 2016 na 2017 huku ikishika nafasi ya pili (2) kwa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki. Kama haitoshi zaidi Tsh. Bilioni 127.9 zimeokolewa na Serikali kwa kuzuia vitendo vya rushwa na mali zenye thamani ya Tsh. Bilioni 4.5 zimezuiliwa na nyumba 6 zimetaifishwa. Hayo ni matunda ya juhudi ya Serikali ya Rais Magufuli.
7. Suala la Serikali kuhamia Dodoma lingeendelea kubaki kwenye makaratasi tangu yalipoasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere mwaka 1973. Juhudi za Rais Magufuli zimefanya leo hii Serikali kuhamia Dodoma na Dar es Salaam kubaki jiji la biashara.
8. Mradi wa ujenzi wa umeme wa Stiegler's Gorge ambao utazalisha megawatz zaidi ya 2100 ulioasisiwa na Mwalimu Nyerere mwaka 1981 ungeendelea kubaki kwenye makabati. Juhudi hizi za Rais Magufuli zitapelekea Watanzania tuwe na umeme wa uhakika na hata bei ya umeme itapungua na gharama za maisha kuendelea kupungua zaidi.
9. Nidhamu na heshima ya Serikali imeimarika sana. Juhudi za utawala wa Rais Magufuli zimepelekea uimarikaji wa ulinzi, amani na usalama nchini; heshima ya viongozi wa Serikali imeimarika; na suala la migomo na maandamano limebaki historia.
10. Mapambano dhidi ya uhuru wa kiuchumi tungechelewa sana kuyaanza. Kwa juhudi, ujasiri, nidhamu na uzalendo wa Rais Magufuli leo hii Watanzania tunaendelea vyema na mapambano ya kujenga uchumi wetu kwani makusanyo ya mapato yetu kwa mwezi yamefikia Tsh. Trilioni 1.3 , ukuaji wa uchumi wetu umefikia asilimia 7.2 , reli inajengwa, bomba la mafuta linajengwa, ndege zinanunuliwa na madini yetu yamedhibitiwa vilivyo ili rasilimali hizi zimnufaishe Mtanzania pekee.
*Shilatu E.J*
Sent using Jamii Forums mobile app
1. Watoto wetu wasingesoma elimu ya msingi mpaka sekondari bure na wangeendelea kutumikishwa majumbani, kuwa Watoto wa mitaani kama ilivyo awali. Juhudi za Rais Magufuli zimemkomboa Mzazi/mlezi na mzigo wa ada na michango na ameokoa kizazi na vizazi dhidi ya mapambano ya adui ujinga.
2. Nidhamu na uwajibikaji kwa Watumishi wa umma usingeimarika na dharau, matusi, uvivu, rushwa na ufisadi ungeendelea kutamalaki kama awali. Juhudi za Rais Magufuli zimeirejesha Tanzania kwenye nidhamu ya kazi.
3. Suala la ujenzi wa flyovers lingeendelea kubaki kwenye makaratasi tofauti na hali ilivyo sasa ambapo Watanzania tunashuhudia flyover ya Tazara. Hizi ni juhudi za kiuwezeshi zinazofanywa na Rais Magufuli katika kupambana na foleni nchini.
4. Ujenzi wa reli ya kisasa kwa standard gauge inayotumia umeme usingekuwepo. Bila ya juhudi hii ya Rais Magufuli, Watanzania tungeendelea kutumia muda mrefu njiani, gharama za usafiri na usafirishaji zingeendelea kuwa juu.
5. Watanzania tungemiliki lini tena ndege za kisasa aina ya dreamliner 787-8 ama ndege ya Bombadier kwani shirika letu la ndege lilishakuwa juu ya mawe. Juhudi za Rais Magufuli zimemrudisha "Twiga" (ndege) angani na leo hii anaonekana mpaka nje ya mipaka ya Tanzania huku akitengeneza faida ya Tsh. Bilioni 4.5
6. Watuhumiwa wakubwa 'Mapapa' ya rushwa na ufisadi wasingepandishwa Mahakamani. Uonefu, upigaji na matabaka ndani ya jamii yangeendelea kukua. Juhudi za Rais Magufuli zimesaidia Leo hii Tanzania imepanda kwa nafasi 13 katika mwaka 2016 na 2017 huku ikishika nafasi ya pili (2) kwa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki. Kama haitoshi zaidi Tsh. Bilioni 127.9 zimeokolewa na Serikali kwa kuzuia vitendo vya rushwa na mali zenye thamani ya Tsh. Bilioni 4.5 zimezuiliwa na nyumba 6 zimetaifishwa. Hayo ni matunda ya juhudi ya Serikali ya Rais Magufuli.
7. Suala la Serikali kuhamia Dodoma lingeendelea kubaki kwenye makaratasi tangu yalipoasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere mwaka 1973. Juhudi za Rais Magufuli zimefanya leo hii Serikali kuhamia Dodoma na Dar es Salaam kubaki jiji la biashara.
8. Mradi wa ujenzi wa umeme wa Stiegler's Gorge ambao utazalisha megawatz zaidi ya 2100 ulioasisiwa na Mwalimu Nyerere mwaka 1981 ungeendelea kubaki kwenye makabati. Juhudi hizi za Rais Magufuli zitapelekea Watanzania tuwe na umeme wa uhakika na hata bei ya umeme itapungua na gharama za maisha kuendelea kupungua zaidi.
9. Nidhamu na heshima ya Serikali imeimarika sana. Juhudi za utawala wa Rais Magufuli zimepelekea uimarikaji wa ulinzi, amani na usalama nchini; heshima ya viongozi wa Serikali imeimarika; na suala la migomo na maandamano limebaki historia.
10. Mapambano dhidi ya uhuru wa kiuchumi tungechelewa sana kuyaanza. Kwa juhudi, ujasiri, nidhamu na uzalendo wa Rais Magufuli leo hii Watanzania tunaendelea vyema na mapambano ya kujenga uchumi wetu kwani makusanyo ya mapato yetu kwa mwezi yamefikia Tsh. Trilioni 1.3 , ukuaji wa uchumi wetu umefikia asilimia 7.2 , reli inajengwa, bomba la mafuta linajengwa, ndege zinanunuliwa na madini yetu yamedhibitiwa vilivyo ili rasilimali hizi zimnufaishe Mtanzania pekee.
*Shilatu E.J*
Sent using Jamii Forums mobile app