Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Law number one. Never outshine your Master, always make him feel brilliant and superior than he is.
Hilo hata mtoto mdogo anajua kwahiyo wewe unafanya inavyokupasa kumsifu
Umemaliza kazi yooote! Uzi unaweza kufungwa.

Kama watu wamejiita kuwa waliokotwa jalalani, then why not you Elly?
 
Ndugu watanzania wenzangu, salaam.

Imekuwa kama sehemu ya utamaduni kutokumpa mtu sifa zake njema angali hai bali ni rahisi sana kuona yale mabaya au tusiyoyapenda. Mtu huyohuyo anapokufa ndio sasa utasikia mema yake lukuki mengine hata hukuwahi kuyasikia.

Awali ya yote, napenda kukumbusha japo ninajua tunafahamu ya kuwa Magufuli kwa mama yake yeye ni mtoto, yaani John, yeye ni mume wa Janet, baba wa akina Jesca na ndugu zake, mjomba, baba mkubwa/mdogo, rafiki na mtanzania kama nilivyo mimi na wewe.

Tukumbuke kuwa Magufuli hajawa malaika ba kamwe hatakuwa malaika. Magufuli sio mtakatifu na wala hajaingia kwenye mchakato wa kuwa mwenye heri. John is just a man.

Ninatambua kuwa unapokuwa Rais kuna sifa za ziada zinazotarajiwa kwako lakini pamoja nazo bado hazikuondolei ule uasili wa ubinadamu wako.

Rais John Magufuli anao udhaifu wake kama mwanadamu lakini tupime zaidi uimara wake hasa kwenye taasisi hiyo ya urais na pale tunapoona madhaifu, basi tumkosoe kistaarabu.

Rais Magufuli amejitahidi mno na nadhani amewashinda marais wote waliomtangulia kwa kigezo cha mambo aliyoyafanya kimaendeleo katika kipindi hiki cha miaka mitano.

Kwanza amekuza sana makusanyo ya Kodi. Udhaifu katika makusanyo ya kodi kilikuwa kilio cha wengi hasa wapinzani. Ameongeza kasi kwenye ujenzi wa barabara na madaraja. Serikali ya awamu ya tano imenunua meli na vivuko vipya.

Kwenye Kilimo mikopo inatolewa kwa wakulima, anapambana na watu wa Kati wanaowadhulumu wakulima. Njaa sasa imekuwa historia nchini kwetu. Nidhamu imeimarika sana serikalini hivyo kuboresha huduma. Rushwa imedhibitiwa kwa kiwango kizuri.

Tumeongeza ndege na kufufua shirika la ndege. Mgawo wa umeme umebaki kuwa historia. Umeme umesambazwa maeneo mbalimbali ya nchi mpaka vijijini. Maji yameendelea kusambazwa.

Elimu bila malipo ambayo imeongeza udahili. Shule zote kongwe zimekarabatiwa kwa kiwango kizuri na kurejesha kiwango chake cha awali. Shule za umma sasa zinaanza kurudi kwenye kumi bora. Zahanati na hospitali nyingi zimejengwa, bajetibya dawa imeongezwa sana. Sera yetu ya mambo ya nje imehuishwa na kuwa inaingalia Tanzania kwanza.

Mambo ni mengi na takwimu zipo. Ukiangalia vizuri utaona Rais Magufuli amegusa kila nyanja na hii ndio maana tumeingia kwenye uchumi wa kati. Ukiwa na jicho la kuangalia baya ni lipi kwenye kila jema basi huwezi kuona kazi kubwa iliyofanyika.

Rai yangu ni kuwa Rais Magufuli ni mchapakazi na mtu mkweli. Tumuunge Mkono kwa kufanya kazi kwa bidii. Kwa wapinzani, ninawashauri wajikite zaidi kwenye kuojenga nchi badala ya kuikwamisha. Mambo yakiharibika, haharibikiwi Magufuli peke yake, tunaharibikiwa watanzania.

Magufuli amekuwa Rais wa mfano, tumuunge mkono kwa vitendo na kuhakikisha tunampa kura tarehe 28.10.2020 ili atupaishe zaidi kama nchi.

Mungu mbariki Rais Magufuli
Mungu ubariki uchaguzi mkuu wa tarehe 28.10.2020
Mungu ibariki Tanzania

Amani Msumari
Tanga
IMG-20200907-WA0016.jpg
 
Watumishi wa umma wamenufaika sana na utawala wa Rais Magufuli, 306,917 wamepandishwa vyeo na madaraja na kulipwa madai yao mbalimbali ya jumla ya shilingi bilioni 472.6.

Kati ya hizo shilingi bilioni 114.5 yalikuwa ni madeni ya mishahara na shilingi bilioni 358.1 yalikuwa ni madeni yasiyokuwa ya mishahara kama vile uhamisho.

Watumishi wengi wa umma ni mashahidi jinsi walivyopandishwa vyeo na madaraja wakati wa utawala wa Rais Magufuli baada ya kugota katika madaraja hayo kwa miaka mingi. Kupandisha watumishi 306,917 kati ya watumishi takriban 500,000 wa umma haijawahi kutokea.

Viva Rais Magufuli, viva watumishi wa umma. Kura zetu tunampa Mhe Rais Magufuli. (Source za takwimu ni hotuba ya Rais Magufuli akifunga Bunge tarehe 16 Juni 2020).

Tunakwenda na Rais Magufuli.
 
Ndugu yangu, hawa ni watumishi wa aina zote na kada zote. Watumishi wenyewe wanajua walivyonufaika na wana jambo lao la kufanya tarehe 28 Okt. Ni kumpa kura zote JPM
 
Wacha kudanganya watu wewe, hao watumishi ni watumishi wa Ikulu?

Kila mahali malalamiko yamejaa na after all watu wanapandishwa madaraja kuanzia baada ya miaka 7 hadi 8 kinyume na utaratibu wa kila ya miaka 3 alivyokuwa akifanya JK.

Usitake kwafanya watu wajinga
 
Hyo miaka mingi ambayo hawakupandishwa madaraja ni mingapi?

Hajapandisha mishahara kwa miaka mitano je ni mingi au michache?

Ingalikua ni Lisu unadhani asingeweza kupandisha mishahara na madaraja?

Pesa za kuwalipa alitoa mfukoni kwake?
 
Bora umetaka kujua ni wa idara zipi . Mkuu ni wa idara zote.

Sekta ya afya ni miongoni mwa watumishi waliogota miaka mingi bila kipandishwa vyeo kabla ya utawala wa Rais Magufuli, ila kwa sasa wengi sana wamepandishwa madaraja. Fanya utafiti japo kwa wachache utapata ukweli huu.

Bahati nzuri wao watumishi wanajua ukweli huu na watatoa appreciation yao kwa kumpa kura nyingi Mhe Rais Magufuli.
 
Watumishi wa umma wamenufaika sana na utawala wa Rais Magufuli, 306,917 wamepandishwa vyeo na madaraja na kulipwa madai yao mbalimbali ya jumla ya shilingi bilioni 472.6. Kati ya hizo shilingi bilioni 114.5 yalikuwa ni madeni ya mishahara na shilingi bilioni 358.1 yalikuwa ni madeni yasiyokuwa ya mishahara kama vile uhamisho. Watumishi wengi wa umma ni mashahidi jinsi walivyopandishwa vyeo na madaraja wakati wa utawala wa Rais Magufuli baada ya kugota katika madaraja hayo kwa miaka mingi. Kupandisha watumishi 306,917 kati ya watumishi takriban 500,000 wa umma haijawahi kutokea. Viva Rais Magufuli, viva watumishi wa umma. Kura zetu tunampa Mhe Rais Magufuli. (Source za takwimu ni hotuba ya Rais Magufuli akifunga Bunge tarehe 16 Juni 2020). Tunakwenda na Rais Magufuli.
Humo serekalini kuna watumishi kibao bado hawajabadilishiwa vyeo na mishahara baada ya kuongeza elimu. Miaka inakatika tu. Awamu hii ni ya kidhulumaji.
 
Jamaa anachekesha sana,usitake kuamsha hasira za watu tukaanza kutafutwa na wasiojulikana.

Malalamiko ya wafanyakazi ni kunyimwa nyongeza ya mshahara ya kila mwaka ambayo awamu hii ya tano kwa miaka yote mitano ongezeko limefanyika Mara moja tu 2017 na mwaka huu 2020 kwa kupunguza kodi.

Kupandishwa madaraja hili limecheleweshwa kwa kisingizio Cha uhakiki wa wafanyakazi hewa na wenye veti feki jambo ambalo kiujumla limeumiza watu hususani wale ambao walikuwa wamefikia umri wa kustafu.

Jingine ni malimbikizo ya mishahara hapa ukweli serikali imejitahidi kulipa na wanaendelea kulipa hapa tuwape pongezi,
 
Yote haya ni matokeo ya utawala bora wa mheshimiwa Rais.

Ndio maana Tundu Lisu anachukiwa sana na wananchi.

Kila anapoenda anazomewa na wananchi ambao shida yao kubwa ni madaraja, Barabara, elimu ya bure, afya, drimliner yaani ndege, vitambulisho vya mmachinga na kadhalika.

Hakika huu utawala hauna mfano wake.
Mitano tena jamani.
 
Back
Top Bottom