Mafia: Watu 7 wafariki dunia baada ya kula nyama ya Kasa

Mafia: Watu 7 wafariki dunia baada ya kula nyama ya Kasa

Mpaka muda huu watu sita wamefariki dunia baada ya kula nyama ya kasa kisiwani Mafia wakiwemo watoto wawili ambao ni ndugu huku baba yao na mama yao wakiwa wapo hospitali hapa Mafia wamelazwa.

Taarifa zinakuja sababu bado huduma inaendelea watu ni wengi waliokula taarifa inakuja ishazikawa miili ya watu watatu, bado watatu.

=======
Watu saba wamefariki dunia baada ya kula samaki aina ya kasa anayesadikiwa kuwa na sumu katika Kijiji cha Bweni na Kanga Wilayani Mafia Mkoani Pwani.

Watu hao wanatoka kwenye kaya nne tofauti kijijini humo na walifariki kwa nyakati tofauti Machi 12 mwaka huu mara baada ya kula samaki hao.

Kaimu Kamanda wa Polisi, Mkoa wa kipolisi Rufiji, Canute Msacky amesema kati ya watu hao saba waliopoteza maisha ni watoto sita.

Kamanda Msacky ametaja majina ya waliokufa ni Mohamed Makame umri miezi Saba, Minza Hatibu (miezi kumi), Ally Seleman (miezi nane), Ramadhan Karimu (miezi nane), Abdala Nyikombo (miaka 4), Makame Nyikombo (miaka tisa) pamoja na Salima Mjohi (miaka 28).

"Ni kweli tukio lipo ni watoto sita wa kuanzia miezi saba na mtu mzima mmoja ndio wamefariki, na taarifa za awali ni kwamba wamekufa baada ya kula samaki aina ya kasa anayesadikika kuwa na sumu, na hawa watu walipoteza maisha kwa nyakati tofauti tofauti kuanzia usiku majira ya saa Moja Machi 12 "amesema Kamanda Msacky.

Ameongeza kuwa miili ya marehemu wote imeshafanyiwa uchunguzi wa kitabibu katika hospitali ya Wilaya ya Mafia na tayari wameshakabidhiwa ndugu kwa taratibu za mazishi. Kuhusu chanzo cha tukio hilo, amesisitiza kuwa bado kinaendelea kuchunguzwa.

Aidha Kamanda Msacky ameeleza tayari watuhumiwa watatu wanashikiliwa na Jeshi hilo kwa mahojiano zaidi.
"Tumefanikiwa kuwakamata watu watatu kwa mahojiano zaidi ambao nao wamelazwa hospitali ya wilaya hapa Mafia baada ya kuzidiwa wakiwa chini ya uangalizi wa Jeshi hilo kwani nao walikula nyama ya samaki huyo" ameongeza

Kufuatia tukio hilo Jeshi la Polisi Mafia limetoa wito kwa wavuvi kuacha tabia ya kuvua samaki aina hiyo ya kasa ambao ni nyara za Serikali.

Kamanda Msacky ameshauri wafuate kanuni na sheria za uvuvi wa samaki hao kwani Polisi wataendelea kuchukua hatua kali kwa wavuvi wasiofuata taratibu na sheria za nchi.

Pia soma > Kwanini watu wanakula Kasa licha ya wengine kufa kwa sumu waliyonayo?
kasa mtamu sana ananyama tam, ukimla kwa wale wapenzi wa lager, rangi ya mende ukishushia na safari 3 kubwa bariiidi, utajihisi goliati
 
Huo ni ulafi
Watu hawajatosheka na nyama zote hizi duniani
Weamua kuhamia kula Kobe[emoji119]
Matatizo mengine ya kujitafutia.

Mpaka sasa kuna aina 24000 za samaki baharini 99% wanaliwa.
Ila inawezekana katika ukanda wako uliobahatika kuwaona ni kama aina 100 tu.
Na tumefanikiwa kuifikia bahari na kuijua 5% tu,kwahiyo bado tuko na tunaendelea na tafiti za vyakula vya habarini.
 
Ulishawahi mla?
Uliumwa?
Au zamani hakuwa na sumu sasa ana Sumu?
Kuna aina at least mbili za kasa, wale wanaoliwa na wenye sumu.

Inataka mtaalamu aweze kutafautisha baina ya hizi species na ndiyo maana wavuvi wengi vijana wanaingia mkenge na kujivulia kasa yo yote na kumla.

Halafu kasa nimewahi kusikia kuwa ni migratory inawezekana wale wanaoliwa wamekuwa wachache kwa hivyo wenye sumu ndiyo wamekuwa wengi wa ukanda huu wetu.

Mimi nakumbuka nyama ya kasa ilikuwa inauzwa pale marikiti Zanzibar bila ya kificho na kwa kipindi kile tulikuwa hatusikii watu kufa kwa kula nyama ya kasa. Pia nakumbuka alikuweko mama mmoja kutoka Madagascar alikuwa akipenda sana nyama ya kasa, akiiona pale inauzwa alikuwa akinunua nyingi tu na wala hakuwahi kupata madhara kwa kipindi kile.
 
Hivi Zanzibar ina visiwa vingapi maana nilikua nafikir ni unguja na pemba.
Hiyo mafia ipo wapi??
Somo kuu la jiografia:

Zanzibar ina visiwa vikuu viwili, Unguja na Pemba, lakini pia vimezungukwa na visiwa vingi vidogo vidogo (ndiyo maana inaitwa Zanzibar archipelago) mfano: Tumbatu, Kisiwa Panza, Kojani, Fundo, Misali, Changuu, Chumbe, Mnemba na Latham.
 
naendelaea vyema ila mwili hauna nguvu

Mkuu unachangamsha genge au ni kweli na wewe ulimla huyo kasa? Najua wewe ni mvuvi huko mafia na mzoefu wa kuwajua samaki ,na kuna misemo sana tunaitumia mashuleni kama "umenilisha kasa yaani umenipa sumu desa bovu" inakuwaje bado elimu ya hawa kasa hamuijui? Kila siku kesi za vifo vitokanavyo na ulaji wa kasa vinatokea lakini nashangaa hadi nyinyi wazoefu hamjifunzi,nini tatizo?
 
Mkuu unachangamsha genge au ni kweli na wewe ulimla huyo kasa? Najua wewe ni mvuvi huko mafia na mzoefu wa kuwajua samaki ,na kuna misemo sana tunaitumia mashuleni kama "umenilisha kasa yaani umenipa sumu desa bovu" inakuwaje bado elimu ya hawa kasa hamuijui? Kila siku kesi za vifo vitokanavyo na ulaji wa kasa vinatokea lakini nashangaa hadi nyinyi wazoefu hamjifunzi,nini tatizo?
kasa hana sumu ila ikitokea ikawa amekula mwani na bahati mbaya akavuliwa ma watu ndio hutokea haya sababu mwani ndio wenye sumu mimi nilimkuta tayari ashapikwa nikala kiasi mwingine nikaweka nimalizie asubuh kumbe dah we acha tu
 
kasa hana sumu ila ikitokea ikawa amekula mwani na bahati mbaya akavuliwa ma watu ndio hutokea haya sababu mwani ndio wenye sumu mimi nilimkuta tayari ashapikwa nikala kiasi mwingine nikaweka nimalizie asubuh kumbe dah we acha tu

Mkuu inabidi uwape elimu wavuvi wenzako kwamba wakivua kasa before kumla watafute wataalam wapime kama ana sumu au lah.
 
Mkuu inabidi uwape elimu wavuvi wenzako kwamba wakivua kasa before kumla watafute wataalam wapime kama ana sumu au lah.
upimaji wake wakati wa kuikata nyama pale inapokuwa mbichi huwa inawasha mikononi sasa sijajua wale jamaa walomvua ila maajabu waliokamtawa sio waliovua baharini
 
kasa hana sumu ila ikitokea ikawa amekula mwani na bahati mbaya akavuliwa ma watu ndio hutokea haya sababu mwani ndio wenye sumu mimi nilimkuta tayari ashapikwa nikala kiasi mwingine nikaweka nimalizie asubuh kumbe dah we acha tu
Nacheka kama mazuri 🤭🤭 kimsingi Tu stay away na huyo Kobe maji , hakuna haja ya kubet na uhai huu wenye Mashaka
 
View attachment 2549206
[emoji115]Bunju anakuwa kama chura fulani na ana miba kibao



View attachment 2549203
[emoji115]mkunga kama nyoka wapo wanatishia kinoma Kuna wengine ni jamii ya nyoka wa bahari ukileta Tamaa ukafiria mkunga ukamla ndo kwisha habari yako...Kuna wavuvi wanagonjwa na wale nyoka bahari wakifiria ni mkunga
Shukrani sana mkuu, hao wadudu wote hawana mvuto asee, uyo mwenye miba mimba nshamwona beach akiwa amekufa mara kadhaa
 
Ukisikia watu wanaosifia utamu wa nyama ya kasa, aisee bora wafe tuu 😂
 
Nimekupata, asante sana!

Hiyo wilaya imejitenga sana maana mara ya mwisho kusikia neno Mafia duu, miaka kadhaa imepita.
Kabila gani wanapatikana huko!?
Hiki ni kisiwa kwahiyo wenyeji wengi ni walowezi kutoka rufiji ambao ni wandengereko. Pia wapo watu kutoka mtwara na kilwa
 
Back
Top Bottom