Mafundi umeme mnisaidie kuhusu hiki kitu

Mafundi umeme mnisaidie kuhusu hiki kitu

View attachment 2292606

Hiko kifaa ni saparet meter maswali yangu ni haya,,

1/ Nikinunua, kimoja kinatumika, kwa, mpangaji mmoja tu?
2/ Kama ni kwa, mpangaji mmoja tu je ile buku ya kila mwezi nikitaka kununua, umeme nikiweka itakatwa?
3/ Vipi kuhusu meter kuu kama wenzangu hawajaingiza umeme na tuko giza mimi wangu nao ukaisha je nitaweza kuendelea kujihudumia umeme bila meter kuu kuwa na umeme?
4/Hii huduma je TANESCO wameipitisha? (inakubalika)

Karibuni mnipe elimu.

NB: Uzi usiunganishwe sehemu nahitaji majibu ya fasta nipate chaguo langu kabla ya maamuzi.

ASANTE!
Nimekupata vizuri kabisa,Ni ivi izo separate mita za kusoma matumizi ya mteja inatakiwa mita kuu ya Tanesco iwe na Umeme,izo separate mita hua zinafungwa sana kwenye majengo makubwa ama hata yale ya kawaida isipokuwa mita kubwa isiwe ya kutumia Luku,Kwetu Tanzania wenye majengo makubwa wao wanatumia zile mita za bili yaani mita zao zinasomwa mwezi hadi mwezi,sasa izo separate mita zilivyo ni zilezile tu kama zile za Tanesco kwani hao agent ndio wanaowauzia tanesco mita,sasa wewe ukishakuwa na mita kubwa unaongea nao kisha wanakufungia halafu kuna ki-softwear wanakupata kinakuwa kinaunganishwa na mita unit zinazosoma mita kubwa,utaamua wewe wakuunge utumie kwenye desktop,laptop ama simu kwaiyo mteja akitaka umeme kwenye mita yake unaingiza mita yake kisha kinakupatia tokeni ndio unayoingiza na mteja hapo atapata umeme na pia ukiisha umeme kwake utakata ila kwa wapangaji wengine wataendelea kupata,ni nzuri sana izo mita ama kama utataka pia kutumia kwa mita ndogo za luku ya tanesco itabidi mwenye nyumba awe anaingiza umeme mwingi kisha anawauzia wapangaji wake umeme,na pia gharama za kununua umeme ni zile zile wanazouza tanesco,
Kuna sehemu nilipo zimefungwa izo mita kama utataka uje uzione karibu
 
Separate meter ina rekodi units zako ulizotumia, hivyo ili kuwe na usawa kila mtu awe na ya kwake na vifaa vyake vyote viwe vime connectiwa kwenye meter hiyo

Umeme wako chanzo chake ni mita kuu, hivyo kuhusu buku ya kila mwezi mtajichanga kadri mlivyo kwenye hiyo nyumba kwa idadi
gharama ya buku inakatwa mara moja tu kweye mita kuu
 
Cha zamani kinahesabu unit kama bill ya maji ilivyo! Continually! Hakistop kama last months uliishia unit 75 next kinaendelea 76,77,78.... Hivyo inakulazimu uwe na daftali kurekodi ilipoishia ili utoe unit za nyuma kupata idadi ya unit alizo tumia ndipo umuombe pesa kulingana na matumizi yake.

Kifupi ni kama ilivyo mita ya maji! Changamoto ni pale mpangaji atakubishia kwamba umekosea ndipo mtapasuana
Je, cha zamani kinaweza kujipimia?
 
Nimekupata vizuri kabisa,Ni ivi izo separate mita za kusoma matumizi ya mteja inatakiwa mita kuu ya Tanesco iwe na Umeme,izo separate mita hua zinafungwa sana kwenye majengo makubwa ama hata yale ya kawaida isipokuwa mita kubwa isiwe ya kutumia Luku,Kwetu Tanzania wenye majengo makubwa wao wanatumia zile mita za bili yaani mita zao zinasomwa mwezi hadi mwezi,sasa izo separate mita zilivyo ni zilezile tu kama zile za Tanesco kwani hao agent ndio wanaowauzia tanesco mita,sasa wewe ukishakuwa na mita kubwa unaongea nao kisha wanakufungia halafu kuna ki-softwear wanakupata kinakuwa kinaunganishwa na mita unit zinazosoma mita kubwa,utaamua wewe wakuunge utumie kwenye desktop,laptop ama simu kwaiyo mteja akitaka umeme kwenye mita yake unaingiza mita yake kisha kinakupatia tokeni ndio unayoingiza na mteja hapo atapata umeme na pia ukiisha umeme kwake utakata ila kwa wapangaji wengine wataendelea kupata,ni nzuri sana izo mita ama kama utataka pia kutumia kwa mita ndogo za luku ya tanesco itabidi mwenye nyumba awe anaingiza umeme mwingi kisha anawauzia wapangaji wake umeme,na pia gharama za kununua umeme ni zile zile wanazouza tanesco,
Kuna sehemu nilipo zimefungwa izo mita kama utataka uje uzione karibu
well done
 
Suluhu ya kudumu kwa hizi nyumba za kupanga ni TANESCO kubadilika na kufunga kila chumba meter yake inayojitegemea kama wanavyofanya wenzao wa kenya


Kenya hawaujui ujamaa hao, ni mabepari, 🤣🤣
 
View attachment 2292825View attachment 2292827
Kenya huwa wanatumia ki hvyo hapo kila chumba kinajitegemea huna hela unalala giza peke yako, si umeme tu bali hata maji kila mtu analipa bill kivyake kama huna hela Koki yako haitoi maji maana mambo ya kuchangishana hayapo


Mambo ya Kenya bwana!!!, nasikia hata wapangaji au majirani kuazimana kalamu, kuombana chumvi, Majani ya chai nk ni mwiko.🤣🤣
 
Majibu ni kama ifuatavyo!
Hiyo separate mita inafanya kazi kwa kutegemea MAIN METER YA TANESCO!

Hivyo cha kwanza kabisa lazima MAIN mita iwe na umeme ili hiko kisepareti meter kifanye kazi!

Hivyo makato yote ya kodi za serikali (Jengo, ewura, rea, na 18VAT) yanakatwa kupitia manunuzi ya MAIN METER YA TANESCO na si vinginevyo!

Je, kinafanyaje kazi?

Ni kwamba unaponunua hicho kiseparete meter dukani au kiwandani unapewa link ya kuingia na kuingiza mita namba ya MAIN METER!

Ambapo ukishaingiza mita namba inakutolea SUB TOKEN za umeme ambazo utalazimika kwenda kuziingiza kwenye separate meter ili umeme uwake!
Hivyo mfano!

MAIN METER YA TANESCO INA UNIT 100Kwh!

Ukitengeneza tokeni ya umeme wa unit 20 inamaana utapunguza kule kwenye 100 zitakuwa zimebaki 80 kwa wapangaji wenzio! Wewe utachukua zako 20kwh!

Zikiisha itabidi MAIN METER ITOP UP KWANZA NDIPO UPATE WAKO!

Mfano kama MAIN METER Wakigoma kununua umeme ikawa na 0Kwh! Unaweza kununua umeme kwenye MAIN METER Halafu ukatengeneza token yenye thamani ya pesa ya umeme wako HIVYO UKAUKOMBA WOTE kutoka kwenye MAIN UKAJA KWAKO kwenye hiyo SEPARATE METER!

Cha kuzingatiwa ni kwamba lazima MITA IWE NA UMEME Ndipo separate meter ifanye kazi, bila hivyo ni kazi bure! Natumai kwa haya machache nimeeleweka

Kama kuna mtu anhitaji kazi za kiufundi UMEME na UJENZI au kwa maelezo zaidi unaweza kupiga simu 0711756341 au tembelea ukurasa wetu Instagram @samico_tanzania PIA TUNATOA USHAURI Bei ni nafuu sana!

Appreciate
 
daaaah kwahyo makelele yapo palepale


i walisema kama umenunua unt 28 wakat unahamisha lazima zibaki na we utoke na unt 25 hivi sasa shida hizo ulizoacha watajichanga kuongezea mainmeter iendelee kuhema au watasubr mpk zikate daah!
[emoji3][emoji3][emoji119][emoji119] " daaah kwahyo makelele yapo palepale"

Nimecheka sana mkuu...

Sent from my SM-A135F using JamiiForums mobile app
 
Cha zamani kinahesabu unit kama bill ya maji ilivyo! Continually! Hakistop kama last months uliishia unit 75 next kinaendelea 76,77,78.... Hivyo inakulazimu uwe na daftali kurekodi ilipoishia ili utoe unit za nyuma kupata idadi ya unit alizo tumia ndipo umuombe pesa kulingana na matumizi yake.

Kifupi ni kama ilivyo mita ya maji! Changamoto ni pale mpangaji atakubishia kwamba umekosea ndipo mtapasuana
Daah

Sent from my SM-A135F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom