Mafundi wengi Bongo wanashindwa kufanya Overhaul ya Engine ya 1ZZ

Mafundi wengi Bongo wanashindwa kufanya Overhaul ya Engine ya 1ZZ

Mbaya zaidi ni bei ya hiyo injini ya 1ZZ. 'Mswaki' ni 2mil, complete ni 2.3mil.

Niliwahi kufanya overhaul ya hiyo injini mwaka 2018. Ilisumbua baada ya hapo ila ilikuja kubainika mafundi wa awali waliruka jino moja la timing chain. Ilipofika 2022 ikaanza tena kuchoma oil. Kila baada ya wiki 2-3 unaongeza lita 1.

Nikafanya overhaul tena (ingawa fundi alishauri tuchukue 'mswaki', pesa ikawa na mipango mingine mikubwa na muhimu zaidi) iligharimu around laki 5 (parts na ufundi). Baada ya hapo kukawa na leakage ya oil. Kila asbhi unakuta oil imechuruzika chini. Ikarekebishwa tena, ikatulia. Hivi karibuni nimeanza tena kuona matone ya oil chini.

Bado ninasukuma nayo siku kabla sijavuta chombo kingine.
Nikupe ngapi uongezeee
 
Mimi ninachojua na hata Manufacturer ame recommended Engine ya 1ZZ haiwezi fanyiwa Overhaul kutokana na muundo wake ulivyo maana kuna part itahitaji ubadili unit nzima ambayo ni heri ukanunue injini nzima uweke, na ndio maan gari kama Allion na nyingine zenye injini ya 1zz sitaki kabisa kumiliki
 
Aisee!! Ila hiyo bei niliyopewa ilikuwa ni Julai mwaka jana (2022). Hiyo overhaul nilifanya Agosti mwanzoni. Simu ilipigwa kwa muuzaji, alivyotamka bei nikahisi kama ninaibiwa hivi. [emoji38][emoji38]
1nz yenyewe mswaki wanaanzia 1.6M kwa sasa, wakati nyuma kidogo tu hapo mswaki wa 1nz ulikuwa laki 9 hadi 8, ila ndani ya muda mfupi tu bei imepanda hadi 1.6M. Na 1zz pia imepanda hvyo hvyo, maana 1zz kipindi cha nyuma ilikuwa 1.6M mswaki na complete ilikuwa 2.2M hadi 2.6M.

Ukitaka kuthibisha hilo ulizia bei ilala utaleta mrejesho hapa.
 
Mimi ninachojua na hata Manufacturer ame recommended Engine ya 1ZZ haiwezi fanyiwa Overhaul kutokana na muundo wake ulivyo maana kuna part itahitaji ubadili unit nzima ambayo ni heri ukanunue injini nzima uweke, na ndio maan gari kama Allion na nyingine zenye injini ya 1zz sitaki kabisa kumiliki
Ungetoa na mifano mkuu ungeeleweka vzr zaidi, watu wanafanya 1sz itakuwaje ishindikane 1zz?
 
Ungetoa na mifano mkuu ungeeleweka vzr zaidi, watu wanafanya 1sz itakuwaje ishindikane 1zz?
Sio mtaalamu sana wa kuelezea Mkuu ila unapofanya Overhaul ya hii injini haihitaji ubabaishaji kwakuwa itahitaji ubadilishe vitu vingi vipya ikiwemo timing chain na tensioner yake, o-ring, gasket, muundo wa pistons na rings zake ambazo zipo complicated in sizes nk ambavyo Cost yake inaweza kuikalibia gharama ya kununua injini tu nyingine na bado isifanye kazi kwa ufanisi, ubwiaji wa mafuta kwa wingi, leaks za oil mara kwa mara na performance kupungua na mwishowe utagombana na fundi mno kwa maana haitotulia kama awali,
 
Back
Top Bottom