Magari gani ya kununua nyakati hizi kwa kijana?

Mi huwa nashangaa eti mtu hutaki kununua gari kama ist kwasababu zipo nyingi mtaani...sasa we una angalia watu wana nini mtaani au una angalia interest yako na mfuko wako?...
Shida inaweza isiwe kwenye wingi wa Ist , ila ndio gari zinaongoza kwa kuibiwa spare. Hakuna kitu kinauma kama unaamka asubihi unakuta watu wameondoka hadi na bampa, halafu unaenda mnadani unanunua vifaaa kama hivyo huku ukijua navyo vimeibiwa kwa mwenzio.

Gari za kijerumani ni nadra sana kusikia zimeibiwa vitu
 
Rafiki yangu aliamka asubuhi akakuta ameachiwa fuvu la gari. Halafu gari ya mkopo na 3rd party insurance alizimia. Saiv mtu akisema kaibiwa gari utasikia alivyokuwepo hayakuwepo haya mambo.
Mjerumani mzuri sema gharama sasa.

Kuna mmama wa kichaga anakwambia watu wanasema vits hazinywi mafuta na gari nyingine zinakunywa sana mafuta unataka zinywe mtori au supu[emoji1][emoji1]
 

Hii ndo shida ya IST

Naskiki kesi za kuibiwa spare za IST na kuibiwa magari zinaongezeka. Niliambiwa pia unakuta muda mwingine funguo za IST zinaingiliana

Mimi natafuta gari la kimkakati kama kijana mwenye malengo ya maisha ya mbeleni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…