Magari ya viongozi wa Serikali na afya za wananchi wa Tanzania kipi muhimu?


Vyote muhimu nhif ina Mipango mizuri sana kwenye afya ni wananchi wanakaza fuvu tu
 
Acheni roho mbaya na NHIF, lazima tukubali kuwa Mfuko huu umefanya kazi kubwa sana kuna marefu ya wagonjwa wako huko hospitalini na matibabu yao ni ya maisha yote na NHIF inalipa.

Leo kuboresha usajili wa toto ndio Mfuko umekuwa mbaya kiasi cha kuwafanya Watanzania wote wajiite maskini?

Watu wanachangia michango ya mambo yasiyo ya msingi mpaka hala milioni, watu wanakunywa pombe kila siku lakini kutumia elfu 26 kwa mwezi ili mzazi na mtoto apate bima inakuwa shida.

Lazima Watanzania ifike mahali tubishane kwa hoja na sio hizi hoja sizizo kuwa na mashiko.
 
Nguvu hii ya uchochezi ungetumia kuandika umuhimu wa bima ya afya kwa wananchi ingekuwa jambo la msingi ila cheki umeandika chuki dhidi ya viongozi
 
Unadiliki vp kusema haya wakat ma elfu ya wananchi tunasaidiwa na nhif ktk afya. Michango yetu ndio inatusaidia
 
Tupewe nini tena na nhif wakati kwa kiasi kdg tu kama mchango wangu nikiumwa naweza kulazwa zaidi ya siku 30 hili hamlioni! Kazi kukosoa tu
 
Unaijua V eite wewe, bora mfe tu ila ccm iendelee kuagiza luxury LC's
 
Nguvu hii ya uchochezi ungetumia kuandika umuhimu wa bima ya afya kwa wananchi ingekuwa jambo la msingi ila cheki umeandika chuki dhidi ya viongozi
Nimeuliza swali, waheshimiwa wanalipia kiasi gani kwenye bima? Na je standard hiyo inatumika kwa mwananchi wa kawaida?
 
Niliwahi kuuliza hivi ni hekima ipi ilitumika kuamua kufanya viongozi kugharamiwa maisha ya kifahari pamoja na kulipwa mishahara mikubwa?
 
Thread za namna hii zimetamalaki siku hizi jf, dawa imeanza kuingia

Tunakitu watanzania tujtahidi tutajikomboa

Na hizi movement zingekuwa zinaenda Hadi nje ya mitandao ingekuwa vizuri kwel

Tunayopitia watanzania yanaumiza sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnasahau kuwa kupitia bima ya nhif mtu anaweza kufanyiwa hadi upasuaji lkn hii hamuongelei kwa nn mnazi kwa kiasi kdg hicho ndio kinafanya mtu apate huduma hiyo lahasha bali umoja wetu wa kutoa michango ndio inawasaidia wagonjwa walio wengi ndio mana tuhimizane kutoa michango
 
Mzazi usizae na kukwepa jukumu la kuhudumia familia yako.
Tanzania ni nchi ya kibepari
 
Tupewe nini tena na nhif wakati kwa kiasi kdg tu kama mchango wangu nikiumwa naweza kulazwa zaidi ya siku 30 hili hamlioni! Kazi kukosoa tu
Bila shaka unacomment hapa ukiwa ndani ya v8,ndio wale wale ptuuu[emoji706][emoji706]
 
Kweli Bima ya Afya ni janga ila Mama Samia hajui ni watoto wangapi walikua wananufaika na Toto Card aliyoifuta kama wanamdangaanya haina impact waache kuiba kura 2025 waone kama CCM watakanyaga Dodoma.
 
Tunashukuru kwa maoni. Bima ya Afya ni suala la kila mmoja, hivyo tuendelee kuhimizana kila mmoja ajiunge kugharimia matibabu. Kwa upande wake, NHIF imeandaa vifurushi ambavyo mwananchi anaweza kujiunga kwa kutegemea umri wake, idadi ya wanufaika katika familia na mahitaji ya huduma kuanzia TZS 192,000 kwa mwaka. Aidha imeanzisha mpango wa kulipa kwa awamu (DUNDULIZA) ambapo mwanachama anaweza kulipa kidogo, kidogo kuanzia TZS 526 kwa siku. Hivyo tunawakaribisha wote kujiunga.
Vilevile, tunashukuru kwa fursa hii katika jukwaa hili kwani watu wengi zaidi wanaelimika na kujua huduma za Mfuko. Tunapokea kupokea maoni kufanya maboresho kwa huduma endelevu. Karibuni sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…