Magufuli aliweza vipi kwa Miaka 5?

Magufuli aliweza vipi kwa Miaka 5?

Umejibu ujinga kwenye kipindi ambacho tunategemea Watu wenye akili kubwa kutupatia majibu ya kutupa faraja!!!
Majibu gani ambayo wewe unataka ili upate faraja kutoka kwa nani? Kama tu kiongozi ambaye mnalipa mshahara na posho anawajibu kwamba asiye taka Kodi aende Burundi mlifanya nini ?

Alafu mimi nimesema kweli ambao naona mnapotosha Kama raisi JPM haja pumzika Chato basi sema usingizi wake wa milele amelala akiwa wapi?

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kwani saivi inapokopwa wazi wazi ndo riba zinapungua? Kwani ushasikia maden ya UK and etc rais wa nchi akiyasema waziwazi kua katoka kwenye ziara za kukopakopa uko? Shame on us yani we unafurahia kiongozi wako wa nchi akiweka wazi kua katoka kukopa uko ndo ujisikie proud ?
Hakuna nchi isiyokopa, hata UK inakopa. Shida ni kudanganya umma kuwa sisi ni matajiri huku unaenda kukopa kisiri tena mikopo ya kibiashara yenye riba kubwa. Serikali ya Jiwe ilikuwa imejaa uongo na udanganyifu mwingi. Ilifanya brainwashing kubwa watu wakaamini tunasonga mbele kumbe tulikuwa tumekwama.
 
Miaka 5 ya kwanza alichukua kwa matajiri na wenye kipato cha kati. Kama angeendelea huenda alikuwa na plan B iwapo matajiri wote wangegeuka mashetani ila ndo hivyo haikuwa.
 
Kinacho ni uma mimi pamoja na tozo hizo hakuna miradi mipya ya kielezo....na ht walioachiwa inaenda mwendo wa kinyonga anaeumwa mdondo...
Dar ilikua ukikatiza unakuta huku Mibarabara inajengwa, huku wanafunga taa barabara za mitaaani, huku mi flyover watu wanachakarika, huku masoko huku hospitali, huku Dawasco wanavuta mabomba...
Asubuhi unapishana na Jaffo na watu wake wa Tamisemi wanaenda kukagua miradi, ukitatiza mbele unakutana na mkutano wa Lukuvi or Bashite wanatatua migogoro ya ardhi...
Ukifungulia TV unakutana na Waziri wa Maji ameliamsha huko mkoani, or waziri wa Nishati yupo Rusumo kwenye Bwawa la Umeme kukagua maendeleo...
Ndalichako na shule zake za Mfano..
Huku Bi Ummy anahangaika na vituo vyake vya Afya
Huku Mpango anapokea gawiwo...
kule Biteko anafungua soko la madini...
kule wakuu wa mkoa wanacheki km tofali za ujenzi ndo zenyewe or wanapokea madawati...
Ukiingia youtube ni video tu za miradi, kuanzia TRC, Tanrods, MeliTV mpaka Tamisemi.
huku JPM anapokea mindege
ili mradi kazi kazi, purukushani za kazi kila sehemu.
Nlikua kila week lazima nipitie website ya Tanraods kujishtua moyo na miradi mipya mipyaaa...now ht ule mradi wa mwendokasi wa kule kwetu g'mboto uliotanganzwa Aug 2020 mpaka leo hakuna jipya.
Now with all that money za mitozo na mikopo inchi bado imelala doro.
What happened to us?
I real miss the old days..
Kumbe unapenda wazee wa show off, kujionesha na misifa mingi!
.
Kufanya kitu kidogo tu lazima uite wanahabari na vyombo vyao uonekane kwa media!
 
Uyasemayo yana ukweli ni haki ya kila mtu kulipa kodi lakini serekali imewawezesha kwa kiwango gani wananchi wake katika maisha yao kuweza kulipa kodi au watu walipe kodi bila kujua uwezo wao wakati kwa sasa kilo 1 ya unga sembe inakaribia 2000.
Ukitaka kuangalia gharama za maisha kwa bei za vitu jaribu kuhusisha angalau awamu 3,,
Mfano ngano kwa jk ilkuwa tshs--, kwa magufuli ilikuwa--- na sasa iko ---! Ukimaliza Fanya mahesabu ujue wapi pameonekana kupanda zaidi!
 
Magufuli aliweza vipi kuendesha nchi kwa miaka 5 bila ya kuwaminya Wananchi kwa kodi na tozo?

Na msiniambie alikopa kwani mpaka Samia anaingia debt to GDP ratio Tanzania ilikuwa one of the lowest Duniani na ndani ya mwaka mmoja deni limeongezeka kwa > 50% sasa aliweza vipi kulipa Mishahara, kujenga Miundo mbinu kama Barabara, Reli, Bandari, Airports, kununua ndege na kufufua shirika la Airtcl, kujenga na kuweka Meli karibia kila Ziwa kubwa Tanzania, kujenga Madaraja kama mto Wami hapo hapo kujenga Dodoma kama Mji Mkuu?

Nijibuni aliweza vipi ? Magufuli was a genius, sasa hivi vilio kila mahali na ndio mwanzo tu, …
Tuliambiwa Magufuli hakukopa maana alikosana na Mabeberu.Siku zote Idiots wakiachwa nafasi watawachagulia viongozi na mwisho wa siku nchi inakuwa inaongozwa kipumbavu.
 
Ila sisi watanzania ni watu tunaongea tusiyoyajua. Hivi wewe wkt wafanyabiashara wanalalamika vyuma vimekaza uliona sawa kwasababu hakukuwa na tozo inayokubana wewe? Wkt akaunti za watu zinafungwa na ela kuchukuliwa wewe uliona sawa kwasababu hazikuwa za kwako? Sasahv tunashirikiana wote kuleta maendeleo........lipa tozo kwa maendeleo ya nchi yako acha porojo......
 
Magufuli aliweza vipi kuendesha nchi kwa miaka 5 bila ya kuwaminya Wananchi kwa kodi na tozo?

Na msiniambie alikopa kwani mpaka Samia anaingia debt to GDP ratio Tanzania ilikuwa one of the lowest Duniani na ndani ya mwaka mmoja deni limeongezeka kwa > 50% sasa aliweza vipi kulipa Mishahara, kujenga Miundo mbinu kama Barabara, Reli, Bandari, Airports, kununua ndege na kufufua shirika la Airtcl, kujenga na kuweka Meli karibia kila Ziwa kubwa Tanzania, kujenga Madaraja kama mto Wami hapo hapo kujenga Dodoma kama Mji Mkuu?

Nijibuni aliweza vipi ? Magufuli was a genius, sasa hivi vilio kila mahali na ndio mwanzo tu, …


Unavyosema hajawaminya wananchi kwani wafanyabiashara sio wananchi kaulize wenye maduka ya pesa, waliochukuliwa pesa bank bila sababu na nenda kariakoo kaulize
 
Alichukua Kwa Wafanyabiashra wakubwa kinguvu.
Masikini wakawa wanacheka cheka.

Sasa zamu yenu mnapiga YOWE!

Hii inaitwa Mkuki Kwa nguruwe Kwa binadamu mchungu.

Kila mtu akatwe Kodi, iwe Masikini iwe tajiri.

Kuwa Masikini sio exceptional ya kutokulipa Kodi.
Tozo ziendelee mpaka fikra za Kupenda maisha ya bure ziishe.
Kupenda kufanyiwa fanyiwa!

Muhimu; Serikali itumie Kodi vizuri, mafisadi na wezi wa Mali za umma watungiwe sheria Kali.
Sio mitozo iwe mingi alafu kuna watu wanaitafuna kimagendo. Hiyo haiko Sawa.
Ukiwa umelewa usiwe unacomment. Brainless goat.
 
Badala ya kuweka tozo ,aliwapora wafanya biashara pesa zao na kuziingiza serikalini kwa kuvunja haki za watu hao
 
Kama ulikuwa una majibu yako tayari sio kwanini umeileta humu! Ukweli lilikopa sana na kukwapua hela za matajiri kinguvu hadi wengine tuliambiwa wametekwa kumbe mtekaji ni kibaraka wake Bashite, hakuwa na maajabu yoyote.
 
"Serikali corrupt,haikusanyi Kodi,inabaki kufukuzana na masikini",Mwl. Nyerere
 
To frozen the economy of our country because of hate late behavior was a stupidity kind of life Jiwe made in our country,this person was an evil person and shall be an evilo person always.
Who is not an evil in the CCM government?Kikwete became rich after coming out of power,where did he get all those wealth,if not plundering and looting of our national resources!!
 
jabalii

misingi lazima ijikite kwenye sheria usimamizi mzuri ulio usema lazima ujengwe na sheria kibaya ni kwamba yeye ndio alikuwa mvunja sheria number moja.
Na haya yanayoendelea ni mwendelezo wa yale aliyo yaanzisha tofauti ni kwamba saivi wanatumia ujanja yeye alitumia ubabe ..
Porojo tu unapiga
 
Hukusikia Wahujumu uchumi wakina Sethi na wenzake?

Wakati Watanzania karibu wote ni wahujumu uchumi kulingana na sheria za Kodi.
Au kisa Sisi ni masikini???
Wewe Seth unamjua?huyo katapeli mpaka serikali ya Kenya,aliletwa hapa na wahuni ajifanye kuwa anainunua IPTL kumbe muhuni tu.
 
Back
Top Bottom