Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, F. Mramba. Amteua Dkt. Mwinuka kukaimu

Mimi sitaki kumlaumu ila nina amini kidon yetu imempa ubuyu wenye ladha ya kumtumbuwa. Shime Magu.
 
Vipi kuhusu board nzima?

Huu mchakato wa kuomba kuongeza bill za umeme inaonekana ulikuwa "haramu" tangu mwanzo na EWURA waliendelea na mchakato haramu.
 
Mwinuka????? Dah haya bwana... Ila katoa fadhila kwa Wahaya ili kesho abwate weee na mambo mengine yaende!! Mwinuka ni mchanga mno na hajawahi kuwa mbunifu hata kidogo.! Hapana!! Mwinuka Tito hapana!!!!!
Huenda unamjua vzr hebu lete habari zake..... maana mtukufu ilimradi uwe unaitwa Dr au Eng
 
Jamaa kama Zirail vile, kila kukicha anapeleka kilio kwa familia kadhaa, dah! Noma sana.
 
Watumishi wa serikali hamisha vitu vyenu toka ofisini. Israil atatokea wakati wowote!
 
Duh...... Yaani siku ya kwanza tu ya mwaka 2017, tayari Magu kauanza kwa kutumbua mtu!

Basi tutarajie mwaka huu utakuwa wa utumbuaji wa kutisha zaidi .......
Kiufupi Mzee hataki masihara....na ni kiashiria kwamba hajachoka kujenga nidhani na uwajibikaji serikalini.

Haijarishi ni siku gani ukiboronga mzee hakuachi. Unakula sikukuu vibaya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…