Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, F. Mramba. Amteua Dkt. Mwinuka kukaimu

Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, F. Mramba. Amteua Dkt. Mwinuka kukaimu

Duh huu mwaka utakua na mitumbuo mingi sana.. Ngoja tusubiri ila hii ya Tanesco ilikua kwenye target tangu wakati wa kampeni basi tu jamaa hakuinamisha kichwa kupisha kimbunga, hatimae kimemzoa.
 
Nadhani jpm hakuiangalia ile mechi ya simba na yanga. Lazima angemtumbua refarii
 
Mkuu, kheri ya Mwaka Mpya.

Mramba hajaonewa ila naona huna facts kuhusu khasa kilichomtoa hapo Tanesco.

Inawezekana likawa ni suala la EWURA au pia tangu mwezi may alipoagizwa asitishe mazungumzo na Symbion kuhusu PPA (power production agreement) na serikali.

Lakini pia inawezekana na gharama kubwa ambazo Tanesco inalipa kwa IPP independent power producers.

Utakumbuka hotuba ya bajeti ya profesa Muhongo bungeni mwezi Juni alisema kwamba serikali ipo kwenye mchakato wa kuondokana na IPPs kwa kuwa sasa tuna hata gesi kutoka Mtwara.

Mramba ameagizwa na serikali kuangalia mikataba ambayo Tanesco ilisaini na hawa IPPs na khasa ule wa Symbion ambao wanalipwa kiasi cha dola bilioni 5 kwa mwezi kwa kuwauzia umeme Tanesco kwenye mikoa ya Dar, Arusha na Dodoma.

Jambo baya kabisa kuhusu huu mkataba wa PPA ni kwamba iwe umeme upo au hakuna lazima Tanesco wawalipe Symbion kasi hicho cha fedha kila mwezi.

Na tatizo Mramba alisaini mkataba huo harakaharaka kabla ya raisi JPM kuingia, hivyo unategemea nini hapo?

Unapopewa maagizo na serikali khasa yenye kuhusu maslahi ya taifa (siyo maslahi binafsi) unatakiwa kuwa mwangalifu.
Huoni kama serikali ya awamu ya 5 kuna tatizo la flow of information kati ya watendaji wa serikali hasa wakurugenzi wa mashirika na mawaziri/Raisi

Angalia hii mifano
1.Waziri wa afya vs NIMR -Hakuna Zika/Zika ipo
2.Waziri wa afya vs MSD-Akiba ya dawa chanjo imeisha/Hakuna upungufu wa dawa/chanjo
3.Raisi vs Hazina/BOT-TRA wamefungua FDA ili wachukue interest/kufungua FDA sio tatizo
4.RCs vs Raisi-Machinga/wachimbaji wadogo waondolewe/Wamachinga na wachimbaji wadogo wasiondolewe

Iko migongano mingi ikiwemo ya kuongeza na kushusha GPA kwa admission vyuoni,Kuteuliwa kwa boss NSSF akatenguliwa baada ya siku moja.Huu ni mwaka wa 2 watendaji wa Raisi bado wanatofautiana.Kuna kipindi naona uamuzi wa JK kuwapeleka watendaji wake semina elekezi Ngurdoto ulikuwa uamuzi mzuri sana
 
Rais Magufuli na Buhari watajwa kama marais walioangusha matumaini ya wananchi::

Wakitoa tathimini ya mwaka 2016 kuelekea mwaka 2017, Redio ya idhaa ya kiswahili ya ujerumani DW wamewataja marais John Pombe Magufuli wa Tanzania na Buhari wa Nigeria kuwa ni marais walioangusha matumaini ya wananchi wao hasa vijana na ikizingatiwa kuwa ni marais walioingia kwa mbwembwe nyingi na kutoa matumaini mapya ya mafanikio.

Wakimzungumzia Rais Magufuli, walisema wanachi wengi walitegemea hali zao za uchumi zikiimarika lakini badala yake wamejikuta katika hali ngumu zaidi, huku vijana wakikata tamaa pale wanapowaona watangulizi wao wakitopea katika lindi la umasikini wa kutupwa.

Wakizungumzia demokrasia walisema rais ameshindwa kabisa katika nyanja hii, anaiendesha nchi kwa mkono wa chuma, matumizi mabaya ya madaraka na upendeleo, kuwakamata na kuwatia ndani wakosoaji wake, kusitisha taasisi mbalimbali, uhuru wa habari na kujieleza umebinywa na kuwafanya hata viongozi wa dini waliokua wanakosoa pale wanapoona hapaendi sawa ku kaa kimya.

Upande wa elimu, vijana wengi waliokua wanashangilia leo wanalia kwa kuwanyima mikopo watoto wa masikini, ajira hakuna, walimu wanayimwa stahiki zao, ufukuzaji usiofuata sheria na maslai duni. Elimu inayotolewa bure imeshindwa kukidhi matarajio.

Uchumi walisema hali ni mbaya sana, masoko yamedorora, biashara zinafungwa,ajira zinapunguzwa hali ambayo haitii matumaini kwa vijana, kodi kubwa ambazo haziendani na kipato halisi cha biashara.

Walimalizia kwa kusema hali ya matumaini kwa wanachi wa Tanzania imefifia sana na ukataji wa matumaini ni mkubwa sana hivyo inahitajika mabadiliko chanya ya kiuchumi na kisera.

Chanzo : DW
 
Angemwacha mpaka tarehe 2, kumwambia "Heri ya mwaka mpya" utaona kama unamchora!
 
Kwa ufupi anachokifanya huyu Juma Poor Manager ni kuharibu na kuboronga tuh

Let say he is right kachukizwa na maamuz ya kupandishwa kwa bei ya umeme ni obvious kwamba Mramba hawez kufanya hivyo bila baraka ya bodi..sasa anaiachaje bodi na kumuondoa mramba.

Pili shirika kama Tanesco linahitaji taaluma ya uendeshaji na siyo kuchukua intruder ambae hata hafaham na hana taaluma hiyo na wala hana experience ya uendeshaji

Mfano Dr Idrisa Rashid ilimchukua muda sana hadi kuja kumaster challanges na kusonga mbele

Wapo watu hapo Tanesco wenye uwezo mkubwa tuh kama Engineer Nazir Kachwamba...Engineer Deklan Mhaiki...na kadhalika ambao may be wangeweza kumrith mramba

Sasa kukimbilia kufanya maamuz ya mlipuko kama hayo ni kutuaminisha kwamba kuna watu wake alishawaandaa na anawatafutia kazi...ma kututhibitishia kwamba katika awamu hii wachaga na waislam ni watu wa kuogopwa kama ukoma
Nimekuelewa sana,hizo ni athari za maamuzi mlipuko
 
Safi sanaa.. Wanadai mapato ya nchi yameongezeka mara dufu alafu wanapandisha bei ya umeme? Nilishangaa sana! Wachukue hizo pesa za kodi wachanganye na gesi iliyotoka mtwara kukava hizo cost za umeme sio kila kitu kuweka mzigo kwa wananchi.. Kama vipi atumbue na huyo wa Ewura aliyehalalisha upandishaji wa bei ya umeme.
 
Mkuu leo ni siku ya tatu ikiwa inanyesha, na leo imenyesha kuanzia saa 7 mchana mpaka saa 11 jioni. Na tena ni mvua ya nguvu.
Daah,hongereni mkuu..
Cc pande za dom hiz,tumezimic saana mvuu..hatuioni
 
Hilo ni kosa? Huyu mtu na maaskofu wake watahukumiwa!
Alicho Fanya JP ndivyo inavyo takiwa walio baki wajihadhari na maamuzi ya kilevi hawajamuelewa magufuli, anacho taka magufuli wewe kama kiongozi kila dakika ubuni mbinu za kumpa faraja mtu wa chini sio kumzidishia mzigo.
 
Back
Top Bottom