Uchaguzi 2020 Magufuli kakosea sana kampeni zake mkoani Mara. Je, haujui mkoa ule au hapendi watu wake?

Uchaguzi 2020 Magufuli kakosea sana kampeni zake mkoani Mara. Je, haujui mkoa ule au hapendi watu wake?

Hajajua kuwa Mara ni mkoa wa kina Mura. Hawarembi. Watamfurumusha huko. Alipoingia Mara aliona kibao kimeandikwa "KARIBU MKOA WA MARA"???
Muwe mnatoka na kutembelea mikoa mingine walau mara moja moja. Sasa mkoa gani ambao ukienda hauna vibao vya karibu?!?
 
Salaam wana JF...

Jana tarehe 04.09.2020 nikiwa nimetulia sehemu nilibahatika kufungulia TBC1 na kukuta kampeni za Dkt. Magufuli akiwa mkoani Mara.

Muda wa alasiri, alikuwa Bunda, badae akapita na kusimama Kiabakari, ni eneo la mnada wilayani Butiama.
Leo najua atakuwa na mkutano Musoma mjini.

Mambo niliyoshangaa kwa Dkt. Magufuli:-

1. Aliwaambia wananchi wa Bunda kwamba hakuwafanyia maendeleo yoyote, kwa sababu wao walichagua upinzani.

-Akawauliza "nyinyi hamjiulizi mko karibu na Ziwa lakini hamna maji?"
-Akawauliza "hamuoni wenzenu Lamadi (mpakani mwa Bunda, jimbo Busega) wana taa za barabarani, nyie hamna?!"
- Akawaambia, hata barabara nimeendeleza zinazowazunguka hapa nikawaruka.

Mwisho akaishia kuwaambia mnichagulie mbunge wa CCM, na madiwani wa CCM.

Nilishangaa hakueleza zaidi atawafanyia nn, ila aliwaahidi kuwa mkinichagulia mbunge wa CCM nitakuja kuwashukuru, na siku hiyo ndio ntakuja na mipango yote kuibadilisha Bunda.

Akawasisitiza wasichague maupinzani tena.

ETI HAWEZI KUACHA MTOTO WAKE, AKAMHUDUMIA WA JIRANI.

Nampa pole Dkt. Magufuli kwa haya na timu yake ya kampeni.

Inaelekea hajui vizuri watu wa Mara (hasa eneo la Bunda).

-Moja, sio watu wa kutishiwa vitu kabisa. Pole Dkt. Magufuli

Kwa hili, Bunda umepoteza.
Wale wamezoea kuishi na upinzani tangu Nyerere akiwa hai.

Unamtishia mwana Bunda (Mwikizu, Msizaki, Mzanaki, Mkurya, n.k) vitu?!!!! Eti ndio akuchague?

UME FAIL....

Hawakuchagui, watasema baki na taa zako za barabarani.

Wale ni kina LadyJaydee hawatishwi na hawapigi magoti.

Sijui huko usukumani labda wanapiga magoti.

- Mbili,
Ni uongo mkubwa kwamba Bunda haina maendeleo kisa kuwa upinzani.

Nikuulize leo upo Musoma mjini, ambayo ipo CCM awamu hii yako ya kwanza;

Mbona Musoma mjini imefubaa kuliko Bunda?, mji umepotea na biashara haziendi mpaka watu wameukimbia?! Mbona huko yupo mbunge wa CCM?

Haya BUTIAMA je?

Mbona siku zote wapo CCM. Tena wanapitaga bila kupingwa. Mbona BUTIAMA imechoka sana.

- BUTIAMA haina maji, lakini ipo CCM.
Mbunge CCM, Madiwani CCM.

- BUTIAMA kampuni yako ya Mayanga imeshindwa kujenga Barabara ya Butiama - Serengeti, na hela walilipwa, Mradi wa kumalizika 2015, mpaka leo umekufa.

Mbunge CCM, Madiwani CCM.

- BUTIAMA haina hospital ya maana, Haina sekondari ya maana, Haina soko la maana.

Mbunge CCM, Madiwani CCM.

ACHA HADAA, HAKUNA CHA CCM.

-HALAFU UNAJIITA KABISA RAIS WA MAENEO YA CCM TU.!!

2. AKIWA KIABAKARI.
Akiwa hapa alisema tatizo kubwa la Jimbo la BUTIAMA, ni ukabila.

Aisee you're very WRONG.

Butiama haina ukabila kabisa.
Ndio maana hata ulivyosema hivyo niliona kila mtu ananyamaza.

Sijui ulimaanishi nini. Ila umedanganywa pakubwa, matatizo ya BUTIAMA ni mengine kabisa.

Nakuhurumia sana.

Halafu mu MSHAURI JPM AACHE KUTISHA WAPIGA KURA kwamba hatawafanyia maendeleo kwa vile wanachagua upinzani.

Ni uongo mkubwa...

Haya ni majimbo ambayo yapo CCM, lakini ni maskini vibaya sana..

1. BUTIAMA
2. BUKOMBE
3. BUSEGA
4. MANYONI
5. MUSOMA VIJIJINI
6. KIBITI
7. RUFIJI
8. MKURANGA
9. MVOMERO
10. UKONGA
11. KAKONKO
12. MAGU
13. IRAMBA
14. MAKETE
15. NEWALA
16. MTAMA
17. KIVUU
18. SUMBAWANGA
19. NZEGA KASKAZINI
20. NZEGA KUSINI
21. SENGEREMA
22. CHATO
23. LONGIDO
24...........

Mwana JF...

Taja MAJIMBO mengine yaliyopo CCM lakini ni maskini vibaya mno...

Comment hapa Chini.....
Mgombea wa aina hii hatufai wa Tanzania, Hayupo kujenga umoja wa watu bali kubomoa miaka yote CCM imekuwa madarakani waseme ni sehemu gani ndani ya hii nchi inakila kitu
 
Mkuu hicho kibao kimeandikwa " Karibu mkoa wa Mara, Be Strong"

Mkuu, nilidhani kimeandikwa "Sasa unaingia Mkoa wa Mara". Neno KARIBU hakuna. Wanaume wale. Ukiingia jiaminishe. Hakuna aliyekukaribisha. Acha kulialia. Hahaha, kumbe Magu hawajui.
 
Salaam wana JF...

Jana tarehe 04.09.2020 nikiwa nimetulia sehemu nilibahatika kufungulia TBC1 na kukuta kampeni za Dkt. Magufuli akiwa mkoani Mara.

Muda wa alasiri, alikuwa Bunda, badae akapita na kusimama Kiabakari, ni eneo la mnada wilayani Butiama.
Leo najua atakuwa na mkutano Musoma mjini.

Mambo niliyoshangaa kwa Dkt. Magufuli:-

1. Aliwaambia wananchi wa Bunda kwamba hakuwafanyia maendeleo yoyote, kwa sababu wao walichagua upinzani.

-Akawauliza "nyinyi hamjiulizi mko karibu na Ziwa lakini hamna maji?"
-Akawauliza "hamuoni wenzenu Lamadi (mpakani mwa Bunda, jimbo Busega) wana taa za barabarani, nyie hamna?!"
- Akawaambia, hata barabara nimeendeleza zinazowazunguka hapa nikawaruka.

Mwisho akaishia kuwaambia mnichagulie mbunge wa CCM, na madiwani wa CCM.

Nilishangaa hakueleza zaidi atawafanyia nn, ila aliwaahidi kuwa mkinichagulia mbunge wa CCM nitakuja kuwashukuru, na siku hiyo ndio ntakuja na mipango yote kuibadilisha Bunda.

Akawasisitiza wasichague maupinzani tena.

ETI HAWEZI KUACHA MTOTO WAKE, AKAMHUDUMIA WA JIRANI.

Nampa pole Dkt. Magufuli kwa haya na timu yake ya kampeni.

Inaelekea hajui vizuri watu wa Mara (hasa eneo la Bunda).

-Moja, sio watu wa kutishiwa vitu kabisa. Pole Dkt. Magufuli

Kwa hili, Bunda umepoteza.
Wale wamezoea kuishi na upinzani tangu Nyerere akiwa hai.

Unamtishia mwana Bunda (Mwikizu, Msizaki, Mzanaki, Mkurya, n.k) vitu?!!!! Eti ndio akuchague?

UME FAIL....

Hawakuchagui, watasema baki na taa zako za barabarani.

Wale ni kina LadyJaydee hawatishwi na hawapigi magoti.

Sijui huko usukumani labda wanapiga magoti.

- Mbili,
Ni uongo mkubwa kwamba Bunda haina maendeleo kisa kuwa upinzani.

Nikuulize leo upo Musoma mjini, ambayo ipo CCM awamu hii yako ya kwanza;

Mbona Musoma mjini imefubaa kuliko Bunda?, mji umepotea na biashara haziendi mpaka watu wameukimbia?! Mbona huko yupo mbunge wa CCM?

Haya BUTIAMA je?

Mbona siku zote wapo CCM. Tena wanapitaga bila kupingwa. Mbona BUTIAMA imechoka sana.

- BUTIAMA haina maji, lakini ipo CCM.
Mbunge CCM, Madiwani CCM.

- BUTIAMA kampuni yako ya Mayanga imeshindwa kujenga Barabara ya Butiama - Serengeti, na hela walilipwa, Mradi wa kumalizika 2015, mpaka leo umekufa.

Mbunge CCM, Madiwani CCM.

- BUTIAMA haina hospital ya maana, Haina sekondari ya maana, Haina soko la maana.

Mbunge CCM, Madiwani CCM.

ACHA HADAA, HAKUNA CHA CCM.

-HALAFU UNAJIITA KABISA RAIS WA MAENEO YA CCM TU.!!

2. AKIWA KIABAKARI.
Akiwa hapa alisema tatizo kubwa la Jimbo la BUTIAMA, ni ukabila.

Aisee you're very WRONG.

Butiama haina ukabila kabisa.
Ndio maana hata ulivyosema hivyo niliona kila mtu ananyamaza.

Sijui ulimaanishi nini. Ila umedanganywa pakubwa, matatizo ya BUTIAMA ni mengine kabisa.

Nakuhurumia sana.

Halafu mu MSHAURI JPM AACHE KUTISHA WAPIGA KURA kwamba hatawafanyia maendeleo kwa vile wanachagua upinzani.

Ni uongo mkubwa...

Haya ni majimbo ambayo yapo CCM, lakini ni maskini vibaya sana..

1. BUTIAMA
2. BUKOMBE
3. BUSEGA
4. MANYONI
5. MUSOMA VIJIJINI
6. KIBITI
7. RUFIJI
8. MKURANGA
9. MVOMERO
10. UKONGA
11. KAKONKO
12. MAGU
13. IRAMBA
14. MAKETE
15. NEWALA
16. MTAMA
17. KIVUU
18. SUMBAWANGA
19. NZEGA KASKAZINI
20. NZEGA KUSINI
21. SENGEREMA
22. CHATO
23. LONGIDO
24...........

Mwana JF...

Taja MAJIMBO mengine yaliyopo CCM lakini ni maskini vibaya mno...

Comment hapa Chini.....
Huu uzi huwezi kuwaona akina bia yangu..wakudadavua .. mgonjwa mtambuka..Mama ntilie wa kawe .. Pascal mayala ..sumve yao..mtashobya ..kipara kipya na USSR ...wanapita juu kwa juu [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Muwe mnatoka na kutembelea mikoa mingine walau mara moja moja. Sasa mkoa gani ambao ukienda hauna vibao vya karibu?!?

Usiseme kinadharia wewe. Umefika Mara? Kibao chao kimeandikwa "SASA UNAINGIA MKOA WA MARA". Neno KARIBU halipo.
 
Mbona karibu Tanzania yote ni masikini sana ingawa CCM wanashikilia sehemu kubwa ya majimbo ya nchi hii!!?
Istoshe watanzania wote ni walipa kodi wanaostahili kupelekewa huduma bila kujali itikadi zao.
Hata hili la itikadi siyo uhaini maana limeruhusiwa kikatiba.
 
Hawa jamaa huwa hawajui kabisa kuwa kauli zao za kutulazimisha kuchagua watu wao, hata kama hawatufai, kwa vitisho vya kutunyima maendeleo, huwa ZINATUTAPISHA!

SOME PEOPLE WENT TO SCHOOL TO COLLECT QUALIFICATIONS THEY USE FOR SELFISH GAINS ONLY!
😅
👊 ✌️✌️✌️💥
 
Hata mimi nashangaa anapoahidi kupeleka maji mbali wakati maeneo ya karibu ns ziwa hayana maji.
Kama anataka wagombea wake wapite ndio walete maendeleo basi afute uchaguzi anaofanya ni ufujaji wa pesa.
Kama anaona hawezi kuwapa haki sawa wananchi kwanini aliomba kuwaongoza.
 
Watendee mema watu wote lakini hasan wale wa nyumba ya Imani, wagalatia 6.10
 
Hii kauli Magufuli inabidi ashauriwe a wazee wa CCM asiitamke tena. Ipo siku mtasikia mkoa mzima wa Mtwara unadai kua nchi huru sababu wananyimwa maendeleo kisa wanachagua upinzani. Wajuzi wa mambo hivi mfano mkoa kama Mtwara, Tanga, na Mbeya zikitaka kujitoa Tanzania kila mtu mkoa wake uwe nchi huru kunaprocess gani zinafatwa.? Kuwagawa watu kimakundi mbaya sana especially sisi watanzania ambao kila Mkoa ukiamua uwe nchi idadi ya raia inatosha kabisa.
 
Back
Top Bottom