Uchaguzi 2020 Magufuli kakosea sana kampeni zake mkoani Mara. Je, haujui mkoa ule au hapendi watu wake?

Uchaguzi 2020 Magufuli kakosea sana kampeni zake mkoani Mara. Je, haujui mkoa ule au hapendi watu wake?

Yaani ni sawa na watoto wako badala ya kuwafugia kuku ili waje wale mayai tunawafugia chatu waje waliwe wao.
#CHAGUACCMKOMESHAWANAO
Na kwa nini dola inamshikilia huyu jamaa asiyefaa..

Si waache adondoke kwenye sanduku la kura. Ndio njia rahisi kumpumzisha..

Anaharibu hata umoja walioujenga kina Nyerere
 
Mgombea wa aina hii hatufai wa Tanzania, Hayupo kujenga umoja wa watu bali kubomoa miaka yote CCM imekuwa madarakani waseme ni sehemu gani ndani ya hii nchi inakila kitu

Kwa kifupi Ni aibu tokea Uhuru Hadi Leo bado watu wanashida ya maji, huduma za afya duni, makazi mabovu nyumba za udongo au nyasi, elimu duni, umasikini, hakuna ajira... Nk.
 
Salaam wana JF...

Jana tarehe 04.09.2020 nikiwa nimetulia sehemu nilibahatika kufungulia TBC1 na kukuta kampeni za Dkt. Magufuli akiwa mkoani Mara.

Muda wa alasiri, alikuwa Bunda, badae akapita na kusimama Kiabakari, ni eneo la mnada wilayani Butiama.
Leo najua atakuwa na mkutano Musoma mjini.

Mambo niliyoshangaa kwa Dkt. Magufuli:-

1. Aliwaambia wananchi wa Bunda kwamba hakuwafanyia maendeleo yoyote, kwa sababu wao walichagua upinzani.

-Akawauliza "nyinyi hamjiulizi mko karibu na Ziwa lakini hamna maji?"
-Akawauliza "hamuoni wenzenu Lamadi (mpakani mwa Bunda, jimbo Busega) wana taa za barabarani, nyie hamna?!"
- Akawaambia, hata barabara nimeendeleza zinazowazunguka hapa nikawaruka.

Mwisho akaishia kuwaambia mnichagulie mbunge wa CCM, na madiwani wa CCM.

Nilishangaa hakueleza zaidi atawafanyia nn, ila aliwaahidi kuwa mkinichagulia mbunge wa CCM nitakuja kuwashukuru, na siku hiyo ndio ntakuja na mipango yote kuibadilisha Bunda.

Akawasisitiza wasichague maupinzani tena.

ETI HAWEZI KUACHA MTOTO WAKE, AKAMHUDUMIA WA JIRANI.

Nampa pole Dkt. Magufuli kwa haya na timu yake ya kampeni.

Inaelekea hajui vizuri watu wa Mara (hasa eneo la Bunda).

-Moja, sio watu wa kutishiwa vitu kabisa. Pole Dkt. Magufuli

Kwa hili, Bunda umepoteza.
Wale wamezoea kuishi na upinzani tangu Nyerere akiwa hai.

Unamtishia mwana Bunda (Mwikizu, Msizaki, Mzanaki, Mkurya, n.k) vitu?!!!! Eti ndio akuchague?

UME FAIL....

Hawakuchagui, watasema baki na taa zako za barabarani.

Wale ni kina LadyJaydee hawatishwi na hawapigi magoti.

Sijui huko usukumani labda wanapiga magoti.

- Mbili,
Ni uongo mkubwa kwamba Bunda haina maendeleo kisa kuwa upinzani.

Nikuulize leo upo Musoma mjini, ambayo ipo CCM awamu hii yako ya kwanza;

Mbona Musoma mjini imefubaa kuliko Bunda?, mji umepotea na biashara haziendi mpaka watu wameukimbia?! Mbona huko yupo mbunge wa CCM?

Haya BUTIAMA je?

Mbona siku zote wapo CCM. Tena wanapitaga bila kupingwa. Mbona BUTIAMA imechoka sana.

- BUTIAMA haina maji, lakini ipo CCM.
Mbunge CCM, Madiwani CCM.

- BUTIAMA kampuni yako ya Mayanga imeshindwa kujenga Barabara ya Butiama - Serengeti, na hela walilipwa, Mradi wa kumalizika 2015, mpaka leo umekufa.

Mbunge CCM, Madiwani CCM.

- BUTIAMA haina hospital ya maana, Haina sekondari ya maana, Haina soko la maana.

Mbunge CCM, Madiwani CCM.

ACHA HADAA, HAKUNA CHA CCM.

-HALAFU UNAJIITA KABISA RAIS WA MAENEO YA CCM TU.!!

2. AKIWA KIABAKARI.
Akiwa hapa alisema tatizo kubwa la Jimbo la BUTIAMA, ni ukabila.

Aisee you're very WRONG.

Butiama haina ukabila kabisa.
Ndio maana hata ulivyosema hivyo niliona kila mtu ananyamaza.

Sijui ulimaanishi nini. Ila umedanganywa pakubwa, matatizo ya BUTIAMA ni mengine kabisa.

Nakuhurumia sana.

Halafu mu MSHAURI JPM AACHE KUTISHA WAPIGA KURA kwamba hatawafanyia maendeleo kwa vile wanachagua upinzani.

Ni uongo mkubwa...

Haya ni majimbo ambayo yapo CCM, lakini ni maskini vibaya sana..

1. BUTIAMA
2. BUKOMBE
3. BUSEGA
4. MANYONI
5. MUSOMA VIJIJINI
6. KIBITI
7. RUFIJI
8. MKURANGA
9. MVOMERO
10. UKONGA
11. KAKONKO
12. MAGU
13. IRAMBA
14. MAKETE
15. NEWALA
16. MTAMA
17. KIVUU
18. SUMBAWANGA
19. NZEGA KASKAZINI
20. NZEGA KUSINI
21. SENGEREMA
22. CHATO
23. LONGIDO
24...........

Mwana JF...

Taja MAJIMBO mengine yaliyopo CCM lakini ni maskini vibaya mno...

Comment hapa Chini.....
Huyo jamaa inawezekana nae ni kundi moja na Bashite i.e wote kichwani ni sifuri.
 
Mkuu, nilidhani kimeandikwa "Sasa unaingia Mkoa wa Mara". Neno KARIBU hakuna. Wanaume wale. Ukiingia jiaminishe. Hakuna aliyekukaribisha. Acha kulialia. Hahaha, kumbe Magu hawajui.
SASA UNAINGIA MKOA WA MARA.

Hakuna karibu.
 
Kwa kifupi Ni aibu tokea Uhuru Hadi Leo bado watu wanashida ya maji, huduma za afya duni, makazi mabovu nyumba za udongo au nyasi, elimu duni, umasikini, hakuna ajira... Nk.
Toka 1961 bado tunazungumza kujenga ZAHANATI na kuchonga MADAWATI????

CCM pumzikeni.
 
Asilimia 100 ya majimbo yote Tanzania ni masikini wa kutupwa. Sema mengine yamezidi umasikini.
hasa ya vijijini, hili huchagizwa sana na wadau wa maendeleo kutopenda kuwekeza miradi yao vijijini, pia hata wasomi hawapendi kuishi vijijini laiti wadau na wasomi wangewekeza maeneo wanakotoka nadhani vijijini pia pangekua na neema bt kwa hili serikali huwezi kuilaumu.
 
Usiseme kinadharia wewe. Umefika Mara? Kibao chao kimeandikwa "SASA UNAINGIA MKOA WA MARA". Neno KARIBU halipo.
Haya bwana na kibao chao. Nimekuelewa lakini Nungunungu na miba zake bado wachumba wanamjia na mimba wanamdunga.
 
Kama aliyasema hayo amekosea sana tena sana, akumbuke sio kila mtu ni mfatiliaji wa siasa hilo kundi linaumizwa na hao wapenda siasa lakini pia anatakiwa ajue maendeleo ni HAKI ya kila Mwananchi wa nchi husika, Siasa zisiifanye serikali kushindwa kutimiza majukumu yake, kama waliruhusu mfumo wa vyama vingi basi hawana budi kutenda mema kwa kila raia haijalishi ni chama gani.
 
Back
Top Bottom