Magufuli lala kwa Amani, kazi tunaiona kabla hata ya mwaka nusu

Magufuli lala kwa Amani, kazi tunaiona kabla hata ya mwaka nusu

Kiongozi hili bandiko lako linaonyesha changamoto tuliyonayo ya kuamini kwenye utashi binafsi badala ya kujenga mifumo ambayo itatuongoza wote leo na kesho.

Na hata angekuja MALAIKA, utaratibu na mazingira ya utawala yaliyopo..hatuwezi kutoboa!

Polepole alishindwa uongozi akiwa kwenye kiti leo anataka afundishe wengine akiwa darasani!
Hiyo mifumo kwa nchi yetu ni migumu wala haitosaidia chochote kwa kuwa kila raisi aingie ana madaraka makubwa bado anaweza akaifumua na akafanya mambo kwa utashi wake!
 
Wale mliojiaminisha miaka 30 ndiyo mnapata tabu alakini Dikteta kalala mungu aliona hili hatuwezi wenyewe akatusaidia kuondo fungu la miiba njiani,, sijawahi kuwa upande wa dikteta akiwa hai kuwa upande wake Sasa akiwa mfu Ni takuwa mnafiki sana,, ila ki uhalisia ametuingiza Chaka saana katuachia shida maana alikuwa shida pia ila kiukweli mpaka Sasa Nina furaha kuondoka kwake!!
 
The best ever one man army John Joseph Pombe Magufuli ulale kwa amani, uliona mbali kwa kutokucheka na kima hilo lilisababisha kupewa majina mabaya ya kuudhi ila leo kazi tunaiona hata kabla ya mwezi na nusu wale watu uliokuwa ukiishi nao wamebadilika labda kikubwa ni sherehe za mwenge kwenda kuzimiwa huko chato.

Mzee baba nchi inalia kukupoteza leo hii Membe anakushambulia ukiwa haupo wala huwezi kumjibu ila atajibiwa na Mungu leo hii yule uliyemsaidia kupita bila kupingwa eti nae anataka ukaguzi kwenye mikopo, Yule askofu sijui nani yule wa Chadema anakusema ulikufa kwa uviko wakati si kweli.

Mama nae anaishi mwezini kila baada ya mwezi anabeba group la watu kwenda nalo huko mwezini kwenye ziara za kutia hasara ambazo kipindi chako ulimtuma yeye.

Baba january anatuletea makampuni na ile mikataba ya kina karl peter wakati alitakiwa aelekeze nguvu bwawa la Nyerere.

Huyo job uliyemuamini hata kabla ya arobaini alikugeuka na kutaka mradi wa bandari ya Bagamoyo.

Mwanao pole pole bado anaendeleza mapambano lakini muda wowote atapigwa Tko, kaka Bashiru kakurwa sijui yu wapi tulipigwa wimbi moja tu wote tukapoteana

Soko letu la kale pale Kariakoo liliungua moto linajengwa upya, ndege bado tunaendelea kuzipokea.

Lala baba kizazi kitakukumbuka daima alama uliyoiwacha haitapotea. Itadumu milele.

NURU YA MILELE IKUANGAZIE
Msalime komredi mwalimu, komredi Mugabe, Komredi mao, komredi Mobuto, Komredi kwame, Samora, Mandela, castro, guevara na wenginio.

Tunawakumbuka daima!
Sukuma Gang, ilifia wapi???
 
Back
Top Bottom