Elections 2015 Magufuli lugha za Kimataifa ni Kizungumkuti, wenye ufahamu tujadiliane

Wewe! tulia upakatwe acha kutapatapa. Magufuli yuko vizuri sana. halafu ngeri sio kigezo. tunachagua Rais wa Tanzania na sio rais wa ughaibuni. plz kuwa muelewa
 
ndugu zangu wakawa kwasasa ni magufuli kushinda na kuingia ikulu kuhusu kizungu tutashughulikia baadae
 
[/QUOTE]

Kuishiwa hoja huko...kiingereza kinahusiana vip na maendeleo yetu..
 
Last edited by a moderator:
ndo maana mikataba inasainiwa miaka 100 kumbe lugha hamna kwa viongozi wetu
 
Nasikia eti baada ya kuhutubia hapo ikawa zamu yao hao wazungu kuhutubia na yeye akawa mtafsiri. Walipomaliza wakawaaga wananchi Bye! Bye! Na yeye akawatafsiria Nunua! Nunua!

Ha ha haaaaaaa tehe tehe tehe
 

Magufuli ni mtu wa Kemia na mathematics, matumizi yake ya kiingereza yako limited katika kubalance equations, tests, na vitu related. Pia, Magufuli sio Muingereza, Ni Mtanzania aliekulia na kusomea Tanzania katika shule za kawaida. Hadhira yake katika siasa kwa kiasi kikubwa imekuwa ya Watanzania, sasa kuna umuhimu gani wa yeye kukijua kiingereza kama anaotarajiwa kuwasiliana nao ni watu wasiokijua kiingereza. Tunahitaji kumuelewa anachozungumza na si kusikilizwa na wazungu hasa katika kipindi hiki ambapo tumejidhatiti katika kupunguza utegemezi wa misaada ya hao wenye kiingereza chao. Issue ya kushangaza, ni mtu wa arts asieweza kuongea kiingereza kwa nadhani hilo ndilo la msingi.
 

anazidiwa hata na diamond platenum mwenye elimu ya darasa la saba
 

Asante, nimekuelewa vizuri.
Mimi nilihoji tu, ila NIMESHAMPIMA KWA VIGEZO VYANGU na kapita with flying colors, ndiye mwenye kura yangu tarehe 25.10.2015.
 
Magufuli ni msomi aso na shaka, inawezekana hata darasani somo la lugha lilimpiga chenga maana hata ukisikiliza anapozungumza kiswahili ni dhahiri(anafikiri) anatafsiri toka kikwao, raisi wa japan hajui kingereza, hata putin hajui kingereza, na lugha sio kigezo cha weledi wa uongozi, uongozi hauna lugha ni karama toka kwa muumba, kama kuna wasiwasi na usomi wake ulinganishwe na wakemia wenzake, watoeni popote ulimwenguni uwafanyie majaribio uone -HAPA KAZI TU.
 
Yaan hii ni aibu sana pombe hajui kiingereza mm nimeleta hapa uzi kuhusu kingereza cha pombe magamba wakabisha.

Tena wengine wakasema eti pombe atauwa anatembea na mkalimani. Hiyo bajeti itatoka wapi?

Mjionee bandugu pombe ni aibu
 
Nasikia alisomea Lake Sekondari ya Mwanza. Kwa wakati wake yeyote aliyemaliza sekondari ya Lake ni wale waliokuwa na kiwango kidogo cha ushindi kwa maana nyingine kwa wakati ule walikuwa wanaenda walioshindwa na kama Baba yako ana uwezo wa kifedha unapelekwa Lake.
 
Yaan hii ni aibu sana pombe hajui kiingereza mm nimeleta hapa uzi kuhusu kingereza cha pombe magamba wakabisha.

Tena wengine wakasema eti pombe atauwa anatembea na mkalimani. Hiyo bajeti itatoka wapi?

Mjionee bandugu pombe ni aibu

Lowassa mnatarajia kuwa atakuwa anatembea na watu wangapi wa ziada ukiacha Walinzi, mpambe na mkalimani? Kuna watu wa kutunza na kunote mawazo yake, kuna mtu wa kumkumbusha vitu basic kabisa vya maisha yake ya kila siku, kuna mtu wa kuzungumza na kuhutubia kwa niaba yake maana Sumaye hatakuwa karibu, kuna madaktari, kuna mtu wa kumpigia signature maana kwa mambo yalivyo! Sasa wote hao ni kwa bajeti ipi? Msitudanganye kuwa eti ana pesa, maana tunajua mpaka sasa mtaji umekata.
 

Watu wametengeneza video halafu wanajaribu kufosi kingi kisela tu.
 
Natumia simu ya mkononi kwa sasa na bahati mbaya imeshindwa kufungua hiyo You Tube video.Ila niseme wazi,kama dokezo hilo kweli ndiyo sample ya kingereza chake it's a disaster.Something is seriously wrong.Daktari wa Filosofia awe na kingereza kibovu namna hiyo.Hapana,ipo shida.Na itakuwaje sasa katika mawasiliano ya kimataifa?Yetu macho. [/QUOTE]
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…