Mahakama hazikuwa zikitenda haki kuhusu kesi za Uhujumu Uchumi

Mahakama hazikuwa zikitenda haki kuhusu kesi za Uhujumu Uchumi

Habari ya ''mujini'' ilikuwa ama uhujumu uchumi au utakatishaji fedha au yote kwa pamoja. Wakikukosa kabisa wanakuwekea noti ya elfu tano njiani ukidhani una bahati na kuokota unaambiwa umetenda kosa la kutakatisha pesa.

Walikuwa kama wamepagawa. Kidogo nikiazima kutoka kwa beberu - "they're like possessed by the devil himself!"

Hiiiiii bagosha!
 
Wengi sana Mkuu na wameporwa mamilioni yao kama si mabilioni na yule dhalimu mwendazake na washirika wake. Huyu mmoja tu walitaka kumpora milioni 200!!!! Bado kuna wale wa maduka ya kuuza FOREX Arusha na Dar ambao nao waliporwa pesa nyingi sana zikiwemo T shs.

Huyo ndiyo tukiaminishwa ana legacy ya kulindwa. Tukisukumwa kuridhia jiwe day na yeye kuwa baba wa taifa.

Washindwe, watepete na kubaki na m@vi yao.

Katelefoni swahiba wake mkuu angalipo kule anafanya nini Yarabi?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Huu msamiati wa Uhujumu Uchumi una shida sana, ulianza na Mwl Jk, PM akiwa Edo, kweli watu walienda ndani baadae akaja mzee Ruksa na wengine hadi awamu jumuishi, sasa kumekuja awamu juimushi .
Huu msamiati UFUTWE kwanza hatuna watu wa namna hiyo Tz,
Tunao wafanyabiashara wazalendo wa kwetu, pia wawekezaji wenye uweledi hizi hujuma zinatoka waaapi?

Watu watoke, anagalau mtaani tuweke heshima ajira zimwagike,
Nani anasema huyu anahujumu, Umemuaona? Thibitisha.
Nani anaweza kuiba vya kwao? Hamna
Nani anaweza ku risk afunge safari toka mbali kwa lengo la kuhujumu serkali na watu wake? Hakuna

Msamiati huu ufutwe. Wivu tu

Huwezi kupora mali halali ya mwenzako ukabaki salama
 
  • Thanks
Reactions: Qwy
Wale wapuuzi wake ndani ya chama na Serikali eti walitaka TUMUENZI!!! Una enzi kipi kwa mtu muovu kama yule!?

Huyo ndiyo tukiaminishwa ana legacy ya kulindwa. Tukisukumwa kuridhia jiwe day na yeye kuwa baba wa taifa.

Washindwe, watepete na kubaki na m@vi yao.

Katelefoni swahiba wake mkuu angalipo kule anafanya nini Yarabi?
 
Wale wapuuzi wake ndani ya chama na Serikali eti walitaka TUMUENZI!!! Una enzi kipi kwa mtu muovu kama yule!?

Walivyopoa sasa hivi bila shaka busara imeanza kuwarejea na kutambua kuwa wamepwelewa.

Bado tuna yetu Mama itabidi atupe kwani twayaomba kwa nia njema na kumsaidia yeye pia:

1. Ripoti ya tume za CAG BOT na TPA.
2. Hitajio la Katiba mpya.
3. Mikutano yake na vyama vya siasa.
4. Haki kwa wote waliodhulumiwa awamu ile.

Moja moja tutalidondoa kwa mapana na marefu yake. Tulishaumwa na nyoka. Hatuwezi kuwaweka rehani watoto au watoto wa watoto wetu tena.

Hakuna ajizi, maana hiyo ni nyumba ya njaa.

La Corona amekishaliwekea mwelekeo. Hapo tunatarajia takwimu kuelekea chanjo.

Mola na amjaliei afya, utashi na uthubutu Mama yetu huyu dhidi ya yaliyowashinda.

Nisiache kumsalimia Mama kwa jina la JMT.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Yule muovu kaondoka kwa laana ya machozi ya wengi,angepewa haki ya kugawa pumzi duniani wallahi hakuna angebakia hai.Hata kama ungebakia hai ungeinunua kwa bei kubwa Sana.
 
Kuna kapewa uhujumu uchumi kwa sababu ya elf 5 na akalipa milioni 15 Ili kununua uhuru wake sembuse hayo mamilioni.
 
Ndugu yangu mmoja alishtakiwa kwa uhujumu uchumi akituhumiwa kukwepa kodi kwenye biashara zake. Lakini yeye anadai ni kesi ya kisiasa. Mwaka 2015 aliombwa kusupport kampeni za CCM akakataa lakini alifadhili kampeni za UKAWA. Anaamini hiki ndicho kilichomponza.

Mwaka 2018 alikamatwa na baadhi ya biashara zake kufungwa, na nyingine zikashindwa kujiendesha kutokana na makadirio makubwa ya kodi.

Baada ya kukaa gerezani miaka miwili akaona bora akiri ili atoke (the lesser evil). Wakati wa majadiliano na DPP akatakiwa kulipa zaidi ya 200M. Akakubali kufilisi biashara zake chache zilizobakia ili "kununua" uhuru wake.

Mwaka jana tulimtembelea gerezani mimi na Dr.Cyrilo. Tukamuuliza kwanini umeamua kukiri? Huoni itakuwekea doa? Kuna nchi utazuiwa kwenda kwa sababu ya "criminal record" ya uhujumu uchumi. Kuna fursa za biashara utashindwa kupata. Kwanini usingepambana ushinde badala ya kukiri.

Huku akilengwalengwa na machozi akajibu, nachotaka kwa sasa ni kuwa huru tu. Nikishatoka hiyo "criminal record" anaweza kuja Rais mwingine akaifuta, huwezi jua. Tukaagana, akarudi zake nyuma ya nondo.

Licha ya kukiri na kuwa tayari kulipa (plea burgaining) lakini bado hakuachiwa. Aliambiwa jalada bado lipo kwa DPP.

Wiki iliyopita amefutiwa mashtaka yote na kuachiwa huru, bila kulipa chochote. Siku anaachiwa wala hakujua kama angeachiwa. Ilitumwa "remove order" gerezani, akaenda mahakani bila kubeba chochote maana haikua siku ya kesi. Hata wakili wake hakuwepo.

Miguuni alivaa kandambili. Alipofika mahakamani akaambiwa, Jamhuri imekufutia mashtka yote na haina nia ya kuendelea na kesi. Akadhani ni mtego ili wamkamate tena. Akajaribu kutoka nje ya mahakama, lakini hakuna mtu aliyehangaika nae.

Akaita taxi, ikampeleka nyumbani. Mkewe akapata suprise ambayo hakuitegemea. Akaanguka, alipoamka akaanza kulia. Watoto walipomuona baba yao nao wakalia. Majirani wakaja na kumkumbatia, wakilia. Nyumba ikatawala machozi.

Hii nchi imepitia kipindi kigumu sana. Kuna jinsi Mungu anamtumia mama Samia kuponya majeraha na kuokoa mioyo iliyopondeka. Biblia inasema Haki huinua taifa bali dhambi ni aibu ya watu wowote (Mithali 14:34).!


Malisa GJ
Hivi tunawezaje kuacha mambo haya bila kulipa visasi ?
 
Kwa nini chama tawala huwa kinafikiri ni lazima wafanyabiashara wakichangie?

Chini ya jiwe walijimilikisha nchi na vyote vilivyomo. Walikuwa wakituona kama mifugo tu.

Tulipo upepo umegeuka. Tunataka haki sawa kwa wote na vikorombwezo vyake vyote. Wala hatutanii.

Tunayemwelewa Mama. Katelefoni hata akirudi Ruangwa wala hatuna pressure naye iwapo hatatajwa kwenye kadhia za kina Ben, Azory, na wote waliopotea.

Kwani haki sawa ni nini basi?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Sio tu uhujumu uchumi, chochote kile kilichokuwa kinaanza na neno vita hakikiwa fair, ile vita ya madwa ya kulevya ya DAB isikie tu, nigekuwa ndani sasa hivi kama sio kuhamisha makazi kwa muda usiojulikana🤣
 
Hivi Mustapha Sabodo yupo wapi kwa sasa?

Enzi za Kikwete Mr Sabodo alikuwa anatoa msaada wa hela, kwa CCM na Upinzani. Ilikuwa wazi kabisa, wala haikuwa siri. Alikuwa neutral.

Tangu alipoingia jiwe hakusikika tena! Yupo wapi kwa sasa?
 
Sio tu uhujumu uchumi, chochote kile kilichokuwa kinaanza na neno vita hakikiwa fair, ile vita ya madwa ya kulevya ya DAB isikie tu, nigekuwa ndani sasa hivi kama sio kuhamisha makazi kwa muda usiojulikana🤣

Pole sana mkuu.

Kenya wanawaita wakora. Wale jamaa walikuwa wakora tu.

Wakora - wezi, vibaka, majambazi, mabazazi, Mabedui, majahili, mafedhuli, nk. Yaani mkuluro wote huo.

Huna utu, huruma wala hujali haki za wengine, wewe ni mtu wa namna gani?
 
Nchi ina usalama wa taifa halafu mtu bogazi kama Magufuli anaruhusiwa kugombea urais!!!.
 
Hivi kile kipengele ch " Awe na akili timamu" huwa wanakifuata kweli?
Maaana MAGUFULI hakuwa na akili timamu.
 
Ndugu yangu mmoja alishtakiwa kwa uhujumu uchumi akituhumiwa kukwepa kodi kwenye biashara zake. Lakini yeye anadai ni kesi ya kisiasa. Mwaka 2015 aliombwa kusupport kampeni za CCM akakataa lakini alifadhili kampeni za UKAWA. Anaamini hiki ndicho kilichomponza.

Mwaka 2018 alikamatwa na baadhi ya biashara zake kufungwa, na nyingine zikashindwa kujiendesha kutokana na makadirio makubwa ya kodi.

Baada ya kukaa gerezani miaka miwili akaona bora akiri ili atoke (the lesser evil). Wakati wa majadiliano na DPP akatakiwa kulipa zaidi ya 200M. Akakubali kufilisi biashara zake chache zilizobakia ili "kununua" uhuru wake.

Mwaka jana tulimtembelea gerezani mimi na Dr.Cyrilo. Tukamuuliza kwanini umeamua kukiri? Huoni itakuwekea doa? Kuna nchi utazuiwa kwenda kwa sababu ya "criminal record" ya uhujumu uchumi. Kuna fursa za biashara utashindwa kupata. Kwanini usingepambana ushinde badala ya kukiri.

Huku akilengwalengwa na machozi akajibu, nachotaka kwa sasa ni kuwa huru tu. Nikishatoka hiyo "criminal record" anaweza kuja Rais mwingine akaifuta, huwezi jua. Tukaagana, akarudi zake nyuma ya nondo.

Licha ya kukiri na kuwa tayari kulipa (plea burgaining) lakini bado hakuachiwa. Aliambiwa jalada bado lipo kwa DPP.

Wiki iliyopita amefutiwa mashtaka yote na kuachiwa huru, bila kulipa chochote. Siku anaachiwa wala hakujua kama angeachiwa. Ilitumwa "remove order" gerezani, akaenda mahakani bila kubeba chochote maana haikua siku ya kesi. Hata wakili wake hakuwepo.

Miguuni alivaa kandambili. Alipofika mahakamani akaambiwa, Jamhuri imekufutia mashtka yote na haina nia ya kuendelea na kesi. Akadhani ni mtego ili wamkamate tena. Akajaribu kutoka nje ya mahakama, lakini hakuna mtu aliyehangaika nae.

Akaita taxi, ikampeleka nyumbani. Mkewe akapata suprise ambayo hakuitegemea. Akaanguka, alipoamka akaanza kulia. Watoto walipomuona baba yao nao wakalia. Majirani wakaja na kumkumbatia, wakilia. Nyumba ikatawala machozi.

Hii nchi imepitia kipindi kigumu sana. Kuna jinsi Mungu anamtumia mama Samia kuponya majeraha na kuokoa mioyo iliyopondeka. Biblia inasema Haki huinua taifa bali dhambi ni aibu ya watu wowote (Mithali 14:34).!


Malisa GJ
Acha uongo mbona huyo ndugu yako humtaji jina. Mnatunga uongo kumdemonise magufuli na kujidai samia ni mtu wenu wapinzani. Mijitu ilikua inafanya magendo au kukwepa kodi mnajifanya ndio wema. Unafikiri bila kodi nchi itafanyaje maendeleo. To hell na li chadema lenu. Jpm yupo tu wala hamuwezi kufuta legacy yake kwa uongo.
 
Back
Top Bottom