Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa yatupilia mbali mapingamizi 2 kesi ndogo ya Mbowe na Wenzake. Jaji Siyani ajitoa kuendelea na kesi

Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa yatupilia mbali mapingamizi 2 kesi ndogo ya Mbowe na Wenzake. Jaji Siyani ajitoa kuendelea na kesi

Hili likesi na makesi yote yaliyoanzishwa awamu ya 5 kwa nia ovu yafutwe, Hangaya na vyombo vyake vya usalama wanashindwa kuona hili? Asubiri hawa akina Mwamba kama watafanya makosa (Ya ukweli) kwenye awamu yake ndipo "arare nao mbere", makesi mengi ya awamu ya 5 yana ukakasi sana. Mfano mmoja tu, Bwana Mrosso asingekuwa na mil 90 ya kumpa Sabaya leo hii angekuwa ndani kwa kesi ya kubambikiwa ya uhujumu uchumi na utakatishaji!! DPP na watu wako futeni hii kesi......
Leo nimekupa Like yangu, Mama aache kubambakia watu kesi. Huku mtaani mama anafanya vizuri sana ni vyema akaachana na hii kesi ya mbowe itamuondolea yale mazuri yote ambayo ameanza kuyafanya ndani ya miezi 7 ya uongozi wake.
 
Ile rushwa ya kupewa ujaji kiongozi haikuwa bure.

Kama hakutakuwa na jitihada nyingine, nje ya kutegemea mahakama ambayo haina uhuru, tutarajie mambo ya ajabu, yasiyotegemewa.
Hizo jitihada nyingine Ni zipi ndg, Kama katiba mpya ndiyo hyo inakula msoto gerezani , na jaji kiongozi + Hangaya ndiyo wanaikanyaga!!
 
Nadhani kama ipo fursa ya kukata rufaa katika kesi hii ndogo ndani ya kesi kubwa Mawakili wa utetezi ni bora wafanye haraka.

Jaji Kiongozi katika shauri hili alionyesha utulivu wa hali ya juu kiasi kuwaaminisha wale wote waliokuwa wakifuatilia shauri hili kwamba angetenda haki na haki ikaonekana.

Rais kwa kutumia mamlaka yake ajamteua katika nafasi ya Jaji Kiongozi.Hata namna alivyotoa hitimisho lake unaona wazi kaamua kuwafurahisha waliompatia nafasi hiyo.

Kupitia kesi hii unaona kabisa umuhimu wa katiba mpya.
 
Siamini Kama kweli Mbowe alikula njama ovu, Ila kwa trend ninayoiona, hapa anafungwa mchana kweupe.

Huenda wale waliokimbi nchi wamemponza.
 
Mengi ya gizani hatuyajuia, mambo ya kimafia hayafanyika mwangani mchana hapana hufanyika gizani.....Mawakili tujikite zaidi kwenye kesi yenyewe kupangua kila kinachokuja... Haki haishindwi...itaonekana tu nani mwenye haki nani hana haki....

Ila kama wote wamehusika kwenye michezo michafu gizani basi hapo ujue atakayeshinda ni aliyesukuma kete vizuri...
 
Shukrani ya kuteuliwa kuwa jaji kiongozi ni lazima Mbowe afungwe 😞
Mashauri yote mawili kayatupa kizembe kwa hoja ambazo ata yeye mwenyewe zinaonyesha upendeleo, yani hoja zote zilikuwa zinabana upande wa utetezi alafu mwisho anakuja anasema mimi naona ... Alafu eti court n mhimili unaojitegemea!!!
 
hiyo umesema wewe, kuna jembe linakuja lililompindua dikteta magufuli, ambalo kwa huyu mama yenu aliyepo sasa, kwake ni sawa na kunywa maji ya kunywa. Naye ni mwamba aliyeshindikana, TUNDU ANTIPHAS LISSU. Mwamba wa upinzani Africa.
😲😲🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Huyu Lissu huyu rafiki wa huyu bwana aitwaye David Mc Allister ?!!
IDU_David_McAllister-600x600.jpg
 
Naona kila mmoja sasa anaanza kulalamika kuhusu Jaji hii ndio Tanzania yetu
 
jaji: Kama Shauri likienda mfululizo ingechukua Miezi kama Minne

jaji: Hivyo kwa Majukumu niliyonayo nimeona nijitoe aje Jaji mwingine haraka iwezekanavyo.
 
UPDATE: MWENYEKITI WA CHADEMA NA WENZAKE WAMEHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 30 PAMOJA NA FAINI YA MILIONI 460
 
Leo ni leo 🔥🔥 mapingamizi mawili yote yametupiliwa mbali. Watu hawataamini kiongozi wa upinzani kuswekwa ndani😂😂😂, nakumbuka kiongozi wa nchi alisema "mbowe n gaidi na ushahidi huo upo", nyie mnataka hao mabwana wa kuteuliwa wafanyaje? Bado mahakama zetu hazijitegemei. Kenya wametuzidi maendeleo yote yote tu kasoro maendeleo ya kujisifu ndiyo tumewazidi😂😂
Mahakama haitishiwi na midemuko ya JF.

Sabaya alipohukumiwa hamukusema majaji wa kuteuliwa leo kulikoni.

Jaji hakikisha unatenda haki bila kuangalia sura Wala umaarufu wa mtu,wala kuaangalia wale vibaraka waliomtuma kila siku wako mahakamani kuhakikisha hawataji.
 
Back
Top Bottom