LULU AKIJITETEA MAHAKAMANI
"Nilipofika kwa marehemu 'Kanumba' nilimkuta yupo kwenye dressing table,nilikaa kitandani kwa kuwa hapa kuwa na sehemu ya kukaa...Nilikuwa nataka kutoka ila marehemu 'Kanumba' alinikataza,alikuwa hataki nitoke na marafiki zangu,Marehemu nilipomwambia natoka na marafiki zangu alinikimbiza na taulo na mimi nilikuwa naogopa kupigwa.
Mara nyingi marehemu alikuwa ananipiga kila akilewa na sio kwa akili zake.
Alipoona simu yangu inaita akahisi ni simu ya mwanaume akasema kwanini naongea na simu ya mwanaume mbele yake,Marehemu akaingia uvunguni akatoa panga akasema leo nakuua huku akinipiga na panga kwenye mapaja.
Marehemu alianguka mwenyewe na kujigonga kwa nguvu na kuinuka sehemu nyingine alikuwa kama anatapatapa.
Nilipoona hivyo nilitoka nikakimbilia chooni na kupiga kelele, Nilipotoka chooni Nilimkuta amelala,nilihisi amejifanyisha nikaanza kumwambia kuwa wakija watu nitawambia kila kitu ulivyonipiga na panga.
Baada ya muda mchache nilisikia kishindo kama mtu anafungua mlango,Nilimwambia Seth kuwa Kanumba amedondoka na akajaribu kumuamsha hakuamka akasema anaenda kumuita daktari
Alivyosema anaenda kumuita daktari nikasema na mimi naondoka nikiogopa anaweza akaamka akaanza kunipiga tena,Niliondoka nikawasha gari kuelekea Coco Beach, Huko Coco Beach hakukuwa na kitu nilienda tu kutuliza akili.
Nilivyofika Coco Beach SMS zilianza kusambaa kuniuliza kuwa nasikia Kanumba amefariki,Nikachukua simu nikampigia kidume 'rafiki yake Kanumba' kumuuliza Kanumba yupo hospitali gani? nije kumuona
Akaniambia wewe usije hospitali,niambie uko wapi tuonane Bamaga? "
Tulivyokutana Bamaga alikuwa kama anataka kuongea na mimi ghafla wakaja askari kunikamata Na kunipeleka Oysterbay polisi,Nilipofika Oysterbay nilikuta watu wengi sana niliyemtambua ni Ray
Nilijua Kanumba amefariki nikiwa polisi,Nilipomkuta Ray Oysterbay polisi nikajua Kanumba amekamatwa kwasababu ya makelele niliyokuwa nayapiga kule nikajua watu walisikia.
Kwa namna yoyote ile mimi sijasababisha kifo cha Kanumba,na mimi ndiye nilieshambuliwa na marehemu kutokana na umbile langu nilikuwa mdogo na alikuwa na uwezo wa kufanya chochote kwenye mwili wangu kwa sababu yeye ndo alikuwa na silaha.
Huu ndio utetezi wa Lulu tusubirie Maswali ya kutoka kwa mawakili wa upande wa serikali na wale wa upande wa mtetezi