Mahakama Kuu yamhukumu Grace Mushi kunyongwa hadi kufa kwa kumchoma mpenzi wake ndani ya nyumba mpaka kufa

Mahakama Kuu yamhukumu Grace Mushi kunyongwa hadi kufa kwa kumchoma mpenzi wake ndani ya nyumba mpaka kufa

Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam imemuhukumu leo kunyongwa hadi kufa Grace Mushi (25) maarufu kama Neema baada ya kumtia hatiani kwa kumuua mpenzi wake Abdallah Sekamba.

Grace alimuua mpenzi wake kwa kumchoma moto hadi kufa kwa kutumia mafuta ya petrol, baada ya kumfungia ndani ya nyumba tukio alilolitenda Julai 16, 2021 eneo la Mbezi Makabe Dar es salaam.



Ilivyokuwa...

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limethibitisha kumshikilia Grace Mushi maarufu mtaani kwao kwa jina la Neema kwa tuhuma za mauaji ya mpenzi wake Hamis Abdallah ‘Zungu’ ambaye alimmwagia Petroli akiwa ndani kisha kumchoma moto.

Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam, ACP Muliro Jumanne Muliro amesema tukio hilo limetokea Mbezi Makabe kwa Mzungu.

"Muda wa saa 8:30 usiku Mtuhumiwa huyu alimfungia ndani ya nyumba Hamis akammwagia mafuta ya Petrol na baadaye akachoma moto kitu kilichosababisha Hamisi kufariki”

“Hamis alikua ni Rafiki yake wa kiume (Boyfriend), Mtuhumiwa alijaribu kutoroka lakini Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Wananchi tukamkamkata na uchunguzi umebaini kulikuwa na mgogoro mkubwa wa kimapenzi kabla kufanyika kwa tukio hili la Kikatili
mshahara wa dhambi ni mauti 🐒
 
Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam imemuhukumu leo kunyongwa hadi kufa Grace Mushi (25) maarufu kama Neema baada ya kumtia hatiani kwa kumuua mpenzi wake Abdallah Sekamba.

Grace alimuua mpenzi wake kwa kumchoma moto hadi kufa kwa kutumia mafuta ya petrol, baada ya kumfungia ndani ya nyumba tukio alilolitenda Julai 16, 2021 eneo la Mbezi Makabe Dar es salaam.



Ilivyokuwa...

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limethibitisha kumshikilia Grace Mushi maarufu mtaani kwao kwa jina la Neema kwa tuhuma za mauaji ya mpenzi wake Hamis Abdallah ‘Zungu’ ambaye alimmwagia Petroli akiwa ndani kisha kumchoma moto.

Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam, ACP Muliro Jumanne Muliro amesema tukio hilo limetokea Mbezi Makabe kwa Mzungu.

"Muda wa saa 8:30 usiku Mtuhumiwa huyu alimfungia ndani ya nyumba Hamis akammwagia mafuta ya Petrol na baadaye akachoma moto kitu kilichosababisha Hamisi kufariki”

“Hamis alikua ni Rafiki yake wa kiume (Boyfriend), Mtuhumiwa alijaribu kutoroka lakini Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Wananchi tukamkamkata na uchunguzi umebaini kulikuwa na mgogoro mkubwa wa kimapenzi kabla kufanyika kwa tukio hili la Kikatili
All in all, sisi sote tu wenye dhambi, na tumepungukiwa na utukufu wa Mungu, Mungu anatupenda sote hivi hivi tulivyo, wengine wachawi, wengine wauaji, wengine wazinzi, wengine waongo, wengine wezi, wengine dhambi mbalimbali, Mungu anatuhitaji sote hivi hivi tulivyo tuipokee neema ya Wokovu kwa njia ya Yesu Kristo. huyo hivyo hivyo anavyoonekana na kuhukumiwa Mungu anampenda na anahitaji roho yake ipone, watu ndio tujue ukiwa nje ya Yesu lolote linaweza kukupata, shetani anaweza kukutumia kufanya kitu cha ajabu kabisa halafu ukinasa anakuacha anakutelekeza, sivyo alivyo Yesu, amesema yeyote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe, na kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka.

nakushauri wewe ambaye maisha yako bado yapo mikononi mwa shetani, mwisho wako hautakuwa mzuri ama hapa duniani ama baada ya kifo, ni heri kuwa mikononi mwa Mungu, heri uyakabidhi maisha yako kwa Mungu leo, uokoke, nawe utamwona Mungu katika maisha yako.
 
Back
Top Bottom