Mahakama ya ICSID: Professional bullying anayofanyiwa Profesa Mruma inafedhehesha jamii ya Wanazuoni

Academicians wanatakiwa ku translate nondo zao to the real world!
Hapo ni unasema Mwalimu wa ujasiliamali wa Chuo anatakiwa kuonesha utajiri wake ,hii haipo popote Duniani kazi Yao ni research wakatumie wengine
 
Hakuna cha bullying hapo, hizo ni mbinu za wanasheria utetereke. Lakini Profesa Mruma kajibu na kujieleza vzuri kabisa.
Acha ukenge... hamna alichojieleza zaidi ya kujikanyaga... angekua bongo hapo akisoma yale maripoti yao uchwara unaweza muona wa maana sana huku akijifuta jasho kumbe hopeless kabisa!

Ni kama Samia tu... mtu mwenye akili huwezi jiingiza kichwa kichwa kwenye uchafu kama ule mkataba.
 
Hapo ni unasema Mwalimu wa ujasiliamali wa Chuo anatakiwa kuonesha utajiri wake ,hii haipo popote Duniani kazi Yao ni research wakatumie wengine
Unajiingiza kwenye mijadala usiyoielewa, kwahiyo hapo Mruma anafanya nini?
 
UVCCM mbona hamtoi comments zenu kwenye hii ishu au ndio tuseme ni mambo ya kitaalamu sana yapo nje ya uwezo wenu wa kufikiri?🀣🀣🀣🀣🀣
 
Haya yata mtokea tena prof mwingine wa Dp world hivi karibuni. Yaani Mruma hajui ashike wapi? Amebaki kusema serikali ilikuwa na imani na muwekezaji. Ana rusha rusha mikono utadhani ni bubu. Maskiniii
Na kutoa ulimi kama nyoka,hii ni aibu kwa taifa.
 
Hivyo ndivyo ilivyo. Inapigwa dili hapo, mkishinda tutalipa, mnatupa cha kwetu, mnasepa, tunasingizia jpm katufikisha hapa
 
Ni witness. Mawakili wamembeba akawe shahidi kwenye kesi kwa sababu ya nafasi aliyowahi kuteuliwa kuishikilia.
 
''Ifike mahali'' ni msemo unaosemwa kila siku lakini abadan haitakaa ''ifike hapo mahali''. Wataalam unawatetea bure. Nakuhakikishia wangekuwa na misimamo na kuweka njaa pembeni viongozi wangebadilika. Hivyo basi, wakulaumiwa ni wataalam wenyewe. Hebu chukulia mfano wa huu mkataba wa bandari. Kuna huyu ''profesa'' mwingine njaa ndugu Kitila ndiyo yuko mbele kuutetea kwa nguvu zote. Mambo yakija kuharibika unaweza kuacha kumlaumu? Ni nini basi maana ya kusoma na kuwa mtaalam kama akija mtu anaweza kukushawishi ufanye kinyume na utaalam wako? Unakumbuka Magufuli na corona? Unakumbuka wataalam wa afya walivyokubali kuendeshwa na kufanya mambo ya hovyo kabisa? Who knows pengine wangemkatalia na kusisitiza afuate utaalam, pengine angekuwa hai sasa!
 
Tatizo kubwa la nchi hii watu hawana Professional Intergrity.
Wasomi wengi wanaendeshwa na Wanasiasa.

Kwenye la kuvunja mikataba wa kulaumiwa anajulikana wala sio Prof. Mruma
Mikataba ilivunjwa kwa sababu ni mibovu na yenye vipengele vyenye kuumiza kwa miaka mingi ijayo, yote awamu ya 4 hiyo. solution ni kuvunja sasa, gharama si kubwa kuliko kuacha tunyonywe milele.
Ndo kitu hicho hicho mnachopambana sasa hivi mkataba wa DP world uvunjwe hata kama tutalipa itakuwa athari ndogo. Mnajifanya kusahau. Akivunja jpm mkataba wa ovyo anaonekana kaingiza hasara coz mnamchukia au maybe wengine mlinufaika na mikataba hiyo?
Mali yetu wenyewe halafu tunabanwa na vifungu, tunapata tu mrabaha 3% ya faida baada ya kutoa ops costs. wala haturuhusiwi kuvunja. Eti ajira, ngapi?
 
Usipotoshe watu kwa masilahi yako. Lete video yote humu. Shida yetu watanzania hatujiongezi zaidi. Lete hapa habari kamili. Kesi ilikuwa inahusu nini na hoja za wenzetu zilikuwaje na sisi tulitoa utetezi gani?.

Naona hao kwanza wamejitahidi mno. Na sijui kana kesi hiyo inayotajwa ndio hiyo tumeshindwa. Ila kikawaida mahamani kushindwa au kushinda kuna sababu nyingi.


TUIPENDE NCHI YETU, TUACHE KUSHADADIA MABEBERU. WEWE UNASHANGILIA KUPIGWA BADALA YA KUSEMA TUTAPAMBANA KULINDA RASILIMALI ZA TAIFA?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…