Mahakama ya Kimataifa ya ICC yatoa hati ya kukamatwa kwa Rais Vladmir Putin wa Urusi

Kabla ya kuzifikia kivipi? Nuke anayetangulia ndio anakuangamiza na maumivu yake hutaweza kurudisha. Hata ukirudisha kashakuvurumishia jingine utatoboaje?
 
Hata Putin sasa hivi akiamuwa kwenda Marekani kuudhuria kikao cha umoja wa mataifa hakuna atakaye thubutu kumkamata kama walimshindwa Albashir wa Sudan pamoja na kutembelea mataifa kibao ndo waje wamkamate Putin.
Hujui siasa za kimataifa na hufuatilii

Ataenda kwa usafiri upi wakati ndege zote za Russia zina vikwazo vya Anga Marekani

Pili yeye na familia yake hawaruhusiwi kukanyaga marekani wako blacklisted ulaya na marekani kwa majina yao
 
Hiyo mahakama haina meno na hiyo warant imetolewa kuiridhisha tu Ukraine lakini kiufupi ni ngumu kutekerezeka hata nchi za Magharibi zina jua.

Hata ikitokea akapinduliwa watakao mpindua hawawezi kumpeleka kwenye hiyo mahakama.
Sikupingi boss sababu Siijui Urusi na mambo wanayoweza au wasiyoweza kuyafanya kwa viongozi wao ila najua ni nchi kubwa na yenye nguvu ya kijeshi.

Wasipomkamata sitashangaa, wakimkamata sitashangaa. Binafsi naona tunapohusika binadamu, lolote linaweza kutokea.
 
Ulisikiliza sababu alizozisema mwenyewe dikteta Putin kuivamia Ukraine??
Na kiburi Cha Ukraine kutaka kuwepo na military Base ya US pale wakati miaka ya 1960's USSR walitaka kuweka military Base Cuba,US akapiga kelele nyingi sana kama mbwa koko
 
Labda asilimia 90 ya Warusi wa Buza kwa Mpalange
Mkuu hizi stori tunacomment kuchangamsha tu kijiwe mimi na were tunajua hakuna wa kumkamata mtu yeyote anayetafutwa na yeyote akiwa urusi, na stori za warusi hawamtaki putin pitia tena culture ya warusi.

Julian Assange wa weakleaks angekimbilia Russia asingekamatwa
 
Msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov amesema!! Moscow haina wajibu wa kukiri "hati ya kukamatwa" kwa Rais Vladimir Putin iliyotangazwa na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu siku ya Ijumaa, "Tunachukulia suala hilo kuwa la kuchukiza na halikubaliki," Peskov aliwaambia waandishi wa habari alipoulizwa kuhusu hati ya uhalifu wa kivita unaodaiwa. "Urusi, kama nchi zingine nyingi, haitambui mamlaka ya mahakama hii. Shirikisho la Urusi linachukulia matamko yake yoyote kuwa batili...

source:: RT

Kremlin calls ICC claims ‘absurd and outrageous’

The Hague-based court has no authority in Russia, President Vladimir Putin’s spokesman has said
Moscow is under no obligation to acknowledge the “arrest warrant” for President Vladimir Putin announced by the International Criminal Court on Friday, Kremlin spokesman Dmitry Peskov has said.

“We consider the very premise outrageous and unacceptable,” Peskov told reporters when asked about the warrant for purported war crimes. “Russia, like many other states, does not recognize the jurisdiction of this court. Accordingly, the Russian Federation considers any of its pronouncements null and void from the legal standpoint.”
 
Hujui siasa za kimataifa na hufuatilii

Ataenda kwa usafiri upi wakati ndege zote za Russia zina vikwazo vya Anga Marekani

Pili yeye na familia yake hawaruhusiwi kukanyaga marekani wako blacklisted ulaya na marekani kwa majina yao

Hiyo mahakama ni kichekesho tu kama walimshindwa Albashir wakati katembelea mataifa kibao yakiwemo yenye mlengo wa kimagharibi.

Kama walimshindwa kenyata mpaka akajipeleka yy mwenyewe ndo wataweza kumkamata putin.
 
Apo n kuchezea sharubu za simba mkuu Apa unaongelea mbabe wa dunia Putin Nani huyo mwenye ubavu huo wa kumkamata
 
Lolote linaweza kutokea sawa ila kiuhalisia hiyo mahakama inadharaulika sana.
 
Reactions: Tsh
Kumbuka September 11 halafu uje uongee hapa....bora waliyaua hayo magaidi...

Gaddafi alifadhiri ulipuaji wa ubalozi wa marekani tz na kny
Unaevidence ya unachozungumza?nyie ni wale mlioambiwa Iraq kuna silaha za nuclear mkaamini.hao ni wauaji wameaua watoto na wanawake wa kiarabu na waafrika.
 
Hakuna chochote wanajificha tu kwenye kivuli cha ICC ili wateke mitandao ya kijamii watu wasahau aibu ya drone ya marekan mahakama ile ipo kwa ajili ya Afrika , Amerika ya kusin na mashariki ya kati koitoa Israel maana mimi ndio Marekani lakini hao waliobaki itakua kelele tu ukimgusa putin nadhani ndio itakua mwisho wa hiyo mahakama na ww3 itaanza
 
Kabla ya kuzifikia kivipi? Nuke anayetangulia ndio anakuangamiza na maumivu yake hutaweza kurudisha. Hata ukirudisha kashakuvurumishia jingine utatoboaje?
Haiko hivyo mkuu. Hizo silaha zina uwezo tofauti-tofauti. Kwa mfano hadi sasa hawajaweza kupata kombora (Nuclear missile) moja tu lenye uwezo litakaloweza kuuangamiza mji wote wa Washington au tuseme Nchi yote ya Tanzania kwa mlipuko mmoja.

Kumbuka pia hata mahasimu wa Urusi wanazo silaha hizo za nuklia na zinalindwa kwa kuzingatia Mkataba. Hazipo kwa siri kivile.

Siku zote Taarifa za kiintelijensia zinapatikana mintaaraf usalama wa silaha hizo za maangamizi.
(Mkuu; Ukugoogle utapata kwa undani habari hizi...)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…