Mahakama ya Kisutu imewatia hatiani Viongozi wa CHADEMA na kuwahukumu kulipa faini ya Tsh. Milioni 350 au kwenda jela, Wapelekwa Segerea

Haki itendeke, walioua mwanafunzi kizembe mbona hawajaitwa pia! Kwamba risasi ilipigwa na watu wa Chadema? [emoji41]

Sent using Jamii Forums mobile app
Kesi hii ni miongoni mwa kesi tata,ambapo ofisi ya mwendesha mashitaka DPP inaonekana kupwaya kubariki maelekezo ya kisiasa na kuharibu umoja na ustawi wa taifa letu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni wazi macho ma masikio ya watanzania yapo kisutu kwa sasa. kitakchoamriwa ama kitatoa taswira chanya ama hasi kwa taifa letu ngazi za kimataifa.
 
Wahukumiwe tuu hakuna namana maana wanahatarisha maisha ya vijana wetu kwa kupandikiza chuki

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kwa nini unamlaumu aliyeangukiwa na mti badala ya mkata mti!

Chuki inapandwa na upinzani au na vyombo, taasisi au serikali.

Je hoja zao hazina ukweli? Je hakuna wasiojulikana? Je hawapo waliouawa? Vyombo haviwatambui? Kazi zao hawazioni? Kama wao hawazioni wala kuzisikia je we hukuziona wala kuzisikia? Na kama ndivyo! basi wewe sio mtanzania, na kama sio mtanzania waachie watanzania wajadili mambo yao kwa maendeleo yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati Hakimu Mkazi Mfawidhi, Thomas Simba wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akisoma hukumu ya viongozi 12 wa Cahdema na mmoja wa CCM (Mashinji) wanaokabiliwa na mashktaka ya uchochezi, Jeshi la Polisi limetumia nguvu kuwafurusha wafuasi wa Chadema waliokuwa wamekusanyika mahakamani hapo kufuatilia mwenendo wa kesi hiyo.

Polisi waliagiza wafuasi wote wa Chadema kuondoka kwenye viunga vya mahakama hiyo, lakini waliendelea kukaa wakidai hawajavunja sheria yoyote kwenda kusikiliza hukumu ya viongozi wao. Hata hivyo polisi walitoa amri ya kutawanyika kwa hiari vinginevyo watatumia nguvu. Wafuasi hao walikataa kutawanyika na kuimba kwa hisia "Mkitaka mtuue, mtuue"
_
Baadae polisi wenye silaha za moto, wakisindikizwa na mbwa waliwavamia wafuasi hao kwa kipigo na kuwatawanya wakati hukumu ikiendelea kusomwa ndani ya mahamkama hiyo.!
 
Kwamba wanasiasa hawapaswi kushtakiwa wala kuadhibiwa wakikosea. Haki itendeka Kama hawana hatia waachiwe na kama kweli walitenda makosa hayo waadhibiwe kama Watanzania wengine wanavyoadhibiwa wakikosea!
 
Kwamba wanasiasa hawapaswi kushtakiwa wala kuadhibiwa wakikosea. Haki itendeka Kama hawana hatia waachiwe na kama kweli walitenda makosa hayo waadhibiwe kama Watanzania wengine wanavyoadhibiwa wakikosea!
hakuna mwenye kosa ni kuwaonea tu,,,,... persecution
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…