Mahakama ya Kisutu leo Machi10, inatarajia kutoa hukumu kwa Viongozi wa CHADEMA wanaokabiliwa na kesi ya uchochezi Mahakamani hapo, Viongozi hao ni pamoja na Mwenyekiti CHADEMA, Freeman Mbowe, pia John Mnyika, Halima Mdee, Ester Bulaya, Ester Matiko, Heche, Msigwa na Mashinji.
Katika kesi hiyo inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, vigogo hao wanakabiliwa na mashtaka 13, wakituhumiwa kwa uchochezi, katika kesi iliyoanza kusilikizwa Machi 7, 2018.
Washtakiwa hao wanadaiwa kuwa kati ya Februari Mosi na 16, mwaka 2018, wakiwa Kinondoni jijini Dar es Salaam, kwa pamoja walikula njama na wengine ambao hawapo mahakamani kwa kutenda kosa la jinai na kuendelea na mkusanyiko isivyo halali na kusababisha chuki na uchochezi wa uasi.
UPDATE
4:30 Asubuhi : Hukumu yaahirishwa mpaka saa 7:30 mchana
Awali kesi hiyo ilipangwa kusomwa saa 4:30 wakati washtakiwa wakiwa ndani ya ukumbi, walifahamishwa kupitia kwa Wakili wao Peter Kibatala kuwa muda umesogezwa hadi saa 7:30 mchana.
7:30 Mchana : Hukumu ya kesi imeanza
Hukumu hiyo inasomwa kwenye Mahakama ya wazi na Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba. Ulinzi umeimarishwa ndani na nje ya Mahakama.
Idadi kubwa ya wananchi na wafuasi wa chama hicho wamezuiwa kuingia mahakamani, kutakiwa kutoka nje. Waliamua kukaa chini karibu na mlango mkuu wa kuingia kwenye jengo la Mahakama mpaka Polisi walipowafukuza kwa vitisho. Baadhi yao wamesikika wakiimba nyimbo za kulituhumu Jeshi la Polisi kuwa CCM.
View attachment 1383035
Video: Taswira ya hali ilivyo ndani na nje ya viunga vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu