Mahakama ya Mwanzo ya Buguruni imevunja ndoa ya waliotengana kwa makubaliano ya kila mmoja aende kutafuta watoto

Mahakama ya Mwanzo ya Buguruni imevunja ndoa ya waliotengana kwa makubaliano ya kila mmoja aende kutafuta watoto

Francis12

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2016
Posts
7,533
Reaction score
22,281
Mahakama ya Mwanzo Buguruni imevunja ndoa ya Wanandoa Raymond Kulaya (44) na Magreth Silaeli (37) waliotengana kwa miaka 10 baada ya kukubaliana kila Mtu akatafute Watoto ‘anapopajua’ baada ya kuishi miaka mitano bila kupata Mtoto, kwa sasa Magreth amepata Watoto wanne na Mwanaume mwingine.

Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu Matrona Luanda ambapo amesema Mahakama hiyo iliangalia viini vikuu vitatu ikiwemo kama ndoa ya wawili hao ni halali baada ya kutengana tangu mwaka 2011.

Katika kesi hiyo Magreth aliiomba Mahakama itoe hati ya talaka, ili aolewe na Mwanaume anayeishi nae sasa ambaye amezaa nae, baada ya kutengana kwa muda na Kulaya, wawili hao walifunga ndoa ya Kikristo mwaka 2006 mkoani Kilimanjaro na waliishi pamoja kwa miaka mitano na kudai wakati anaolewa na Kulaya alimkuta tayari na Watoto wawili, lakini katika kipindi chote walichoishi pamoja hawakubahatika kupata watoto.

Alidai mwaka 2011 Mume wake alimueleza kuwa wamekaa kwa muda mrefu bila ya kuwa na Watoto na kumwomba watengane ili kila Mtu aende akatafute Watoto na kusema katika kipindi walichoishi pamoja, Familia ya Ndugu wa Mwanaume ilikuwa inawasumbua kuhusiana na Watoto na kuwasababishia kukosa raha.

Magreth alidai yeye na Kulaya walitengana kwa makubaliano hawakuwahi kuwa na ugomvi na sababu kubwa ya kutengana ilikuwa kukaa muda wa miaka mitano bila ya kupata Mtoto licha ya kwamba Mwanaume alikuwa na Watoto watatu kabla ya kumuoa Magreth.


Pia Soma >> Aeleza walivyokubaliana na mume wake kutafuta watoto nje ya ndoa
 
Aisee! Sasa baada ya miaka kumi mkataba ukiisha mwanamume unarudi huna mtoto ata mmoja mkeo anakuja na vitoto vya wanaume wenzio

Bora tuachane mazima tu aisee, mbaya kabisa hiyo
 
Hapa ilibidi wapigane chini mazima tu. Hakuna cha kwenda na kurudi
IMG-20210313-WA0028.jpg
 
Ni maamuzi mazuri kulingana na umri wao.

Japo kama bado wanapendana wangetafuta staili nyingine kuliko kupata kibali cha mahakama cha kutengana. Sikuhizi mbona Muhimbili wanapandikiza ujauzito?.
 
Kwahiyo hapo aliyekuja kurudi na Watoto Nani !?

Hahahaa Ila dunia inamambo [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Hivi ndoa ya kikristo ya mke/mme mmoja inafaa kuvunjwa na mahakama kisheria au kiimani inakua
Ebana,ndoa yeyote ile hata iwe yachuma itavunjwa/tenganishwa na mahakama ilimradi tu ushahidi upo kujitoshereza
 
Aah asiyejua ni nani, kua mlioana kanisani na mkaachana mahakamani.../

Kwakua ndoa si nyepesi ndoa ni yai, ndoa ni kama kesi ya jinai.../

Ndoa ni hukumu wanasema ndoa ni ngumu jamani ndoa ni sumu, au mpaka mume alete ukimwi nyumbani ndo uamini ndoa si tunu.../

JeSUSTA
 
Jamaa alienda akazaa watoto watatu nje akawa nao jumla 4 ndan ya miaka 10

Mkewe naye akaenda kazaa watoto wann ndan ya miaka hiyo 10[emoji23][emoji23]..hapa mke wajamaa alikua kaamua kuzaaa maana alichekwa sana.

Mke akafungua kesi ya Talaka, ili aoane na waliyezaa naye...Jamaa akawa hataki anataka arudiane mke wake.

Mwenye picha ya mwanamke muiweke hapa Jamani
 
Jamaa alienda akazaa watoto watatu nje akawa nao jumla 4 ndan ya miaka 10



Mkewe naye akaenda kazaa watoto wann ndan ya miaka hiyo 10[emoji23][emoji23]..hapa mke wajamaa alikua kaamua kuzaaa maana alichekwa sana.


Mke akafungua kesi ya Talaka, ili aoane na waliyezaa naye...Jamaa akawa hataki anataka arudiane mke wake.



Mwenye picha ya mwanamke muiweke hapa Jamani
FB_IMG_1615983815852.jpg
 
Aah asiyejua ni nani, kua mlioana kanisani na mkaachana mahakamani.../

Kwakua ndoa si nyepesi ndoa ni yai, ndoa ni kama kesi ya jinai.../

Ndoa ni hukumu wanasema ndoa ni ngumu jamani ndoa ni sumu, au mpaka mume alete ukimwi nyumbani ndo uamini ndoa si tunu.../

JeSUSTA
Kweli kabisa
 
Mke huyoo
 

Attachments

  • Screenshot_20210317-154613_Instagram.jpg
    Screenshot_20210317-154613_Instagram.jpg
    106.3 KB · Views: 3
Back
Top Bottom