Mahakama yatupilia mbali mapingamizi ya utetezi, maelezo ya Mohamed Lingw'enya yapokelewa na Mahakama. Kesi kuu kuendelea Des. 15, 2021


Kuna watu hamuwezi kuelewa vitu before the fact. Na hili la katiba mtakuja kuliekewa baada ya kupata katiba mpya na kuona matatizo yetu bado yako palepale. Katiba hutafisiriwa na kupindishwa kukidhi matakwa ya walioshika hatamu.

Trust me, kwa nafasi ya Rais, hakuna substitute ya uadilifu. Mkipata president ambaye sio muadilifu, hata kama katiba yenu ingekuwa nzuri kiasi gani lazima mtalia. Tambua kwamba presidents wanaochaguliwa kwa kura ya moja kwa moja ya mwananchi are way too powerful na wana kila resource ya kufanya manipulation na kuweza kuiteka ile mihimili mingine. Kumbuka, mihimili yote mitatu ni political. Presidents wana kawaida ya kujitengenezea makundi imara ya allies kwenye mihimili miwili ya mahakama na bunge. Angalia, kwa mfano, Trump alivyoivuruga Marekani. Kimsingi, Trump alikuwa above the law. As you may know, alikuwa impeached mara mbili, lakini kila mara U.S. Senate ilishindwa kumtia hatiani, kwa sababu alikuwa na allies wa kutosha. Aliyeiokoa Marekani isitumbukie kwenye full dictatorship ni Mike Pence, ambaye alikataa kufuata utashi wa Trump, wa kukataa kuzipokea electoral votes za key swing states. Kama VP angekuwa Rudy Giuliani, with Trump, Marekani ilikuwa imeingia mkenge usio wa kawaida.
 
Seriously? Kuhudhuria tangu lini kumekuwa interference? Kwani mnaogopa wataona nini?

Amandla...

Kabisa! Hiyo ni diplomatic pressure, kwasababu sio customary kwa diplomats kuhudhuria kesi za raia wa host country. Mahakama zetu zina maelfu ya kesi zingine za jinai ambazo ziko kwenye mchakato wa kusikilizwa, lakini hakuna diplomat anayehangaika kuzifuatilia.
 
My friend, you are nuts! Unashabikia Katiba ya Kenya kuwa CJ anaomba kazi kama tunavyoomba ukarani ? You do not know what you are talking about and are clueless about who it is you are tslking about. Ni nani anayemfanya interview katika Wakenya milioni 43? Maybe 5 or 6, sasa hujui hawo interviewers ni kina nani.

Kenya kuna Ukabila wa kutupwa, more ingrained kuliko uccm wetu au uchadema wetu, allegiance kwa makabila is total. It is very fortunate that they are small and equal - dholuo 1.3m hata ukihesabu na kina Heche wana mke huku na huku; Gikuyu wakiwemo Wameru na Wamasai huko huitwa Maasai) 1.5m ; Abaluhya 2m (kina mudavadi, wako wengi hadi Yuganda); kalenjin (na pokot, suk na kipsigis, bonde la ufa) ni 1.7m; Mijikenda (pwani, wagiriama, wadigo hadi Chumbageni, na shifta wa garissa), jumla ni 1m. Akamba (kina Kilonzo Musyoka, wakiwemo Wapare wetu) jumla ni laki 9 tu.

Ili upate 50%+1 uwe Rais, lazima uwe na kabila 7. Ndiyo maana BBI ya Raila ina figurehead President mmoja na Vice-Presidents 2. Exceutive head ni PM, naye ana Vice Premiers 4. Jumla 7 so that kila "kabila tawala" lina mtu wake ale "jikoni". Serkali ni "Counties", Majimbo, kama wanayotaka CHADEMA, kila Jimbo na Mangi wake huitwa Governor.

So, hiyo Application Form yako eti ya kuwaomba uwe Jaji ni daganyatoto tu, wachana nay What matters ni kabila lako, kama huna huna!

Kwa uzoefu wangu (I've seen a fair bit of the world), Tanzania has got the best Constitution in the world. It has the most representative Parliament in the world. We have one of the, if not the, most independent Judiciary(s) in the world, certainly better than the US where each President appoints his own kind each time there is a vacancy (i.e., mmoja akifa, they die in the office, hawastaafu). Ours is better than the German one that gassed 6m Jews (that equals 2 and a half Israels of today) and 3m Russians - whatever they say NOW. It is better than the Australian one that butchered the Aborigines or the Canadian one which murdered the Eskimos. In Africa it is better than that of Chad and Benin snd Tunisia or Congo or Djibouti that you don't even now.

Who gets the credit? ZFZMWCCM, of course.
 
 

Nilichoandika mimi na ulichoandika wewe vina uhusiano gani, mzee mzima?
 
Ukabila ni tatizo la kijamii na haliondolewi kupitia katiba.Katiba ya nchi inashughulika na mienendo na shughuli za nchi kiserikali kwa maana ya siasa na wajibu.sasa sijui ukabila wa kenya unahusikaje na katiba yao.
 
Pressure kwa nani? Serikali au Mahakama? Mahakama si iko huru? Jaji ndio muamuzi wa mwisho katika kesi na suala la nani anamsikiliza halipaswi kumstua. Hivi kweli unalinganisha kesi za wizi wa kuku na kesi ya Mwenyekiti wa chama kikubwa cha upinzani!
Hii ni opportunity ya Mahakama kuonyesha kuwa iko juu ya siasa. Kwa mawazo yangu Mahakama ilitakiwa kuirusha live au kuistream kwenye social media kuwahakikishia watanzania kuwa haki inatendeka. Mabalozi nao na dunia nzima wangeweza kuangalia ili kukata mzizi wa fitna.

Amandla...
 
Huwezi Ukafuta Utaifa, Ukabila, na Lugha!
Ndio sababu hata nyani wa India ni Muhindi na nyani wa Afrika ni Mwafrika!
 

Pressure kwa JMT, ambaye ndiye mlalamikaji. Mbowe hajashitakiwa katika capacity yake ya mwenyekiti wa CDM. Ni kesi ya jinai kama kesi zingine za jinai. Kesi ya Mbowe sio high profile case ya kwanza kusikilizwa na mahakama zetu. Raia wote wa Tanzania wanayo haki ya kupata equal treatment mbele ya sheria; hatupaswi kuwa na first-class citizens wala second-class citizens. Kama hatufanyi streaming kwa kesi zingine, hakuna sababu ya kufanya streaming kwa kesi hii moja tu!
 
ahsante sana Mkuu kwa kueleza kwa ufasaha.
naamini wafuasi wa Mbowe watakuwa wamekuelewa.

umeongelea suala la "Rule of Law" ktk lugha nyepesi na rahisi zaidi.
 
Nakubali Hanna imani na Mahakama ya Tanzania. Nakumbuka baada ya Uchaguzi Mkuu, baadhi ya wafuasi na wapenzi wenu walienda kufungua kesi The Hague mnapopaamini. Hivi hizo kesi ziliishia wapi? Ahahahahahahahah!!!
 
Nakubali Hanna imani na Mahakama ya Tanzania. Nakumbuka baada ya Uchaguzi Mkuu, baadhi ya wafuasi na wapenzi wenu walienda kufungua kesi The Hague mnapopaamini. Hivi hizo kesi ziliishia wapi? Ahahahahahahahah!!!

Yap hatuna imani na hizo mahakama za Makada wa CCM, zile kesi za the Hague ziliishia ilipoishia Tanzania ya viwanda.
 
You’re right, hiyo sio kazi ya diplomatic missions. Ni interference ya wazi kwenye internal affairs za host country!
tena interference kwa mahakama, interference kwenye uhuru wa mahakama/rule of law, wakati siku zote huwa wanahubiri respect of the rule of law, ila wao wanavunja, wanaingilia mahakama. hapo ndio utaona unafiki wa wazungu.
 
..Ujerumani wametupa fedha kuboresha mifumo yetu ya sheria. Pia wamekuwa wafadhili wakubwa wa kitivo cha sheria Udsm. Kwa hiyo lazima wafuatilie kinachoendelea.
mifumo ipi ya sheria? majengo ya mahakama yanafadhiliwa na world bank. taja hiyo mifumo ya sheria iliyoboreshwa na wajerumani? kwanza hao walitutawala halafu wanataka kuleta ujinga ningekuwa rais wangenitambua.
 
mifumo ipi ya sheria? majengo ya mahakama yanafadhiliwa na world bank. taja hiyo mifumo ya sheria iliyoboreshwa na wajerumani? kwanza hao walitutawala halafu wanataka kuleta ujinga ningekuwa rais wangenitambua.

..kuna mapitio ya sheria yanafanyika sasa hivi yanafadhiliwa na Ujerumani.

..wakoloni weusi wa Tanu na Ccm wametawala kwa muda mrefu kuliko Wajerumani.
 
Sina uhakika kama unaelewa hoja. Kwanza, hakuna katiba 100% duniani zipo zinazokidhi mahitaji 80-90%

Katiba iliyotengenezwa kwa umakini inaziba mianya ya hovyo na kutoa mwelekeo
Katiba haitarajiwi ku solve kila tatizo bali ni msingi wa mifumo (systems) za nchi

Mfano:
-India imewahi kukaa miezi 3 bila Waziri mkuu na nchi ilikuwa salama
-Uingereza ambayo haina katiba iliyoandikwa ilikaa wiki 3 bila Waziri mkuu , salama salimini
-Germany majuzi wamekaa wiki 3 kutafuta muafaka wa nani aongoze baada ya kutopatikana mshindi wa moja kwa moja. Ndivyo ilivyo kwa Israel n.k.

Nchi hizo hazikufanikiwa kwa kubahatisha, ni mifumo ya nchi imara na taasisi zake

Kwa nchi yetu ni tofauti.
Rais anamuondoa CAG kinyume cha sheria kwasababu hakuna chombo kitakachomhoji
Spika ''anawajibika'' kwa Rais kwasababu Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama anaweza kumuondoa kwa kupitia ''caucus' au kamati za chama.
CJ anateuliwa na Rais na tumeona kituko cha CJ kuwekwa probation na mhimili wa serikali
NEC inateuliwa na Rais na ndiye anatangaza matokeo ya 'mechi' ya Rais na watu wengine
Msajili wa vyama anateuliwa na kuondolewa na Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama
DPP, DCI na Takukuru wanateuliwa na Rais na Takukuru ipo chini ya ofisi ya Rais
Waziri mkuu na VP wote ni wateuliwa wa Rais
Vyombo vyote vya ulinzi na usalama vipo chini yake
Orodha inaendelea hadi kwa maDC na Wakurugenzi wa Halmshauri

Katika hao hakuna 'checks and balances'' . Sauti ya Mwananchi kama mwenye nchi ipo wapi?
Rais ana 'absolute power'

Kautokana na absolute power Rais anaweza ku manipulate pillars na institution za nchi.
Mfano, kuteua majaji na kisha kuweza kuwateua tena baada ya kustaafu kwa kazi nyingine kuna ''compromise'' utendaji wa mahakama na utoaji haki.

Kuhusu US, kuna kitu husemi. Kwamba, Trump amekuwa impeached twice. Matokeo ya impeachment hayahusiani na process. Clinton alitenda kosa lakini halikumuondoa madarakani
Usichanganye kati ya ''process na results''

Pence kukataa ilikuwa kuhofia sheria. Hata leo wanaokataa wito wa kamati za Bunge wanashtakiwa, asikudanganye mtu Trump hakutaka kuondoka lakini mifumo ilikuwa tayari kumbeba akakimbia.

Hebu angalia Biden anavyosumbuka na Senate na House katika kupata pesa au kupitisha miswada
Hata national debt inajadliwa, vipi sisi tunajua nini kuhusu national debt zaidi ya kuona namba?

Kesi ya Mbowe ni muhimu na yenye heri sana, afadhali imetokea. Watu wasioelewa wanaelewa sasa na kila siku matundu yanaonekana. Mhimili wa sheria unapotiliwa shaka haki itapatikana wapi? Kama hakuna haki upendo na amani vinatokeaje?
 

Nadhani unaishi kwenye dunia ya kufikirika. Strength ya katiba (na hata ya sheria) bila watawala waadilifu doesn’t exist. Kama Mike Pence angekosa huo uadilifu, Marekani ilikuwa imegota. Hakuna Ibara ya US Constitution inayoilazimisha US Senate kuthibitisha electoral votes za state yoyote. Kama VP (ambaye ndiye president of the US Senate) na US Senate yake wangeamua kuzikataa electoral votes za swing states, Marekani ilikuwa haina ujanja wowote zaidi ya kuwa kwenye impasse ambayo ingempa Trump excuse ya kutangaza state of emergency. Department of Justice (ambayo kimsingi ndiyo ina dhamana ya kulinda rule of law) ni toothless linapokutana na president mhuni kama Trump. Uliona jinsi alivyomtumbua then AG Jeff Sessions kwasababu tu alijiengua katika kusimamia uchunguzi wa interference ya Russia katika US General Election ya 2016. Uliona pia alivyomtumbua then FBI Director James Comey. Where were the US Constitution and Laws when this occurred?

Asikudanganye mtu, ni nchi chache sana ambazo zina judges na CAG ambao sio wateule wa Rais au Prime Minister. Kuwa mteule wa Rais au Prime Minister sio tatizo, provided the appointing authority ni muadilifu. Mahakama nayo ni political institution yenye vulnerabilities zote za political institutions. A rogue president can easily engineer the removal of a strong CJ (hata kama huyo CJ sio mteule wa Rais). Rais anazo resources za kila aina kuwezesha hili kufanyika.

Narudia tena, kwa nafasi ya Rais, hakuna substitute ya uadilifu! Ni sawa tu na jinsi crimes zingine zinavyoendelea kuwepo hata baada ya nchi kuwa na sheria zinazotoa adhabu kali, including the death penalty. Kwa mtu muadilifu, ukimuambia “having an affair with a schoolchild is illegal” inatosha kabisa. Kwa yule ambaye sio muadilifu, hata ukimuambia “the penalty for having an affair with a schoolchild is 30 years of prison time” haitoshi; bado atafanya tu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…