Maharage Chande kutoka Ukurugenzi TANESCO hadi Postamasta - amepanda au ameshuka?

Maharage Chande kutoka Ukurugenzi TANESCO hadi Postamasta - amepanda au ameshuka?

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Umofia kwenu

Uteuzi uliofanywa na Rais Samia kwa kumtoa Maharage Chande TANESCO na kumpeleka kuwa Mkurugenzi TTCL na hatimaye ndani ya siku mbili akamteua kuwa PostaMasta inaleta tafakuri jadidifu kidogo.

Sisi wanaNzengo tunaweza kuwa na maswali yanayosumbua bongo zetu

  1. Cheo cha Postamsta kina nafasi gani kwenye madaraja ya utumishi wa umma?
  2. Sababu zilizosababisha aondolewe TANESCO zinafanana na zilizopelekea aondolewe TTCL?
  3. Mteuzi yaani Rais, anatuma ujumbe gani kwa umma kwa teuzi hizi kanganyifu? Yaani leo unamteua huyu unamuweka mahala fulani lakini kesho yake unamuondoa hapo kumpeleka kwingine
  4. PostaMasta anafanyakazi chini ya Mkurugenzi wa Posta. Je kwa level aliyofikia Maharage Chande inampa hadhi hiyo ama inamshusha hadhi awe hivyo?
  5. Kama endapo kuna sababu zinazoligharimu Taifa kwa kumuondoa Chande TANESCO, je aendelee kuligharimu Taifa huko aendako au alipata ajali ta kiutendaji?
  6. Je tuendelee kuamini kwamba Rais yupo makini kusimamia utumishi wa umma au anatekeleza matakwa ya waliomzunguka bila kuzingatia manufaa ya Umma?
  7. Je, CCM sasa inatapatapa kulazimisha maji kupanda mlima baada ya kukosa kuungwa mkono na wananchi ambapo kupitia kauli za makada waandamizi kwamba hata ikishindwa uchaguzi haiondoki madarakani?
  8. Kwa utendaji huu wenye mashaka mengi wa marais wa CCM l, je ni mara ngapi CCM imeipindua serikali kwa kuiba matokeo ya chaguzi mbalimbali nchini?
  9. Mkeka wa teuzi wa jana, umeonesha uwepo wa ombwe la utumishi wa umma. Tutarajie nini kwenye utendaji wenye kuleta matokeo?
CC: Pascal Mayalla Erythrocyte Retired Mshana Jr johnthebaptist Kidu52 Money Penny Dr Akeelah masa2000 Kigogo333 raraa reree Extrovert FaizaFoxy ChoiceVariable Lucas mwashambwa
 
Hayatuhusu, watajuana wenyewe.

Mimi hata leo sijui nitakula nini, hivyo mbuzi ni mali ya bwana Abdul amekula kwenye shamba la Abdul.
Chawa fulani mwandamizi amesema.kuwa Watanzania mna imani na matumaini makubwa kwa Hangaya. Sasa kusema hujui utakula nini inaleta ukakasi sana kwenye uaminifu kwake😀

Au nasema.uongo bw Lucas mwashambwa ?
 
Sababu zilizosababisha aondolewe TANESCO zinafanana na zilizopelekea aondolewe TTCL?

Sio kwamba sababu "zinafanana." Sababu ni zile zile. Watu wengi waliomba asiendelee kuwepo pale TTCL kwa sababu zile zile zilizomtoa TANESCO.

Huko Posta hakuna kukuru kakara zilizoko TTCL na TANESCO. Sasa amepangiwa eneo la kazi linaloonekana kwendana na uwezo wake wa kufikiri, kuhukumu na kutenda.

Rais amefanya uamuzi sahihi na kwa wakati sahihi. Pia, Rais amejisahihisha haraka.

Kwangu naona hatua zote mbili za sasa ni za kupongezwa.

TTCL is dying my friend!

It needs a strategic-cum-micro-manager, which Maharage is not and has never been!
 
Sio kwamba sababu "zinafanana." Sababu ni zile zile. Watu wengi waliomba asiendelee kuwepo pale TTCL kwa sababu zile zile zilizomtoa TANESCO.

Huko Posta hakuna kukuru kakara zilizoko TTCL na TANESCO. Sasa amepangiwa eneo la kazi linaloonekana kwendana na uwezo wake wa kufikiri, kuhukumu na kutenda.

Rais amefanya uamuzi sahihi na kwa wakati sahihi. Pia, Rais amejisahihisha haraka.

Kwangu naona hatua zote mbili za sasa ni za kupongezwa.

TTCL is dying my friend!

It needs a strategic-cum-micro-manager, which Maharage is not and has never been!
Umemaliza kila kitu
 
Sio kwamba sababu "zinafanana." Sababu ni zile zile. Watu wengi waliomba asiendelee kuwepo pale TTCL kwa sababu zile zile zilizomtoa TANESCO.

Huko Posta hakuna kukuru kakara zilizoko TTCL na TANESCO. Sasa amepangiwa eneo la kazi linaloonekana kwendana na uwezo wake wa kufikiri, kuhukumu na kutenda.

Rais amefanya uamuzi sahihi na kwa wakati sahihi. Pia, Rais amejisahihisha haraka.

Kwangu naona hatua zote mbili za sasa ni za kupongezwa.

TTCL is dying my friend!

It needs a strategic-cum-micro-manager, which Maharage is not and has never been!
Sasa amepangiwa eneo la kazi linaloonekana kwendana na uwezo wake wa kufikiri, kuhukumu na kutenda.[emoji419][emoji375]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngongole ! Mh rais Ila bado una kazi mbele wengi unaowamini kukusaidia wanaweka maslahi yao mbele badala ya maslahi ya taifa wanafanya wananchi wa Tanzania wapagazi wao
 
Tarehe 21/9/2023 Mkurugenzi Wa TANESCO - Maharage Chande

Tarehe 23/9/2023 Mkurugenzi Wa TTCL - Maharage Chande

Tarehe 25/9/2023 Mkurugenzi Wa POSTA - Maharage Chande

Kuna Shida Kubwa Kwenye Mamlaka Ya Uteuzi... Kuna SHIDA KUBWA SANA

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo ni kubwa sana.
Huko ndani kuna kugawanyika kutikana na ideologies na utamaduni aliouanzisha Mkapa
 
Back
Top Bottom