Maharage Chande kutoka Ukurugenzi TANESCO hadi Postamasta - amepanda au ameshuka?

Maharage Chande kutoka Ukurugenzi TANESCO hadi Postamasta - amepanda au ameshuka?

Fvc
Umofia kwenu

Uteuzi uliofanywa na Rais Samia kwa kumtoa Maharage Chande TANESCO na kumpeleka kuwa Mkurugenzi TTCL na hatimaye ndani ya siku mbili akamteua kuwa PostaMasta inaleta tafakuri jadidifu kidogo.

Sisi wanaNzengo tunaweza kuwa na maswali yanayosumbua bongo zetu

  1. Cheo cha Postamsta kina nafasi gani kwenye madaraja ya utumishi wa umma?
  2. Sababu zilizosababisha aondolewe TANESCO zinafanana na zilizopelekea aondolewe TTCL?
  3. Mteuzi yaani Rais, anatuma ujumbe gani kwa umma kwa teuzi hizi kanganyifu? Yaani leo unamteua huyu unamuweka mahala fulani lakini kesho yake unamuondoa hapo kumpeleka kwingine
  4. PostaMasta anafanyakazi chini ya Mkurugenzi wa Posta. Je kwa level aliyofikia Maharage Chande inampa hadhi hiyo ama inamshusha hadhi awe hivyo?
  5. Kama endapo kuna sababu zinazoligharimu Taifa kwa kumuondoa Chande TANESCO, je aendelee kuligharimu Taifa huko aendako au alipata ajali ta kiutendaji?
  6. Je tuendelee kuamini kwamba Rais yupo makini kusimamia utumishi wa umma au anatekeleza matakwa ya waliomzunguka bila kuzingatia manufaa ya Umma?
  7. Je, CCM sasa inatapatapa kulazimisha maji kupanda mlima baada ya kukosa kuungwa mkono na wananchi ambapo kupitia kauli za makada waandamizi kwamba hata ikishindwa uchaguzi haiondoki madarakani?
  8. Kwa utendaji huu wenye mashaka mengi wa marais wa CCM l, je ni mara ngapi CCM imeipindua serikali kwa kuiba matokeo ya chaguzi mbalimbali nchini?
  9. Mkeka wa teuzi wa jana, umeonesha uwepo wa ombwe la utumishi wa umma. Tutarajie nini kwenye utendaji wenye kuleta matokeo?
CC: Pascal Mayalla Erythrocyte Retired Mshana Jr johnthebaptist Kidu52 Money Penny Dr Akeelah masa2000 Kigogo333 raraa reree Extrovert FaizaFoxy ChoiceVariable Lucas mwashambwa
Fvck "utumishi wa umma"

Anybody helping government with anything got no respect atleast from me!
 
Je Magufuli aliwezaje bila kuleta mgao na wakati huo huo mvua dusko zilikuwa zinaleta ukavu?

Je Magu alitudanganya kuwa wanafungulia maji ili kutengeneza punguzo la maji kwenye mabwawa kwa minajili ya biashara zao?
Kipindi kile mambo mengi " hasi" yalikuwa hayafiki magazetini. Nyakati hazifanani kukiwa na mvua mabwawa ya umeme yanakuwa hayana shida, kama vyanzo vyetu vya umeme vitabaki kutegemea maji ya mvua hatuwezi kusonga mbele, matatizo ya umeme yatazidi kuongezeka kwakuwa, viwanda vipya vinajengwa na matreni ya umeme karibu yataanza kazi.
 
Kipindi kile mambo mengi " hasi" yalikuwa hayafiki magazetini. Nyakati hazifanani kukiwa na mvua mabwawa ya umeme yanakuwa hayana shida, kama vyanzo vyetu vya umeme vitabaki kutegemea maji ya mvua hatuwezi kusonga mbele, matatizo ya umeme yatazidi kuongezeka kwakuwa, viwanda vipya vinajengwa na matreni ya umeme karibu yataanza kazi.
Wewe na Rais nani mkweli? I mean rais Magu
 
Umofia kwenu

Uteuzi uliofanywa na Rais Samia kwa kumtoa Maharage Chande TANESCO na kumpeleka kuwa Mkurugenzi TTCL na hatimaye ndani ya siku mbili akamteua kuwa PostaMasta inaleta tafakuri jadidifu kidogo.

Sisi wanaNzengo tunaweza kuwa na maswali yanayosumbua bongo zetu

  1. Cheo cha Postamsta kina nafasi gani kwenye madaraja ya utumishi wa umma?
  2. Sababu zilizosababisha aondolewe TANESCO zinafanana na zilizopelekea aondolewe TTCL?
  3. Mteuzi yaani Rais, anatuma ujumbe gani kwa umma kwa teuzi hizi kanganyifu? Yaani leo unamteua huyu unamuweka mahala fulani lakini kesho yake unamuondoa hapo kumpeleka kwingine
  4. PostaMasta anafanyakazi chini ya Mkurugenzi wa Posta. Je kwa level aliyofikia Maharage Chande inampa hadhi hiyo ama inamshusha hadhi awe hivyo?
  5. Kama endapo kuna sababu zinazoligharimu Taifa kwa kumuondoa Chande TANESCO, je aendelee kuligharimu Taifa huko aendako au alipata ajali ta kiutendaji?
  6. Je tuendelee kuamini kwamba Rais yupo makini kusimamia utumishi wa umma au anatekeleza matakwa ya waliomzunguka bila kuzingatia manufaa ya Umma?
  7. Je, CCM sasa inatapatapa kulazimisha maji kupanda mlima baada ya kukosa kuungwa mkono na wananchi ambapo kupitia kauli za makada waandamizi kwamba hata ikishindwa uchaguzi haiondoki madarakani?
  8. Kwa utendaji huu wenye mashaka mengi wa marais wa CCM l, je ni mara ngapi CCM imeipindua serikali kwa kuiba matokeo ya chaguzi mbalimbali nchini?
  9. Mkeka wa teuzi wa jana, umeonesha uwepo wa ombwe la utumishi wa umma. Tutarajie nini kwenye utendaji wenye kuleta matokeo?
CC: Pascal Mayalla Erythrocyte Retired Mshana Jr johnthebaptist Kidu52 Money Penny Dr Akeelah masa2000 Kigogo333 raraa reree Extrovert FaizaFoxy ChoiceVariable Lucas mwashambwa
Wewe unadhani kwanini Yuda Iskarioti japo Mitume wote walimjua kuwa ni mwizi lakini Yesu hakumtumbua hadi mwisho wa Utumishi wake hapa Duniani?
 
Kuna yule aliyeteuliwa sijui ilikuwa ni nafasi gani hakuingia hata ofisini akahamishwa tena

Sent using Jamii Forums mobile app
Alirudishwa kutoka U.N office New York akateuliwa na kuapishwa siku ja ijumaa kama katibu mkuu wa Foreign na jumatatu kabla ya kuingia ofisini mambo ya nje akatenguliwa na kupewa kazi ya naibu mwanasheria mkuu!!
Ni dhahiri Samia hawajui anaowateua hivyo hupelekewa majina na kuteua bila kuhakiki kuwa. Wamefanyiwa thorough vetting!
Samia anasema amemuhamisha Maharage kutoka TTCL kwenda Posta kuepusha “conflict of interest “ ya Maharage na biashara zake! Je ana uhakika gani kuwa hatakuwa na conflict of interest huko Posta?
Mama Abdul hiyo kazi imemzidi nguvu akubali yaishe tu hao wapambe wanalinda maslahi yao na sio ya nchi!
 
Huyo alitakiwa awe gerezani kwa ufisadi waliofanya Tanesco ila kwasababu ngao yao kikwete maana wanapangiwa tu
Maharage na January wanatakiwa wahojiwe kuhusu mkataba wa software worth billions of shillings waliosaini na kampuni ya kihindi!
Mkataba ule unanuka rushwa ya dhahiri kabisa.
 
Back
Top Bottom